Thursday, August 18, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa China nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Youqing alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Agosti, 2016. Mazungumzo yao yalijikita katika kujadili masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na China na taratibu zinazoendelea kwa upande Serikali za kuhamia Dodoma. 
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Mbelwa Kairuki pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Halmenshi Lunyumbu wakifuatilia mazungumzo. 
Mazungumzo yakiendelea

Wakiwa katika  picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.