Wednesday, August 10, 2016

Waziri Mahiga akutana na Waziri wa Mambo ya Nje mstaafu wa China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akutana na kufanya mazungumzo na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Zhaoxing ambaye ameongoza ujumbe kutoka Taasisi ya Diplomasia ya Umma ya China. Ujumbe huo upo nchini kwa ajili ya kuhamasisha  ushirikiano katika masuala ya Habari na Mawasiliano hususan kupitia vyombo vya habari ambavyo ni msingi katika kueleimisha umma masuala mbalimbali ya maendeleo.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Mhe. Zhaoxing ukifuatilia mazungumzo kati yake na Mhe. Waziri Mahiga
Sehemu nyingine ya ujumbe kutoka China.
Mhe. Zhaoxing naye akimweleza jambo Mhe. Waziri Mahiga
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasilino ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Halmenshi Lunyumbu wakinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Waziri Mahiga na Mhe. Zhaoxing (hawapo pichani).
Waziri Mahiga akimkabidhi zawadi ya Kahawa na Majani ya Chai yanayozalishwa nchini 
Waziri Mahiga na Mhe. Zhaoxing na wajumbe wengine waliohudhuria mkutano wakiwa katika picha ya pamoja. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.