Wednesday, August 24, 2016

Rais Shein afungua Kongamano la 3 la Watanzania waishio Ughaibuni.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akizungumza katika ufunguzi wa Kongamano la tatu (3) la Diaspora lililofanyika katika Hotel ya Zanzibar Beaach Resort Visiwani Zanzibar, 24 Agosti, 2016.
Kongamano hilo ambalo linafanyika kwa mara ya kwanza visiwani Zanzibar limehudhuria na Watanzania wanaoishi nje ya nchi wapatao 342 na kushirikisha Taasisi na Idara za Serikali, Sekta binafsi na makundi ya wafanyabiashara.
Mhe. Dkt. Shein akiendelea kuzungumza
Naibu Katibu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi (wa pili kushoto) akiwa pamoja na Mkururugenzi wa Idara ya Diaspora Balozi Anisa Mbega (wa kwanza kulia ), Balozi Mohamed Mahundi (wa tatu kutoka kushoto) na Balozi Charles Sanga wakifuatilia kongamano kwa makini.
Mkurugenzi wa Idara ya Wizara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Silima Kombo Haji (wa tatu kutoka kulia),  na washiriki wengine wakifuatilia Kongamano.
Waziri wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Haji Ussi Gavu akitoa taarifa fupi ya kongamano la Diaspora pamoja na kumshukuru Mhe, Rais Shein kwa kuitikia wito wa kuwa mgeni Raismi na kufanya ufungunzi, sambamba na kumkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushiriki katika kongamano hilo pamoja na viongozi wengine walioshiriki katika Kongamano la tatu la Diaspora. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akihutubia katika Kongamano hilo ambapo aliwapongeza washiriki wote kwa kushiriki pamoja na kueleza nafasi ya diaspora katika kutumia fursa za uwekezaji zilizopo ili kuiletea Tanzania maendeleo.
Mwakilishi wa Watanzanzania wanaoishi ya Nje ya nchi ambaye aliishi ughaibuni kwa muda mrefu na baadae kurejea nchini Bw. Hussein M. Nyang'anyi akitoa taarifa katika Kongamano hilo. Bw. Nyang'anyi alitoa shukurani kwa Serikali kwa kuweza kuandaa Kongamano hilo kila mwaka na kuweza kuwakutanisha Watanzania waishio nje ya Nje, waliopo nchini na viongozi wakuu wa Serikali kwa lengo la kupeana taarifa na kupeana uzoefu katika masuala wa maendeleo hasa katika sekta ya Uwekezaji na Biashara.
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akiratibu katika kongamano la tatu (3) la Diaspora, linalofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort.
Sehemu ya washiriki wakiendelea kufuatilia mkutano wa pili kutoka kushoto ni Konseli Mkuu Dubai Bw. Mwadini   Wizara ya Mambo ya nje wakifuatilia Kongamano.
Sehemu ya Wawezeshaji walioshiriki katika Kongamano na kutoa mada mbalimbali wakifuatilia Kongamano
Sehemu nyingine ya Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na washiriki wengine wakifuatilia Kongamano
Kutoka kushoto ni Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Adolf Mchemwa pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Hangi Mgaka na washiriki wengine wakifuatilia Kongamano
Sehemu nyingine yamaafisa wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Kongamano
Mkutano ukiendelea
Viongozi wa meza kuu wakiwa wamesimama wakati nyimbo za Taifa zikipigwa
Washiriki wakiwa wamesimama wakati nyimbo za Taifa zikipigwa
Bendi ya Jeshi la Polisi (Brass Band) wakipiga nyimbo za Taifa katika Kongamano
Mhe. Rais Shein akijadili jambo na Mhe. Waziri Mahiga mara baada ya kumaliza ufunguzi wa Kongamano
Picha ya Pamoja ya mgeni Rasmi Mhe. Dkt. Shein na meza kuu.
Picha ya pamoja ya meza kuu pamoja na wawezeshaji walioshiriki katika Kongamano

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.