Wednesday, August 31, 2016

Mkurugenzi wa Idara ya Asia akutana na Mwakilishi masuala ya Uchumi Ubalozi wa China

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbelwa Kairuki (kulia) akizungumza na  mwakilishi wa masuala ya Uchumi na Biashara wa Jamhuri ya Watu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw.Li Zhiyong ambaye alimtembelea katika Ofisi za Wizara tarehe 31 Agosti, 2016.
 Mazungumzo yao yalijikita katika kujadili maandalizi ya mkutano wa 5 wa Kamati ya Pamoja ya Uchumi, Biashara, Uwekezaji na Ushirikiano wa masuala ya Teknolojia  kati ya Tanzania na China unaotarajiwa kufanyika nchini   tarehe 13 Oktoba, 2016.
Maafisa wa Ubalozi wa China wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mbelwa na Bw. Zhiyong (hawapo pichani)
Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.