Tuesday, August 2, 2016

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Japan nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akizungumza na Balozi wa Japan nchini Mhe. Masaharu Yoshida alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo Mhe. Waziri alieleza mafanikio yaliyopatikana kupitia miradi ya ushirikiano na Serikali ya Japan hususan miradi ya miundombinu na Sekta ya Elimu. 
Balozi wa Japan nchini, Mhe. Masaharu Yoshida akieleza nia ya Serikali ya Japan katika kuimarisha ushirikiano hususan katika kuhakikisha utekelezaji wa majukumu unaenda sambamba na kasi ya utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Bertha Makilagi (kushoto) pamoja na Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.