Thursday, August 4, 2016

Waziri Mahiga akutana na Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill na Melinda ya Marekani

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Mwakilishi kutoka Taasisi ya Bill na Belinda Gates ya Marekani, Bi. Rosita Najmi. Katika mazungumzo yao Waziri Mahiga alimweleza Bi. Najmi kuwa Tanzania inathamini mchango unaotolewa na Taasisi ya Bill na Melinda katika miradi mbalimbali  ikiwemo kuboresha sekta ya afya na kilimo kwa maendeleo ya Taifa.
 Bi. Rosita  akimwelezea namna Taasisi hiyo ilivyojipanga kuendelea kushirikiana na Tanzania.
Bw. John Ndunguru, Afisa wa Program kutoka Taasisi ya Bill na Melinda naye akichangia jambo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kulia) akiwa na  Bi. Ramla Hamis (katikati) na Bi. Prisca Mwanjesa, Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia  mazungumzo ya Dkt. Mahiga na Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill na Belinda Gates (hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea
Picha ya pamoja .

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.