Thursday, August 18, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Israel nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Israel nchini Mhe. Yahel Vilan alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam leo tarehe 18 Agosti, 2016. Katika mazumgumzo yao walijadili namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya mataifa yao hususan katika sekta za Kilimo, Elimu na Masuala ya kuwawezesha Wanawake katika kufikia maendeleo.
Mhe. Yahel akimweleza Waziri Mahiga namna Serikali ya Israel ilivyofanikiwa katika miradi ya kilimo na umwagiliaji ambayo imesaidia katika kuwahakikishia wananchi wake upatikanaji wa chakula.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Abdallah Kilima (wa kwanza kushoto) pamoja na Maafisa  Mambo ya Nje  Bw. Hangi Mgaka (wa pili kushoto) na Bi. Kisa Doris Mwaseba wakifuatilia mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea
Wakijadili jambo mara baada ya mazungumzo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.