Wednesday, August 24, 2016

Rais Shein afungua Kongamano la 3 la Watanzania waishio Ughaibuni.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akizungumza katika ufunguzi wa Kongamano la tatu (3) la Diaspora lililofanyika katika Hotel ya Zanzibar Beaach Resort Visiwani Zanzibar, 24 Agosti, 2016.
Kongamano hilo ambalo linafanyika kwa mara ya kwanza visiwani Zanzibar limehudhuria na Watanzania wanaoishi nje ya nchi wapatao 342 na kushirikisha Taasisi na Idara za Serikali, Sekta binafsi na makundi ya wafanyabiashara.
Mhe. Dkt. Shein akiendelea kuzungumza
Naibu Katibu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi (wa pili kushoto) akiwa pamoja na Mkururugenzi wa Idara ya Diaspora Balozi Anisa Mbega (wa kwanza kulia ), Balozi Mohamed Mahundi (wa tatu kutoka kushoto) na Balozi Charles Sanga wakifuatilia kongamano kwa makini.
Mkurugenzi wa Idara ya Wizara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Silima Kombo Haji (wa tatu kutoka kulia),  na washiriki wengine wakifuatilia Kongamano.
Waziri wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Haji Ussi Gavu akitoa taarifa fupi ya kongamano la Diaspora pamoja na kumshukuru Mhe, Rais Shein kwa kuitikia wito wa kuwa mgeni Raismi na kufanya ufungunzi, sambamba na kumkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushiriki katika kongamano hilo pamoja na viongozi wengine walioshiriki katika Kongamano la tatu la Diaspora. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akihutubia katika Kongamano hilo ambapo aliwapongeza washiriki wote kwa kushiriki pamoja na kueleza nafasi ya diaspora katika kutumia fursa za uwekezaji zilizopo ili kuiletea Tanzania maendeleo.
Mwakilishi wa Watanzanzania wanaoishi ya Nje ya nchi ambaye aliishi ughaibuni kwa muda mrefu na baadae kurejea nchini Bw. Hussein M. Nyang'anyi akitoa taarifa katika Kongamano hilo. Bw. Nyang'anyi alitoa shukurani kwa Serikali kwa kuweza kuandaa Kongamano hilo kila mwaka na kuweza kuwakutanisha Watanzania waishio nje ya Nje, waliopo nchini na viongozi wakuu wa Serikali kwa lengo la kupeana taarifa na kupeana uzoefu katika masuala wa maendeleo hasa katika sekta ya Uwekezaji na Biashara.
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akiratibu katika kongamano la tatu (3) la Diaspora, linalofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort.
Sehemu ya washiriki wakiendelea kufuatilia mkutano wa pili kutoka kushoto ni Konseli Mkuu Dubai Bw. Mwadini   Wizara ya Mambo ya nje wakifuatilia Kongamano.
Sehemu ya Wawezeshaji walioshiriki katika Kongamano na kutoa mada mbalimbali wakifuatilia Kongamano
Sehemu nyingine ya Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na washiriki wengine wakifuatilia Kongamano
Kutoka kushoto ni Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Adolf Mchemwa pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Hangi Mgaka na washiriki wengine wakifuatilia Kongamano
Sehemu nyingine yamaafisa wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Kongamano
Mkutano ukiendelea
Viongozi wa meza kuu wakiwa wamesimama wakati nyimbo za Taifa zikipigwa
Washiriki wakiwa wamesimama wakati nyimbo za Taifa zikipigwa
Bendi ya Jeshi la Polisi (Brass Band) wakipiga nyimbo za Taifa katika Kongamano
Mhe. Rais Shein akijadili jambo na Mhe. Waziri Mahiga mara baada ya kumaliza ufunguzi wa Kongamano
Picha ya Pamoja ya mgeni Rasmi Mhe. Dkt. Shein na meza kuu.
Picha ya pamoja ya meza kuu pamoja na wawezeshaji walioshiriki katika Kongamano

*****************************

Rais Shein afungua Kongamano la tatu (3) la Diaspora

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya ufunguzi wa Kongamano la tatu la Watanzania waishio Ughaibuni “Diaspora home coming” lililofunguliwa leo na linatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku mbili  katika Hotel ya Zanzibar Beach Resort Visiwani Zanzibar.

Kongamano hilo lenye kauli mbiu isemayo “Bridging Tanzania Tourism and Investment: A new Outlook” MTU KWAO NDIO NGAO ikiwa na lengo la kusisitiza kuunganishwa kwa sekta ya Utalii na Uwekezaji ili kwenda sambamba na kasi ya maendeleo ya Serikali. Kongamano hili kwa mara ya kwanza linafanyika Zanzibar na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa, lilitanguliwa na Makongamano mawili yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Shein katika hotuba yake ya ufunguzi, alieleza jitihada za makusudi zinazochukuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano katika kutambua haki na wajibu wa Watanzania waishio Ughaibuni.  Hivyo kufuatia umuhimu huo Serikali iliamua kuanzisha Idara ya Diaspora ambayo inasimamia masuala yote ya jumuiya za wanadiaspora popote walipo katika mataifa mengine, sambamba na kuandaa sera ya diaspora ambayo itamtambua mwanadiaspora pamoja na kuainisha fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta ya utalii na uchumi na namna Wanadiaspora hao wanavyoweza kuchangia katika bajeti ya Serikali kwa kuchangia fedha katika akaunti maalum na katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo.

 Vilevile Mheshimiwa Rais Shein akaongeza kwa kusema kuwa “endapo sera hiyo ikikamilika jumuiya za wanadiaspora zitaweza kusoma sera hiyo kupitia Tovuti ya Ikulu na pale itakapohitajika kutunga sheria basi mamlaka zitafanya hivyo”.

Wazizi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Mhe. Dkt. Augustine Mahiga ambaye pia alishiriki katika hafla hiyo ya ufunguzi wa Kongamano, alitumia fursa hiyo kuwaeleza kuwa Tanzania inavivutio vingi na kuwashauri ni vema  wakatumia fursa hiyo kuvitangaza vivutio vilivyopo na pia kuvipa kipaumbele vivutio ambavyo bado havijatambuliwa ili viweze kutambuliwa rasmi na kutangazwa duniani kwote na kuiwezesha nchi ya Tanzania kushika nafasi ya juu miongoni mwa mataifa yenye vivutio na maajabu mengi duniani.
Pia alieleza Wizara kupitia Idara ya diaspora inaendelea na utaratibu wa kuandaa mfumo wa kuwatambua wanadiaspora na utekelezaji wake unaelekea kukamilika na kwamba zoezi hilo litakuwa la kuendelea ambapo takwimu zitakuwa zikihuishwa mara kwa mara katika ofisi zote za Ubalozi zinazoiwakilisha nchi ya Tanzania katika mataifa mengine.

Pia aliwaasa wanadiaspora hao kujiepusha kushiriki katika makosa ya kihalifu na makosa mengine ambayo yanapingana na sheria na taratibu za nchi husika. “Wizara yangu wakati mwingine imekuwa ikipokea taarifa za vitendo ambavyo zinaichafua sifa ya nchi yetu au kuleta masikitiko kwa ndugu na jamaa” alisema Waziri Mahiga.

Hivyo ni wakati sasa kila mwanadiaspora akawa balozi wa Tanzania katika nchi anayoishi kwa kutumia vizuri fursa za kimaendeleo zilizopo katika Taifa analoishi, pamoja na kudumisha sifa nzuri ya upendo, amani na mshikamano iliyojengeka tangu siku nyingi, ikiwa ni pamoja na kudumisha utamaduni wa Taifa.

Aidha, Watanzania waishio Ughaibuni walipata fursa ya kusikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na watoa mada kutoka katika Taasisi na Idara za Serikali pamoja na sekta binafsi zilizolenga katika kuwapa taarifa  za taratibu za uwekezaji na miradi mbalimbali inayotekelezwa  na mashirika ya Umma na Makampuni binafsi sambamba na kuwaeleza  fursa nyingine mpya za miradi ya kiuchumi kama ujenzi, masoko kwaajili ya biashara mbalimbali,  utalii pamoja na uwekezaji katika sekta ya viwanda kwa lengo la kuunga mkono sera ya serikali ya awamu ya tano katika adhima yake ya kujenga Tanzania ya viwanda. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.