Wednesday, August 3, 2016

Kaimu Katibu Mkuu azungumza na Wataalam Elekezi kuhusu ushirikiano na Washirika wa Maendeleo


Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akizungumza na Mtaalam Mwelekezi kuhusu masuala ya Ushirikiano wa Kimaendeleo kati ya Serikali na Washirika wa Maendeleo, Dkt. James Adams alipotembelea Wizarani na ujumbe wake kwa ajili ya kupata maoni mbalimbali ya namna bora ya kukuza ushirikiano kati ya Serikali na Washirika wake wa Maendeleo. Dkt. Adams aliwahi kuwa Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia na Mkurugenzi wa Benki hiyo hapa nchini.

Dkt. Adams nae akieleza jambo kwa Kaimu Katibu Mkuu, Balozi Mwinyi
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy naye akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Kaimu Katibu Mkuu na Dkt. Adams (hawapo pichani). Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Wizarani, Bw. James Lugaganya (katikati) na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Eva Ng'itu.
Bw. Lugaganya akichangia hoja
Ujumbe uliofuatana na Dkt. Adams nao wakifuatilia mazungumzo. Kulia ni Bw. Steve Kayizzi-Mugerwa na Bw.Mugisha Kamugisha.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.