Monday, August 29, 2016

Waziri Mkuu atembelea Banda la Tanzania na nchi zingine maonesho ya TICAD VI


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka kuhusu Michoro maarufu ya Tanzania ijulikanayoo kama Tingatinga alipotembelea Banda la Tanzania kwenye Maonesho ya Biashara ya Afrika na Japan yaliyofanyika Jijini Nairobi wakati wa Mkutano wa TICAD VI. Wengine wanaoshuhudia ni Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Chirau Ali Mwakere (wa kwanza kushto),  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki ya Kenya, Bi. Betty Maina na Kaimu Balozi wa Tanzania, Kenya, Bi. Talha Waziri.
Bw. Rutageruka akisisitiza jambo kuhusu michoro hiyo kuwa asili yake ni Tanzania na si sehemu nyingine yoyote
Mhe. Waziri Mkuu akifurahia jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Cliford Tandari (kushoto) alipowasili kwenye Banda la maonesho la TIC.
Mhe. Waziri Mkuu akisaini kitabu cha wageni kwenye Banda la TIC huku Kaimu Mkurugenzi wa Kituo hicho Bw. Tandari na Maafisa kutoka TIC wakishuhudia.
Mhe. Wazir Mkuu akimsikiliza Meneja wa Uwekezaji wa EPZA, Bw. Lameck Borega alipotembelea Banda lao la Maonesho.
Mhe. Waziri Mkuu akisalimiana na Bi. Alistidia Karaze, Afisa Utafiti Mkuu kutoka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) alipotembelea Banda la Maonesho la TTB.
Bi. Karaze akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu kuhusu mikakati ya kutangaza Utalii inayofanywa na TTB.
Mhe. Waziri Mkuu nae akitoa maelekezo kuhusu namna bora ya kujipanga katika kutangaza utalii. Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Sayansi, Prof. Makame Mbarawa ambaye naye alikuwa Jijini Nairobi kuhudhuria Mkutano wa TICAD VI
Mhe. Waziri Mkuu akipata maelezo kuhusu soko la Batiki kutoka kwa mmoja wa akina mama wa Kitanzania wanaoshiriki maonesho ya Biashara ya Afrika na Japan Jijini Nairobi alipotembelea Banda lao. Kushoto ni Bw. Francis Mosongo, Afisa Mwandamizi wa Dawati la Japan katika Ubalozi wa Tanzania, Japan.
Mhe. Waziri Mkuu akimsikiliza mshiriki mwingine kutoka Tanzania ambaye anajishughulisha na biashara ya bidhaa kutoka Tanzania kama vitege, khanga, na batiki

Mhe. Waziri Mkuu akiwa ametembelea Banda la Maonesho la Rwanda

Mhe. Waziri Mkuu akipata maelezo alipotembelea Banda la Maonesho la Kenya

Mhe. Waziri Mkuu akikaribishwa alipotembelea Banda la Maonesho la Uganda
Mhe. Waziri Mkuu akinsikiliza Mkurugenzi wa Kampuni ya Sumitomo ya Japan alipotembelea Bandani hapo. Kampuni ya Sumitomo ndiyo inajenga mitambo ya uzalishaji wa Umeme wa gesi asilia wa Megawati 240 iliyopo Kinyerezi Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi huyo wa Sumitomo akimwonesha Waziri Mkuu picha za Mitambo ya Umeme iliyopo Kinyerezi
Mhe. Waziri Mkuu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya waliofika Uwanja wa Ndege wa Jommo Kenya kwa ajili ya kumsindikiza kabla ya kuondoka kurejea nchini mara baada ya kuhudhuria Mkutano wa TICAD VI. Katika Picha ni Bi. Talha Waziri, Kaimu Balozi wa Tanzania, Kenya; Bw. Mkumbwa Ally (wa pili kushoto), Bw. Amos Mwakasege (kushoto) na Bw. Loshilaari Ole Kambainei (Kulia), Maafisa Waandamizi Ubalozini hapo.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.