Sunday, August 28, 2016

Waziri Mkuu akutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Jijini Nairobi

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan, Mhe. Luteni Jenerali Barki Hassan Salih walipokutana Jijini na Nairobi wakati wa Mkutano wa TICAD VI kwa mazungumzo ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Mhe. Majaliwa akiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba(kushoto) na Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Bi. Talha Waziri (wa pili kulia) na Bi. Irene Bwire, Mwandishi wa Waziri Mkuu wakifuatilia mazungumzo  kati yake na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan, Mhe. Lt. Gen. Salih na ujumbe wake hawapo pichani)
Mhe. Salih (wa tatu kushoto) akiwa na ujmbe aliofuatana nao wakati wa mazungumzo yake na Mhe. Majaliwa (hayupo pichani)



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.