Wednesday, August 10, 2016

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atembelea Kiwanda cha kushona nguo cha Tooku

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akikagua ushonaji wa suruali za Jeans wakati alipotembelea kiwanda cha kushona nguo cha Tooku kilichopo kwenye eneo la EPZ, Mabibo External jijini Dar es salaam Agosti 10, 2016.  Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa  Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dr. Adelhem Meru na wapili kushoto ni Meneja Mkuu Msaidizi wa kiwanda hicho, Rigobert Massawe.


Mfano wa suruali ya Jeans zinazotengenezwa na kiwanda hicho zikiwa na utambulisho wa kutengenezwa nchini Tanzania. Hivi sasa kiwanda kimeanzisha programu ya kutoa mafunzo kwa vijana 400 kila mwezi katika miezi 12 na ifikapo mwisho wa mwaka jumla ya watanzania 6000 watakuwa wameajiriwa. 
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akikagua ushonaji wa suruali za Jeans wakati alipotembelea kiwanda cha kushona nguo cha Tooku kilichopo kwenye eneo la EPZ, Mabibo External jijini Dar es salaam Agosti 10, 2016.  Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa  Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dr. Adelhem Meru na wapili kushoto ni Meneja Mkuu Msaidizi wa kiwanda hicho, Rigobert Massawe.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akikagua ushonaji wa suruali za Jeans wakati alipotembelea kiwanda cha kushona nguo cha Tooku kilichopo kwenye eneo la EPZ, Mabibo External jijini Dar es salaam  Agost 10, 2016 .  Kulia ni Balozi wa China nchini, Dkt Lu Youqing na kushoto ni Meneja Mkuu Msaidizi wa kiwanda hicho, Rigobert Massawe.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza  baada ya kutembelea kiwanda cha kushona nguo cha Tooku kilichopo kwenye eneo la EPZ, Mabibo External jijini Dar es salaam Agost 10, 2016.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa kiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa kiwanda cha kushona nguo cha  Tooku kilichopo eneo la EPZ,Mabibo External jijini Dar es salaam baada ya kutembelea kiwanda hicho na kuzungumza, Agosti 10,2016.  Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Adelhem Meru na kulia kwake ni Balozi wa China nchini, Dkt. Lu Youqing. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.