Friday, August 26, 2016

Naibu Waziri akutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba  akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Mhe. Zhang Ming walipokutana Nairobi  kwa mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na China.  Mhe. Dkt. Kolimba pamoja na Mhe. Zhang wapo mjini humo kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa TICAD VI utakaofanyika tarehe 27 na 28 Agosti, 2016.
Mhe. Kolimba akimweleza jambo Mhe. Zhang wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Zhang na ujumbe wake wakati wa mkutano na Mhe. Dkt. Kolimba (hayupo pichani)
Mhe. Dkt. Susan Kolimba akiwa na Waziri wa Fedha na Uchumi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Khalid Salum Mohammed (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbelwa Kairuki (wa pili kutoka kushoto) na Bw. Adam Isara, Msaidizi wa Naibu Waziri.
Mhe. Naibu Waziri na Mhe. Waziri Mohammed pamoja na wajumbe wengine wakimsikiliza Mhe. Zhang ambaye hayupo pichani. Kulia ni Bi. Bertha Makilagi, Afisa Mambo ya Nje. 








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.