Friday, August 12, 2016

Waziri Mahiga azungumza na Waandishi wa Habari


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani)  kuhusu  Mkutano wa 18 wa  Kamati ya Mawaziri ya Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama  ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika-SADC  uliofanyika Maputo, Msumbiji kuanzia tarehe 1-5 Agosti, 2016. Mkutano huo pamoja na mambo mengine ulizungumzia hali ya usalama na amani katika nchi za Lesotho, DRC na Madagascar.
Mhe. Waziri Mahiga akiwaeleza waandishi kuhusu 
Kitabu cha Harakati za Ukombozi katika Nchi za Kusini mwa Afrika ambacho kimepewa jina la Hashim Mbita  kufuatia mchango Mkubwa wa Hayati Brigedia Jenerali (Mstaafu) Balozi Hashimu Mbita katika harakati za ukombozi na uandishi wa kitabu hicho.Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Innocent Shiyo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga.
 Mkutano huo ukiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.