Wednesday, January 31, 2018

Kongamano la Biashara la Tanzania na Jamhuri ya Korea katika Picha

Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na Bw. Jundong Kim, Makamu Mwenyekiti wa "Korea Chambers of Commerce and Industry" muda mfupi kabla ya uzinduzi wa Kongamano la kwanza la Biashara kati ya Tanzania na Korea Kusini tarehe 31 Januari 2018.  

Bw. Kim akimuelezea Mheshimiwa Waziri Mahiga na ujumbe wake kwa kifupi kuhusu kazi za KCCI kabla ya kufungua Kongamano la Kwanza la Biashara kati ya Tanzania na Korea Kusini. 

Mheshimiwa Matilda Masuka, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea akiwakaribisha wajumbe waliofuatana na Mheshimiwa Waziri kwenye ziara hiyo kuingia kwenye ukumbi wa Kongamano.

Watanzania wanaoishi nchini Korea wakiwa kwenye mashati maalum ya kutangaza Kongamano ambao pia walikua wakitoa huduma mbalimbali wakati Kongamano likiendelea.









Pichani juu na chini Mheshimiwa Waziri Mahiga akiagana na Watanzania walioshiriki kwenye Kongamano hilo baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya majadiliano.



Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania na Korea Kusini


Mheshimiwa Augustine Phillip Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akilakiwa na mwenyeji wake Mheshimiwa Kang Kyung-hwa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea, mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa mazungumzo ya kikazi tarehe 31 Januari 2018. 


Mheshimiwa Augustine Mahiga na mwenyeji wake Mheshimiwa Kang Kyung-hwa wakiwa kwenye mazungumzo ya kikazi ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Korea tarehe 31 Januari 2018. Wakwanza kushoto ni Mheshimiwa Matilda Masuka, Balozi wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Korea. Wakwanza kulia ni Bw. Park Young min, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Korea





Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania akimkabidhi zawadi ya picha ya mlima Kilimanjaro na kinyago cha mnyama waziri mwenzake wa Jamhuri ya Korea Mheshimiwa Kang Kyung-hwa baada ya kukamilisha mazungumzo ya kikazi yanayolenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na uchumi baina ya nchi hizo mbili. 


Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Korea wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kukamilisha mazungumzo ya kikazi. Wakwanza kulia ni Mheshimiwa Balozi Matilda Masuka, Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Bi. Bertha Makilagi, afisa dawati wa Korea Kusini, Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Park Young min, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo  ya Nje ya Korea Kusini na Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Tuesday, January 30, 2018

WAZIRI MAHIGA AANZA ZIARA YA SIKU 3 NCHINI KOREA KUSINI

Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akipokelewa na maua na Mheshimiwa Matilda Masuka, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Jamhuri ya Korea Kusini. Kushoto ni Ndugu Masuka, mume wa Balozi Masuka. 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

ZIARA YA WAZIRI MAHIGA KOREA KUSINI KUKUZA DIPLOMASIA YA UCHUMI

                                                                                                                                                                                                                                                                                
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu nchini Jamhuri ya Korea Kusini yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Korea ya Kusini.

Mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Incheon Mjini Seoul, Mheshimiwa Waziri Mahiga amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya GS E&C Bw. Min Jeong na timu yake inayoshugulikia uwekezaji na biashara nchini Tanzania.

Waziri Mahiga aliyeongozana na Bw. Edwin Rutageruka, Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE) na Bw. Geoffrey Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji  cha Tanzania alielezea utayari wa Tanzania kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo kama ule wa ujenzi wa reli ya kisasa ya viwango vya kimataifa wa “Standard Gauge Railway” inayohusisha makampuni makubwa ya kimataifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Jeong alielezea kuwa Kampuni ya GS E&C iliyojikita kwenye ujenzi wa miundombinu ya viwango vya kimataifa, ufuaji na usambazaji wa umeme, usafishaji wa mafuta n.k., sasa imejipanga pia kushiriki katika Ujenzi wa SGR (kupitia ushirikiano na kampuni ya Uturuki (awamu ya 3-5), na Ujenzi wa Daraja la Selanda.

Mbali na mpango huo, kwa sasa Kampuni hiyo yenye makao yake makuu kwenye mji mkuu wa Korea Kusini, Seoul, imeshiriki katika Mradi ya Umeme nchini Tanzania wa Dar-Arusha “Transmition Line”.

Waziri Mahiga alisisitiza nia ya dhati ya Serikali ya Tanzania katika kusimamia ujenzi wa Reli ya Kisasa ya Viwango na kuhakikisha inakamilika kwa wakati. Vilevile alitumia fursa hiyo kumuelezea Mkurugenzi Jeong na timu yake kuhusu mpango wa uendelezaji wa ujenzi wa reli hiyo ya viwango kutoka Isaka hadi Kigali, mpango ambao ulitangazwa na Waheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli na Mheshimiwa Paul Kagame, Rais wa Tanzania na Rwanda hivi karibuni.

Mheshimiwa Mahiga alimhakikishia mkurugenzi huyo na kundi la makampuni anayoyaongoza, ushirikiano wake na kumkaribisha kuwekeza zaidi nchini Tanzania kwenye miradi mbalimbali ya umeme na miundombinu mingine.

Kampuni ya GS E&C ni miongoni mwa makampuni kumi “Top Ten” yanayofanya vizuri zaidi nchini Korea Kusini inayokusanya faida ya kiasi cha $10 bilioni kwa mwaka.

Mheshimiwa Waziri Mahiga ambaye yupo nchini hapa kuanzia leo tarehe 30 Januari hadi tarehe 2 Februari, 2018, kufuatia mwaliko wa Mhe. Dkt. Kang Kyung-wha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea anatarajiwa pia kuzindua Kongamano la kwanza la wafanyabiashara, kufungua majengo ya Ubalozi wa Tanzania na kufanya mazungumzo maalum na mwenyeji wake Waziri Kang Kyung-wha.

Mheshimiwa Mahiga atatumia sehemu kubwa ya ziara hiyo kukutana na kufanya mazungumzo na makampuni makubwa yalikwisha onesha nia ya kuwekeza nchini Tanzania. Mwishoni mwa ziara hiyo, Mheshimiwa Waziri Mahiga anategemewa kutembelea Chuo cha Taifa cha Diploamasia cha Korea Kusini, kabla ya kurejea nchini Tanzania.

-Mwisho-

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Seoul, Korea Kusini,

30 Januari 2018.


Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na wawakilishi wa kampuni ya GS E&C waliofika hotelini kwake na kufanya naye mazungumzo ya kikazi kwenye Mji Mkuu wa Jamhuri ya Korea, Seoul. Pichani wawili ni Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni hayo Bw. Min Jeoung. 





Ujumbe wa Mheshimiwa Mahiga ukiongozwa na Mheshimiwa Matilda Masuka, Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Bw. Geoffrey Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa TIC na Bw. Edwin Rutageruka, Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE wakiwa kwenye mazungumzo na wawakilishi wa makampuni ya GS E&C.

Picha ya Pamoja

Tanzania kuendelea kuimarisha ushirikiano na Singapore

Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akizungumza na Balozi wa Singapore nchini mwenye makazi yake nchini Singapore, Mhe. Tan Puay Hiang alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Mazungumzo yao yalijikita katika kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano pamoja na kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara ili kuweza kuinua uchumi wa mataifa hayo.
Mazungumzo yakiendelea.

Mhe. Tan Puay Hiang akimkabidhi Balozi Mwinyi zawadi ya kitabu.

Picha ya pamoja Kaimu Katibu Mkuu, Mhe. Balozi Tan Puay Hiang, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Luhangisa (kulia) na Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa Singapore, Bw. Lucien Hong(kushoto) 

Naibu Waziri akutana na Balozi wa Singapore nchini

 Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba akizungumza na Balozi wa Singapore nchini Mhe. Balozi Tan Puay Hiang, alipomtembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam, tarehe 29/11/2018. 
Katika mazungumzo hayo Mhe. Dkt. Kolimba alishukuru Serikali ya Singapore kwa misaada wanayoitoa kwa Tanzania hasa katika eneo la elimu, Mhe. Dkt Suzan alitumia nafasi hiyo kumwalika Balozi huyo kutembelea vivutio vya utalii vilivyo nchini ikiwa ni pamoja na kuhamasisha Watalii kutoka nchi hiyo kutembelea Tanzania. 
Kwa upande wake Mhe. Puay Hiang aliikaribisha Tanzania kujifunza Singapore hasa katika eneo la Utalii na alimhakikishia Mhe. Waziri kwamba nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mbalimbali.

Mhe. Dkt Suzan Kolimba na Mhe. Balozi Puay Hiang wakiendelea na mazungumzo, wanaofuatilia ni Bw. Emmanuel Luangisa; Kaimu Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia (Kushoto), Bw. Charles Faini Msaidizi wa Naibu Waziri ( Mwisho kushoto) na Bw. Lucien Hong Mkurugenzi msaidizi kutoka ubalozi wa Singapore ( kulia).    
                                     
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo.

Monday, January 29, 2018

Mhe. Naibu Waziri amuaga Balozi wa Zimbabwe.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Suzan Kolimba akimkabidhi zawadi Balozi wa Zimbabwe nchini anayemaliza muda wake Mhe. Balozi Edzai Chimonyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika Serena Hotel tarehe 29/01/2018. 

Katika hafla hiyo Mhe. Dkt Suzan alimshukuru kwa ushirikiano mkubwa kwa kipindi chote alichokuwa Balozi hapa nchini na kumtakia heri katika majukumu yake mapya. Mhe. Balozi  alimshukuru Naibu Waziri kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Ushirikiano mkubwa alioupata wakati akitekeleza majukumu yake hapa nchini.

Waheshimiwa Mabalozi, Mhe. Brahim Buseif Balozi wa Sahara Magharibi nchini (wa kwanza kushoto) na Mhe. Benson Keith Chali Balozi wa Zambia Nchini wakifuatilia hafla hiyo

Mhe. Naibu Waziri Dkt Suzan Kolimba akiteta jambo na Mhe. Balozi Edzai Chimonyo katika hafla hiyo.


 Baadhi ya Maafisa kutoka Wizarani Bi. Elizabeth Mutunga na Bi. Robi Bwiru wakifuatilia hafla hiyo.

 Bw.Ayoub Mdeme Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika (Kulia) na Bw. Martin Tavenyika kutoka Ubalozi wa Zimbabwe nchini (kushoto) wakiwa katika hafla hiyo.

Bw. Suleiman Saleh Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika akiteta jambo na Mhe. Thamsanga Dennis Msekelu Balozi wa Afrika Kusini nchini, anayefuatilia ni Mhe. Balozi Edzai Chimonyo.

Maafisa kutoka Wizarani Bw. Charles Faini na Bi. Mercy Kitonga nao wakiwa katika hafla hiyo.

Friday, January 26, 2018

Mhe. Hamad Rashid akutana na Naibu Waziri wa Kilimo wa China

Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohammed akizungumza na Naibu Waziri wa Kilimo wa China, Mhe. Dkt. QU DONGYU walipokutana katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijijni Dar es Salaam tarehe 26 Januari, 2018 kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikino katika sekta ya kilimo na uvuvi kati ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na China.  Mhe. Dkt. QU DONGYU yupo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mazungumzo kati ya Mhe. Hamad Rashid na Mhe. Dkt. QU DONGYU yakiendelea huku wajumbe wa China na Tanzania wakifuatilia.
Mhe. Hamad Rashid na Dkt. QU kwa pamoja wakipitia baadhi ya nyaraka za ushirikiano


Picha ya pamoja kati ya Mhe. Hamad Rashid na Dkt. QU DONGYU pamoja na wajumbe wengine walioshiriki kikao hicho. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki
Mhe. Hamad Rashid akiagana na Dkt. QU DONGYU mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.

Thursday, January 25, 2018

Naibu Waziri wa Kilimo wa China atembelea Tanzania


Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt.Charles Tizeba ( Katikati mwenye kipaza sauti), akiongoza mazungumzo wakati wa Mkutano na Naibu Waziri wa Kilimo wa China, Mhe. DK QU DONGYU(hayupo pichani) uliofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) tarehe 25 Januari,2018. 
Wengine katika picha ni Balozi wa Tanzania China Mhe. Balozi Mbelwa Kairuki ( wa kwanza kulia), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Dkt.Thomas Kashilila, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (wa pili kutoka mwisho kushoto). 

Katika majadiliano hayo pande zote mbili zimekubaliana kuundwa kikosi kazi ambacho kitakuwa na kazi ya kuhakikisha maeneo waliyokubaliana kushirikiana yanatekelezwa, kikosi kazi hicho kitahusisha wataalam kutoka Tanzania na China. Baadhi ya maeneo ambayo China na Tanzania watashirikiana ili kuinua kilimo cha Tanzania ni; kuboresha miundombinu ya Kilimo kama vile Scheme za Umwagiliaji, ushirikiano kati ya chuo cha Kilimo cha Sokoine na vyuo vya kilimo vya China, kushirikiana katika tafiti mbalimbali, China kuwekeza katika viwanda vya kuongeza thamani katika mazao, masoko n.k. Mhe. DONGYU  anatarajiwa kuondoka nchini tarehe 28, Januari,2018. 


Naibu Waziri wa Kilimo wa China Mhe. DK QU DONGYU ( wa tatu kulia mwenye kipaza sauti) akielezea jambo katika mazungumzo hayo, kushoto kwake ni balozi wa China nchini Mhe. Balozi Wang Ke na wengine ni ujumbe wa watalaam waliongozana na Mhe. Waziri DONGYU

  Waziri wa Kilimo kutoka China Mhe. DK QU DONGYU pamoja na ujumbe aliongozana nao wakifuatilia mazungumzo
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Mkutano.

Tuesday, January 23, 2018

Timu Maalum ya ADB yatembelea Tanzania



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Aldof Mkenda (kulia) akiwa katika mazungumzo na Bw. Alieu Jeng- Mjumbe wa Timu kutoka Bank ya Maendeleo ya Afrika (African Development Bank), walipomtembelea Wizarani tarehe 22 Januari,2018
Timu hiyo yenye jumla ya wajumbe watatu ambao watakuwa nchini kwa lengo la kujadiliana na Serikali kuhusu maeneo ya vipaombele ambayo wanaweza kusaidia kupitia bajeti yao ya 2018/2019. wakiwa nchini watakutana na Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali. Kwa mujibu wa wajumbe hao, bajeti hii itazingatia zaidi kusaidia Serikali kupitia maeneo  ya vipaombele yaliyoanishwa  ili kuwezesha Sekta binafsi kuweza kuchochea uchumi wa nchi kupitia biashara na Uwekezaji katika maeneo mbalimbali.  wajumbe hao waliwasili tarehe 14 Januari, 2018 na wanatarajiwa kuondoka tarehe 27 Januari,2018.


 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Aldof Mkenda (kulia), akiendelea na mazungumzo na wajumbe wa Timu kutoka ADB ambao ni Bw.Alieu Jeng(Kushoto), Bw. Frsncois Nkulikiyimfura anayefuata na mwisho kushoto ni Bi.Eline Okuozeto

Katibu Mkuu, timu ya ADB na Wataalam kutoka Wizarani wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo