Thursday, April 12, 2018

Waziri Mahiga ampokea nchini Waziri wa Mambo ya Nje wa Poland

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Poland, Mhe. Prof. Jacek Czaputowicz mara baada ya kumkaribisha rasmi Wizarani tarehe 12 Aprili, 2018. Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali zikiwemo elimu, kilimo, utalii, biashara na uwekezaji. Mhe. Czaputowicz yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo pamoja na mambo mengine atazindua rasmi ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini.
Mhe. Waziri Mahiga na Mhe. Waziri Czaputowicz wakionesha Mkataba wa Makubaliano kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na Poland.
Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin (kulia)  kwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi (kushoto), Afisa Mambo ya Nje, Bi. Mona Mahecha (wa pili kushoto) na Afisa Mawasiliano, Bi. Robi Bwiru (wa pili kulia) wakifuatilia mazungumzo kati ya Waziri Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Poland, Mhe. Czaputowicz (hawapo pichani).
Balozi wa Poland nchini, Mhe. Krzysztof Buzalski (kulia) akiwa na Wajumbe wengine kutoka Poland  wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Waziri Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Poland, Mhe  Czaputowicz (hawapo pichani)
Picha ya pamoja.

Waziri Mahiga ahimiza wadhamini zaidi kujitokeza kufanikisha Wiki ya Tanzania nchini Kenya

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiwa na  Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Maandalizi ya Maonesho ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania nchini Kenya, Balozi Anisa Mbega walipokutana na Wadhamini na Wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya maonesho hayo (hawapo pichani) yanayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 25 - 28 Aprili 2018 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi, Kenya. 

Mazungumzo hayo yamefanyika leo tarehe 12 Aprili 2018 katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam  na kuambatana na hafla ya kukabidhi udhamini kwa ajili ya  kufanikisha  maonesho hayo maarufu kama ''Wiki ya Tanzania nchini Kenya'' ambayo yataenda sambamba na sherehe za miaka 54 za Muungano wa Tanzania. 


Sehemu ya wadhamini na  wajumbe wa kamati ya maandalizi wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiongozwa na Mhe. Waziri Mahiga (hayupo pichani)
Viongozi wa Kampuni ya NIDA TEXTILE MILLS (T) wakimkabidhi Mhe. Waziri Mahiga mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi 22,700,000/- kwa ajili ya kudhamini maonesho ya didhaa za viwanda vya Tanzania nchini Kenya. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Bw. Muhammad Waseem.

Mhe. Waziri Mahiga akimshukuru Mwakilishi wa Kampuni ya Mohamed Enterprises, Bi. Barbara Gonzale baada ya kutoa ahadi ya udhamini wa kiasi cha shillingi millioni ishirini na tano (25,000,000) kwa ajili ya kudhamini maonesho hayo.
Mhe. Waziri Mahiga akimshukuru mwakilishi kutoka kampuni ya Tanzania Distilleries Ltd, Bw. Maleke Hans baada ya kutoa ahadi ya udhamini wa kiasi cha Dola za Marekani 5,000 (sawa na shilingi milioni kumi na moja  za Tanzania).
Mhe. Waziri Mahiga akisikiliza taarifa fupi ya udhamini na hatua ya maandalizi iliyofikiwa  kutoka kwa Katibu wa Kamati, Balozi Mbega, pembeni ni baadhi ya Wadhamini na Wajumbe wa Kamati.
Sehemu nyingine ya wajumbe wa kamati wakifuatilia ufafanuzi uliokuwa ukitolewa na Balozi Mbega kwa Mhe. Waziri Mahiga.
Picha ya pamoja.



Wednesday, April 11, 2018

Wizara ya Mambo ya Nje yaikabidhi TBA nyumba zilizorejeshwa na Umoja wa Ulaya nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kulia) kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa pamoja na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Roeland van de Geer wakisaini Hati ya Makabidhiano ya nyumba nne (4) kutoka Umoja wa Ulaya zilizopo katika maeneo tofauti ya Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam. Nyumba hizo zimekabidhiwa kwa Wizara  na EU baada ya kutumiwa na Umoja huo tokea miaka ya 1975. Baada ya makabiadhiano hayo, Wizara ilizikabidhi nyumba hizo kwa Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA). Makabidhiano hayo yalifanyika Wizarani tarehe 11 Aprili, 2018.
Balozi Mushy kwa pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Mhandisi. Elius Mwakalinga wakisaini hati ya makabidhiano kama ishara kwa Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuzikabidhi kwa TBA nyumba nne (4) zilizopokelewa na Wizara kutoka EU.
Balozi Mushy na Balozi Roeland van de Geer wakibadilishana hati hiyo baada ya kusaini
Balozi Mushy na Balozi van de Geer wakionesha hati hiyo
Balozi Mushy na Mhandisi Mwakalinga wakibadilishana hati hiyo mara baada ya kusaini
Wakionesha hati hiyo
Mhandisi Mwakalinga na Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin wakishuhudia Balozi Mushy na Balozi Roeland (hawapo pichani) wakisaini hati ya makabidhiano ya nyumba kutoka EU
Ujumbe uliofuatana na Balozi Roeland kutoka Ofisi za EU nchini nao wakishuhudia tukio hilo
Balozi Mushy na Balozi Roeland wakiteta jambo
Bw. Batholomeo Jungu, Afisa Mambo ya Nje katika Idara ya Itifaki akitoa maelezo na utaratibu kwa Mabalozi kabla ya kuanza kusainiwa kwa hati hizo za makabidhiano
Picha ya pamoja


PRESS RELEASE

 




MADE IN TANZANIA WEEK IN KENYA
 
The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation through its Embassy in Nairobi, Kenya and in collaboration with the Ministry of Industry, Trade and Investment (Tanzania Mainland); Ministry of Trade, Industry and Marketing (Zanzibar); Tanzania Trade Development Authority (TanTrade) and Tanzania Private Sectors has organized “Made in Tanzania Week” seeking to pursue wider and broader markets opportunities for country’s industrial products and tourism potentials in the East African Community which will take place between 25th to 28th April 2018 in Kenya.
 This comes as an effort in the implementation of the country’s Foreign Policy which focuses on Economic Diplomacy with much emphasis on the development of sectors like trade, investment and tourism. The event will fall within the National Day (54th Union Day celebration) on 26th April 2018 and will feature industrial products, services in particular tourism, technology, agribusiness, culture, arts and craft.
It should be recalled that, in 2010 the East African Community Partner States signed an agreement on the Common Market Protocol; hence “Made in Tanzania Week in Kenya” will be amongst Government initiatives to promote the forging relationship that has been existing among the Partner States in the Community and spearhead economic development. 
‘’Made in Tanzania week in Kenya’’ which will take place at the Kenyatta International Convention Center (KICC) is scheduled as follows; on the 25th– 28th April 2018 "Made in Tanzania” Exhibitions to showcase Tanzanian products will take place followed by Tanzania - Kenya Business to Business (B2B) meeting on 25th April 2018. Again, on 26th April 2018 a reception for the 54th Union Anniversary will be held at the High Commissioner’s residence in Nairobi. The 54th Union celebrations will be concluded by two major events; the Tanzania - Kenya Business Forum that will take place on 27th April 2018 and Made in Tanzania Business Gala Dinner.
On behalf of the Organizing Committee Co-Chaired by Tanzania Trade Development Authority (TanTrade) and Tanzania Private Sector Foundation (TPSF), the Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation would like to invite the key stakeholders particularly the business community to take advantage of this opportunity and participate in the event.
 For more information on Made in Tanzania Week in Kenya, kindly call +255767123055 or +255687368443 or register ONLINE via www.tanzaniakenya.com.

Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dar es Salaam.
11th April 2018.
 
 
 


 


 

Tuesday, April 10, 2018

Balozi Mwinyi azungumza na Wajumbe wa Mkutano wa 8 wa Kijani Zanzibar

Naibu Katibu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhan Mwinyi Muombwa akizungumza kwenye mkutano wa 8 wa wiki ya Kijani ambao umeingia siku ya pili leo, ambapo katika mkutano wa leo wadau wamejadili kuhusu athari za mionzi itokanayo na vyombo chakavu vya kielektroniki. 
Sehemu ya wajumbe wa Mkutano huo wakimsikiliza Balozi Mwinyi akitoa hotuba yake. 
Balozi Mwinyi akiendelea kuzungumza kwenye Mkutano huo wa 8 wa Wiki ya Kijani unaoendelea kwenye Hoteli ya Sea Cliff Zanzibar, Tanzania.
Dkt. Chaesub Lee naye akizungumza jambo kabla ya wataalamu kuanza kudajili athari za matumizi ya vyombo chakavu vya kielektroniki kwenye Mkutano wa 8 wa Wiki ya Kijani.

Sehemu ya wataalamu wakiendelea na mijadala mbalimbali kwenye mkutano wa 8 wa wiki ya Kijani







OPENING REMARKS BY AMBASSADOR RAMADHANI M. MWINYI,

DEPUTY PERMANENT SECRETARY FOR THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND EAST AFRICAN COOPERATION,

DURING THE 8TH GREEN STANDARDS WEEK DURING THE
FORUM & TRAINING ON WITH ICTs EVERYWHERE – “HOW SAFE IS EMF?”
SEA CLIFF HOTEL, ZANZIBAR

10TH APRIL, 2018
___________________________

Dr. Maria Sassabo, Permanent Secretary, Ministry of Works, Transportation and Communication;
Dr. Chaesub Lee, Director, Telecommunication Standardization Bureau, ITU;
Distinguished Participants;
Ladies and Gentlemen;

It is my pleasure to welcome you all to a second day of the 8th Green Standard Week. The topic for today’s discussion is very impressive.  We are going to see how safe is the Exposure to Electromagnetic Fields (EMF).  We are lucky to have experts who will make presentations on the topic, including activities of the ITU on Human Exposure to EMFs.   I wish to thank all the experts gathered here today and the organizers for a job well done.

Distinguished participants; as you are all aware exposure to human made   electromagnetic fields have increased over the past years. The deployment of different sources of EMF to cater for the telecommunication and ICT needs of the population has developed very rapidly; the use of mobile phones and other wireless system is expanding rapidly all over the world.  This is because of strong competition, quality of service requirements, network coverage extension and introduction of new technologies. 

ITU estimates that 95 percent of the global population lives in an area that is covered by a mobile –cellular network. For the case of Tanzania, there are almost over 45 million mobile – cellular subscribers.

While this expansion provides the opportunity for advances in public and personal safety, education, medicine and the economy, it also brings new responsibilities and challenges to all of us.

It is undeniable fact that the widespread use of EFM sources has possible adverse effects of prolonged exposure to emissions on people’s health. Unfortunately, the EFM is unknown and undetectable for the people; there is lack or limited regulations; and also there is rare mechanism to inform the people.  That’s why ITU as an institution remains extremely relevant in the world today and in the future in designing activities to mitigate effects of EFM due to radio systems and mobile equipment to human beings.

There is a need for the ITU to come up with a global framework and standard that will help to facilitate compliance with international standards; strengthening international technical cooperation and capacity building as well as strengthening collaboration among stakeholders like the World Health Organization.

Distinguished participants; I do understand that the health impact of electromagnetic fields similarly falls within the mandate of the World Health Organization (WHO) in the area of environmental health. The WHO came up with EMF project to respond to the general concern over health effects of EMF exposure in 1996.  That’s why today we are going to hear from the WHO representative on EMF research and future needs.
I wish to welcome you all to openly discuss, share and exchange experiences, knowledge, challenges and possible solutions. It is through these discussions that will enable ITU to come with the standards and framework we are aspiring too.

Before I handover to our moderator to proceed, on behalf of us all, I want to say KARIBUNI SANA. It is a pleasure to see so many of you here. I wish you all successful deliberations in this Forum and Training.


ASANTENI SANA…!!!!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



ZIARA YA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA POLAND NCHINI 11-13 APRILI 2018

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Poland, Mhe. Prof. Jacek Craputowicz atafanya ziara ya kikazi nchini Tanzania kuanzia tarehe 11 hadi 13 Aprili 2018.  Katika ziara hiyo, Prof. Craputowicz pamoja na mambo mengine, atafanya mazungumzo na mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) Jijini Dar Es Salaam tarehe 12 Aprili 2018.  Viongozi hao watajadili namna ya kuboresha mahusiano na mashirikiano ya kidiplomasia baina ya Tanzania na Poland, hususan katika eneo la uwekezaji na biashara.   

Poland ni moja ya nchi zinazounga mkono Sera ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2020. Katika kuunga mkono Sera hiyo, Serikali ya Poland imetoa mkopo wa masharti nafuu wa Dola za Marekani milioni 110 kwa Serikali ya Tanzania.

Kati ya fedha hizo, Dola za Marekani milioni 55 zimetumika kujenga kiwanda cha kuunganisha matrekta Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani ambacho kimeshaanza kazi na Dola za Marekani milioni 55 ni kwa ajili ya kujenga maghala ya kuhifadhia mazao ya kilimo katika mikoa minane ya Rukwa, Katavi, Manyara, Ruvuma, Dodoma, Shinyanga, Njombe na Songwe.

Prof. Craputowicz na mwenyeji wake watashiriki hafla fupi ya uzinduzi rasmi wa ofisi ya Ubalozi wa nchi hiyo zilizopo nyumba namba 15, mtaa wa Mtwara, Masaki Jijini Dar es Salaam tarehe 12 Aprili 2018. Poland ilifungua upya Ubalozi wake nchini mwaka 2017 baada ya kuufunga mwaka 2008 na kabla ya hapo nchi hiyo ilikuwa inawakilishwa kutokea Nairobi, Kenya.

Baada ya ufunguzi viongozi hao watafanya mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi hizo saa tano asubuhi. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
 10 Aprili, 2018