Wednesday, April 11, 2018

Wizara ya Mambo ya Nje yaikabidhi TBA nyumba zilizorejeshwa na Umoja wa Ulaya nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kulia) kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa pamoja na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Roeland van de Geer wakisaini Hati ya Makabidhiano ya nyumba nne (4) kutoka Umoja wa Ulaya zilizopo katika maeneo tofauti ya Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam. Nyumba hizo zimekabidhiwa kwa Wizara  na EU baada ya kutumiwa na Umoja huo tokea miaka ya 1975. Baada ya makabiadhiano hayo, Wizara ilizikabidhi nyumba hizo kwa Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA). Makabidhiano hayo yalifanyika Wizarani tarehe 11 Aprili, 2018.
Balozi Mushy kwa pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Mhandisi. Elius Mwakalinga wakisaini hati ya makabidhiano kama ishara kwa Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuzikabidhi kwa TBA nyumba nne (4) zilizopokelewa na Wizara kutoka EU.
Balozi Mushy na Balozi Roeland van de Geer wakibadilishana hati hiyo baada ya kusaini
Balozi Mushy na Balozi van de Geer wakionesha hati hiyo
Balozi Mushy na Mhandisi Mwakalinga wakibadilishana hati hiyo mara baada ya kusaini
Wakionesha hati hiyo
Mhandisi Mwakalinga na Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin wakishuhudia Balozi Mushy na Balozi Roeland (hawapo pichani) wakisaini hati ya makabidhiano ya nyumba kutoka EU
Ujumbe uliofuatana na Balozi Roeland kutoka Ofisi za EU nchini nao wakishuhudia tukio hilo
Balozi Mushy na Balozi Roeland wakiteta jambo
Bw. Batholomeo Jungu, Afisa Mambo ya Nje katika Idara ya Itifaki akitoa maelezo na utaratibu kwa Mabalozi kabla ya kuanza kusainiwa kwa hati hizo za makabidhiano
Picha ya pamoja


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.