Friday, April 27, 2018

Naibu Waziri akutana na kufanya mazungumzo na mshindi wa shindano la 28 la urembo katika taji la World Miss University Africa 2017

Mhe. Dkt. Susan Kolimba Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akizunguza na Bi. Queen Elizabeth Manule mshindi wa shindano la 28 la urembo katika taji la World Miss University Africa (2017) lililofanyika Cambodia tarehe 20 Desemba, 2017.Membo Bi. Queen Elizabeth alikuja kumsalimu Naibu Waziri na kuomba ushirikiano kutoka Wizarani na Serikalini kwa ujumla katika kutekeleza mpango wake wa kutangaza amani Duniani na kusaidia jamii.

Mhe. Naibu Waziri alimshukuru kwa kuja kumsalimia na kumpongeza kwa ushindi alioupata ambao unaitangaza Tanzania nje ya mipaka ya nchi.

Alimtaka ajivunie ushindi huo aliopata na kuwa mfano mzuri kwa wasichana wengine katika masomo na kuhudumia jamii inayomzunguka. Alimuahidi ushirikiano wa Wizara katika masuala ambayo ameazimia kuyafanya kwa ajili ya Jamii na kuitangaza Tanzania.
Mrembo Bi. Queen Elizabeth Manule ni mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Shahada ya Kwanza (Public Sector Accounting and Finance) katika Chuo cha Uhasibu (TIA).
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Dkt.Susan Kolimba akisalimiana na Bi. Queen Elizabeth Manule walipokutana kwa mazungumzo Wizarani jijini Dodoma

Naibu Waziri Mhe. Dkt.Susan Kolimba akimsiliza Mrembo Bi. Queen Elizabeth Manule wapokutana kwa mzungumzo Wizarani jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.