Friday, April 6, 2018

Waziri Mahiga aongoza kumbukumbu za Wataalam wa Kichina waliokufa wakati wa ujenzi wa Reli ya TAZARA



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), pamoja na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke  wakiweka mashada ya maua kwenye mnara uliopo kwenye makaburi ya wataalam 70 kutoka China waliokufa wakati wa ujenzi wa Reli ya Tazara, wakati wa maadhimisho ya utamaduni wa Wachina na kuwakumbuka wataalam hao yaliyofanyika kwenye eneo la makaburi walikozikwa wataalam hao lililopo Gongo la mboto, Dar es Salaam. Maadhimisho hayo yalihudhuriwa pia na Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi na Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Bw. Joseph Butiku. 
Dkt. Mahiga pamoja na Viongozi mbalimbali kutoka Serikalini wakitoa heshima zao kwa kuinamisha vichwa kama ishara ya kuwakumbuka wataalam hao kutoka China.  


Dkt. Mahiga akiweka Ua katika moja ya kaburi la wataalam hao.Wanaoshuhudia ni Balozi wa China, Mhe. Wang Ke, Prof. Palamagamba Kabudi, Bw. Joseph Butiku na viongozi wengine.
Dkt. Mahiga akihutubia katika hafla hiyo mara baada ya kumaliza zoezi la kuweka maua kwenye makaburi ya wataalam wa kichina waliokufa wakati wa ujenzi wa reli ya Tazara. Katika Hotuba hiyo waziri mahiga aliendelea kuusifu ushirikiano wa Tanzania na China katika sekta mbalimbali, ambapo  Ujenzi wa reli ya Tazara ulipelekea kuanzishwa kwa  viwanda mbalimbali, vikiwemo Kiwanda cha nguo cha Urafiki, Kiwanda cha dhana za kilimo cha Ufi, ambavyo vilipelekea chachu ya maendeleo Tanzania. 
Naye Balozi Wang Ke naye akitoa hotuba yake wakati wa hafla hiyo.
Dkt. Mahiga akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza hafla hiyo.
Dkt. Mahiga akiweka saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya vifo vya wataalam hao.








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.