Thursday, April 19, 2018

Wizara ya Mambo ya Nje kutumia fursa za maadhimisho ya kitaifa katika kutekeleza Diplomasia ya Uchumi.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha pamoja kati ya wafanyabiashara na kamati ya maandalizi ya wiki ya Tanzania nchini Kenya inayotarajiwa kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (KICC) Jijini Nairobi, Kenya kuanzia tarehe 25 hadi 28 Aprili 2018 ambapo kilele cha wiki hiyo ni tarehe 26 April 2018 siku ya maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanzania.

Balozi Mwinyi alitumia fursa hiyo kuwaaga wafanyabiashara na wajumbe wa kamati wanaoenda nchini Kenya kuratibu wiki hiyo  ambapo alisisitiza umuhimu wa kutumia fursa hiyo muhimu katika kuliletea taifa maendeleo kwakua kukua kwa biashara nchini kutaleta ajira, kutakuza pato la taifa na mabadiliko katika ustawi wa maisha ya wananchi kwa ujumla.

Balozi Mwinyi akiwa na viongozi wa kamati ya maandalizi ya wiki ya Tanzania nchini Kenya, wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE) ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati, Bw. Edwin Rutageruka, wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni katibu wa kamati, Balozi Anisa Mbega, wa kwanza kulia  ni mwakilishi kutoka Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa kamati hiyo, Bi. Lilian Ndosi na wa kwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya kati ambaye pia ni katibu msaidizi wa kamati, Bw. Suleiman Saleh. 

Sehemu ya wafanyabiashara waliothibitisha ushiriki katika maonesho ya bidhaa za Tanzania nchini Kenya wakifuatilia taarifa mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na viongozi wa kamati.

Sehemu nyingine ya wajumbe wa kamati, wadhamini na wafanyabiashara watakaoshiriki katika maonesho  hayo wakifuatilia kikao.

Wajumbe wakifuatilia kikao.

Picha ya pamoja meza kuu na wajumbe wa kamati ya maandalizi ya wiki ya Tanzania nchini Kenya.

Picha ya pamoja meza kuu, wadhamini na wafanyabiashara watakaoshiriki katika wiki ya Tanzania nchini Kenya.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.