Wednesday, April 4, 2018

Katibu Mkuu akutana na Ujumbe kutoka Ubalozi wa Japan



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Aldof Mkenda(Kulia) akifafanua jambo kwa Kaimu Balozi wa Japan nchini Bw. Hiroyuki Kubota katika mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Wizara, Dar es Salaam, tarehe 03 Aprili,2018. 

Mazungumzo hayo yalijikita katika kuboresha mahusiano ya Tanzania na nchi ya Japan. Prof. Mkenda alisema Mahusiano ya Tanzania na Japan ni  ya Kihistoria na katika kuendelea kudumisha mahusiano haya na kwa kuzingatia Japan ni kati ya nchi zinazosifika katika Teknolojia mbalimbali za kisasa, aliwakaribisha kuongeza uwekezaji katika eneo hilo. Naye Bw. Kubota aliahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mbalimbali hasa katika kujenga uwezo wa wataalamu wa Tanzania ili kuweza kushiriki vyema katika uchumi wa Viwanda.
                                     

     Mazungumzo yakiendelea, wanaofuatilia mazungumzo hayo kutoka kushoto ni Maafisa kutoka Ubalozi wa Japan na kulia ni Maafisa kutoka Wizarani.
                                      
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.