Friday, April 6, 2018

Balozi Mwinyi akutana na Wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya Maonyesho ya Bidhaa za Viwanda Vya Tanzania nchini Kenya

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi akizungumza na wajumbe wa kamati maalum ya maandalizi na Wadhamini wa maonesho ya bidhaa za viwanda vya Tanzania nchini Kenya kwa ajili ya kueleza mikakati mbalimbali itakayowezesha utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa vitendo katika kuelekea Tanzania ya Viwanda. Kikao hicho kilifanyika Ijumaa 6 Aprili  2018.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi na wadhamini wa maonesho ya bidhaa za viwanda vya Tanzania nchini Kenya wakisikiliza kwa makini maelekezo ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi wakati wa kikao baina yao kilichofanyika leo Ijumaa April 6, 2018.
Baadhi ya wadhamini wa maonesho ya bidhaa za viwanda vya Tanzania nchini Kenya wakifuatilia kwa makini maelekezo ya Balozi Mwinyi hayupo pichani
Balozi Ramadhan Mwinyi akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) Bw. Edwin Rutageruki ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya maonesho hayo mara baada ya kumalizika kwa kikao.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya LAKEGAS, Rajesh Chidambarani (katikati) ambaye pia ni mmoja wa wadhamini akibadilisha mawazo na Balozi Mwinyi mara baada ya kumalizika kwa kikao.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (katikati) akibadilisha mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Ramadhani Mwinyi na Meneja Mkuu wa Kampuni ya mafuta ya LAKEGAS, Rajesh Chidambarani mara baada ya kumalizika kwa mkutano baina yao tarehe 6 Aprili 2018.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi (wa tano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya maandalizi na wadhamini wa maonesho ya bidhaa za Viwanda vya Tanzania nchini Kenya tarehe 6 Aprili 2018.








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.