Thursday, April 5, 2018

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akimkaribisha Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Balozi Sara Catherine cooke, alipomtembelea Wizarani kwa ajili ya mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mkutano wa Wizara tarehe 4 Aprili,2018, Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine yalijikita kwenye ushiriki wa Tanzania katika Mkutano wa Wakuu wa Serikali na nchi za Umoja wa Madola (CHOGM), Mkutano huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 16-20, Jijini London, Uingereza. 

 Prof. Mkenda akifafanua jambo kwa Balozi Sarah Cooke katika mazungumzo hayo.

 Mazungumzo yakiendelea, wanaofuatilia mazungumzo hayo ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy(katikati kulia), anayefuata ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Bw. Deusdedit Kaganda na wa mwisho kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi Bw. Mark Thayre.

Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.