Tuesday, April 3, 2018

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda akutana kwa mazungumzo na Balozi wa China nchini


Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke. Katika mazungumzo yao waligusia umuhimu wa kuimarisha  ushirikiano kati ya Tanzania na China hususan kwenye sekta ya elimu. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani, Dar es Salaam tarehe 03 Aprili, 2018.
Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke kwa pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinga iliyopo Moshi Vijijini, Bi. Martina Mroso wakisaini Cheti cha Makabidhiano ya Mchango kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa matundu 16 ya Vyoo na Bwalo la Kulia Chakula katika Shule ya Msingi Msinga. Thamani ya Mchango huo ni shilingi milioni 32.
Mwalimu Mroso akimshukuru Balozi Wang Ke kwa mchango waliotoa kwa ajili ya kuisaidia Shule ya Msingi Msinga iliyopo Moshi Vijijini.
Maafisa kutoka Ubalozi wa China.
Balozi Shiyo na Balozi Wang Ke wakiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu Mroso (wa tatu kushoto) pamoja na wajumbe wengine walioshiriki mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.