Wednesday, May 9, 2018

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Balozi wa Ujerumani nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda(kulia) akiwa katika mazungumzo na  Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Detlef Waechter alipomtembelea wizarani tarehe 9 Mei,2018, Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine mazungumzo hayo yalilenga katika kuendelea kuboresha mahusiano yaliyopo kati ya Tanzania na Ujerumani.
Mazungumzo yakiendelea, wanaofuatilia mazungumzo hayo ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy( Katikati kulia), kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Justus Nyamanga na kulia kwake ni Afisa Mambo ya Nje, Bi Lilian Kimaro.



Dkt, Mahiga afungua Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania, Israel



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akikata utepe kuashiria ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel Ufunguzi huo ulifanyika jijini Tel Aviv tarehe 08 Mei 2018. Wengine katika picha ni Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked na Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked na Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima.wakigongesheana glasi kwa ajili ya kuwatakia afya njema viongozi wa mataifa yao, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Israel.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga wakisalimiana na Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked walipowasili kwa ajili ya kushiriki ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiweka saini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili kwenye ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel kwa ajili ya kuzifungua rasmi. Anayemwangalia ni Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked Add caption

Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked akiweka saini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili kwenye ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel kwa ajili ya kushiriki ufunguzi rasmi wa ofisi hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akibadilishana mawazo na Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked walipowasili kwa ajili ya kushiriki ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel.

 caption

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwahutubia mamia ya watu hawapo pichani waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel. Pembeni yake ni Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet.

Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked akiwahutubia mamia ya watu hawapo pichani waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel. Kushoto ni Waziriwa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga na kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima.

Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima akiwahutubia mamia ya watu hawapo pichani waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel. Waliokaa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Ayelet Shaked.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watanzania wanaoishi Israel.



Bi. Kisa Doris Mwaseba (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Watanzania wanaoishi Israel.

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambaye anaiwakilisha pia Tanzanaia nchini Uswisi, Mhe. Dkt. Abdallah Possi akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga katika Uwanja wa Ndege wa Zurich. Dkt. Possi alikuja kumpokea na kumsindikiza Mhe. Waziri akiwa njiani kuelekea Israel.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Dkt, Mahiga afungua Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania, Israel

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga amezindua rasmi ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Israel na kuitaka Israel nayo iharakishe kufungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania.

Ufunguzi wa ofisi hiyo ya ubalozi iliyopo katika mji wa Tel Aviv ulifanyika leo na ulihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Ayelet Shaked, Mabalozi wa nchi za Afrika na Watanzania wanaoishi nchini humo.

Katika hotuba yake, Dkt. Mahiga aliitaja Israel kama nchi ya kupigiwa mfano kwa sababu licha ya changamoto za kimahusiano na baadhi ya jirani zake lakini bado nchi hiyo imepiiga hatua kubwa za kimaendeleo katika sekta mbalimbali zikiwemo kilimo cha umwagiliaji, viwanda, matibabu, TEHAMA, ulinzi na usalama, uhifadhi wa maji na masuala ya nishati ikiwemo nishati ya kutumia joto ardhi.

Kwa upande wa ulinzi na usalama, Waziri Mahiga alisema Watanzania hawataisahau Israel kwa kuwa ndiyo nchi iliyoisaidia Tanzania kuanzisha Jeshi la Kujenga Taifa ambalo mafanikio na mchango wa jeshi hilo unajulikana na kila Mtanzania. Alisema JKT baada ya lugha ya Kiswahili ndiyo chombo cha pili kilichosaidia kwa kiasi kikubwa kuunganisha makabila zaidi ya 120 ya Watanzania na kuwa wamoja hadi leo.

Dkt. Mahiga alieleza kuwa Israel ni nchi yenye mafanikio makubwa duniani ambapo imepelekea raia wake wengi kushinda tuzo za Nobel na hiyo imetokana na harakati zao kwa ajili ya wanadamu.

Aliishukuru Israel kufuatia mawaziri wake wawili kufanya ziara za kikazi nchini Tanzania hivi karibuni. Mawaziri hao ni Waziri wa Ulinzi, Mhe. Avigdor Liberman aliyetembelea Tanzania tarehe 20 hadi 22 Machi 2018 na Waziri wa Sheria, Mhe. Ayelet Shaked ambaye alikuwa nchini tarehe 23 na 24 Aprili 2018.

Katika ziara hizo masuala mbalimbali yaliafikiwa ikwemo Israel kuisaidia Tanzania kuanzisha chombo cha kutoa msaada wa kisheria kwa wasiojiweza ambacho kwa upande wa Israel kimeshaanzishwa na kina mafanikio makubwa.

Dkt.Mahiga aliwakaribisha Waisrael kuja Tanzania kwa ajili ya kufanya utalii kwa kuwa Tanzania ina vivutio lukuki vya utalii. Alisema zaidi ya watalii elf 50 wanakuja Tanzania kila mwaka lakini hawatoshi kutokana na uwingi wa vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Kwa upande wake, Mhe. Shaked alibainisha kuwa Israel ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo kusaidia teknolojia ya kisasa kwenye kilimo ili kuongeza tija katika uzalishaji.
Aidha, Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima alishukuru wadau wote ikiwemo Serikali ya Israel kwa kumpa ushirikiano wa kutosha uliofanikisha upatikanaji wa ofisi hiyo na kufunguliwa rasmi tarehe 08 Mei 2018. Aliwahakikishia umma uliohudhuria hafla hiyo na wadau wengine kuwa wasisite kufika kwenye ofisi hiyo kwa ajili ya kupata huduma watakazozihitaji.      
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Israel
09 Mei 2017


Tuesday, May 8, 2018

Balozi Mushy akutana na Mabalozi kutoka nchi zinazounda kundi la Unitedfor Consensus


       
     
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy(kulia) akisisitiza jambo kwa Balozi wa Italy Nchini Mhe. Roberto Mengoni(kushoto), kwenye mazungumzo na Mabalozi wa Nchi zinazounda kundi linaloitwa United for Consensus ambazo zinakaa na kujadiliana kwa pamoja kuhusu mabadiliko yanayotakiwa kufanyika katika Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa  ( UN Security Council), walipotembelea Wizarani, tarehe 08 Mei,2018, Dar es Salaam.

Mabalozi kutoka Nchi zinazounda kundi linaloitwa United for Consensus wakifuatilia mazungumzo hayo kutoka kulia ni Balozi wa Pakistan nchini, Mhe. Amir Mohamed Khan, balozi wa Hispania nchini, Mhe. Felix Costales, Balozi wa Canada nchini, Mhe. Alexander Leveque, Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Song Geum Yong na Mwisho ni Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Ali Davutaglu.
Mhe. Roberto Mengoni akifafanua jambo kwenye mazungumzo hayo.
Mkutano ukiendelea.
Picha ya pamoja baada ya mazungumzo.




Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Kampuni ya kutengeneza magari ya Foton.

Katibu Mkuu  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Bw. Apple Sun, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Kutengeneza Magari ya Foton Motors Group Kenya,
 Mazungumzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara, Tarehe 08 Mei,2018, Dar es Salaam.

Katika kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli za Tanzania mpya ya Viwanda na pia katika kuendelea kutekeleza Diplomasia ya Uchumi, Prof.Mkenda alitumia mazungumzo hayo kuishawishi kampuni hiyo kujenga kiwanda cha kutengeneza magari hapa nchini, Kampuni hiyo iwapo itajenga kiwanda hicho hapa nchini itachangia kwa kiwango kikubwa kuongeza ajira kwa Watanzania na pia kusaidia katika juhudi za kutunza mazingira kwani itapunguza uagizaji wa magari yaliyotumika ambayo huchangia katika uharibifu wa mazingira. 

Prof. Mkenda amewahakikishia ushirikiano kutoka Serikalini iwapo watajenga kiwanda hicho hapa nchini.Kampuni hiyo kutoka nchini China inatengeneza magari mbalimbali kama vile pick-up, magari ya kawaida, SUV, maroli, matrekta n.k yenye kutumia teknologia ya hali ya juu na  ubora mkubwa.   
Kwa sasa Kampuni hiyo ina Kiwanda cha kutengeneza magari (Assembling Plant) nchini Kenya. 

Naye Bw. Sun alisema Kampuni yake iko tayari kwa mazungumzo na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuona uwezekano wa kujenga Kiwanda hicho hapa nchini, hata hivyo kwa sasa wameishafungua ofisi ya uwakilishi hapa nchini. 

Bw. Justin Kisoka(Kushoto) na Bw. Bernard Msuya, Maafisa Mambo ya Nje kutoka Wizarani wakifuatilia Mkutano huo.
Bw. Apple Sun akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.


Mkutano ukiendelea

Picha ya Pamoja baada ya mazungumzo

Sunday, May 6, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO HABARI


TAARIFA KWA VYOMBO HABARI
Waziri Mahiga kuzuru Israel
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) atafanya ziara ya kikazi nchini Israel kuanzia tarehe 07 hadi 10 Mei 2018. Ziara hiyo imekuja kufuatia mwaliko wa mwenyeji wake ambaye ni Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Mhe. Benjamin Netanyahu. Dkt. Mahiga anakuwa Waziri wa kwanza wa Mambo ya Nje kutoka Tanzania kufanya ziara nchini Israel.
Atakapowasili nchini Israel, Dkt. Mahiga atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Mhe. Netanyahu na kushiriki uzinduzi rasmi wa Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini humo.
Ikumbukwe Israel ni moja kati ya nchi sita ambazo Serikali ya awamu ya tano imefungua Balozi Mpya. Mhe. Job Masima aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuwa Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini humo.
Waziri Mahiga ataitumia ziara hiyo sio tu kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo bali pia kuishawishi Serikali ya Israel iunge mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wa viwanda.
Israel ni moja ya nchi zenye maendeleo makubwa duniani katika sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, viwanda, uhifadhi wa maji, matibabu, ulinzi na usalama, mawasiliano na nishati ya joto ardhi. Hivyo kupitia ziara hiyo, agenda ya uchumi wa viwanda ya Tanzania inaweza kupata ushirikiano mkubwa wa Israel kutokana na hatua kubwa ya kimaendeleo iliyofikia.
Kabla ya Tanzania haijafungua ofisi ya Ubalozi Israel, ilikuwa inawakilishwa kupitia ubalozi wake Misri na Ubalozi wa Israel nchini Kenya unawakilisha pia Tanzania hadi sasa.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
 06 Mei, 2018

Saturday, May 5, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Wizara ya Mambo ya Nje imejipanga kutekeleza Sera ya Uchumi wa Viwanda
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wametakiwa kufanya kazi kwa weledi ili kutimiza malengo ya Serikali ya awamu ya tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda. Kauli hiyo ilitolewa leo jijini Dar Es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.)  wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Waziri Mahiga alieleza kuwa Wizara inatakiwa kuweka Sera na mikakati ya utekelezaji kwa kuzingatia miongozo na maelekezo ya Viongozi wa juu akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
“Sera ya Serikali ya awamu ya tano ni kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda, hivyo Sera yetu ya Mambo ya Nje lazima ijikite katika diplomasia ya uchumi wa viwanda”. Dkt. Mahiga alieleza.
 Dkt. Mahiga alihitimisha hotuba yake kwa kuwataka watumishi kuhakikisha kuwa Wizara inatekeleza majukumu yake kwa kujiwekea ratiba ya kuyakamilisha kwa kuzingatia hotuba za Mhe. Rais Magufuli  alizozitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kikao cha Mabalozi na Mhe. Rais Magufuli na kikao cha watumishi wa Wizara na   Mhe. Rais Magufuli. 

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda amesema  kuwa Wizara yake imejipanga ipasavyo  kuhakikisha kwamba jukumu la kuchochea uchumi wa nchi kupitia Sera ya Mambo ya Nje inayojikita katika  diplomasia ya uchumi inatekelezwa kikamilifu.
Prof. Mkenda alisema Wizara kwa kushirikiana na ofisi zake za Ubalozi, licha ya changamoto mbalimbali inazokutana nazo, lakini imekuwa ikitafuta fursa za uwekezaji, mitaji, masoko, utalii na elimu na kuzileta nchini ili kufikia azma ya Serikali ya awamu ya tano  inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2020.

Alizitaja Balozi chache zilizoleta wafanyabiashara wakubwa kwa ajili ya kutafuta fursa za uwekezaji nchini kuwa  ni pamoja na Balozi za Tanzania nchini China, Ufaransa, Korea Kusini, Kenya, Ujerumani na Israel. "Balozi wetu China, Mhe. Mbelwa Kairuki
ametafuta taasisi za kifedha kwa ajili ya kuzikopesha benki za Tanzania ili zikuze mitaji ya kutoa mikopo kwa wawekezaji. Aidha, Serikali ya Ujerumani imefungua ofisi maalum kwa ajili ya kuratibu na kusaidia shughuli za kibiashara na uwekezaji hapa nchini" Prof. Mkenda alisema.

Prof. Mkenda alisifu jitihada zilizofanywa na Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya hivi karibuni za kuandaa maonesho ya bidhaa za viwanda vya hapa nchini yaliyofanyika jijini Nairobi tarehe 25 - 28 Aprili 2018. Alisema maonesho hayo ya kipekee yalikuwa na mafanikio makubwa ambapo wafanyabiashara walioshiriki waliingia makubaliano na wafanyabiashara wa Kenya ya kupeleka bidhaa zao nchini Kenya.
"Tunatakiwa tuondoe vikwazo vya kufanya biashsra, kuondoa vikwazo hivyo haina maana Tanzania iwe gulio la kuuzia bidhaa kutoka nje, bali wafanyabiashara wetu wanatakiwa kuchangamkia masoko ya nje ili wauze bidhaa zao kwa wingi nje ya nchi", Katibu Mkuu alisisitiza.
Katibu Mkuu alisema ili watumishi waweze kutimiza malengo ya Wizara yakiwemo ya kuvutia wawekezaji kutoka nje, Wizara imejipanga kuwawezesha watumishi kupata elimu, ujuzi, teknolojia na uzoefu unaohitajika kutimiza majukumu hayo.
Kuhusu suala la kupeleka watumishi kwenye vituo vya Ubalozi, Katibu Mkuu alieleza kuwa Wizara itatekeleza jukumu hilo kwa haki kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa ambavyo ni weledi, ujuzi na mahitaji ya Balozi husika. “Wizara haitapeleka watumishi vituoni kutokana na shinikizo au kuangalia sura, kabila na dini ya mtu ili kuondoa malalamiko yaliyokuwepo kwa muda mrefu Wizarani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
 05 Mei, 2018

Ziara ya Waziri Heiko Maas Jijini Arusha


Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Mhe. Heiko Maas akiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), tayari kwa kuendelea na ziara yake katika mkoa wa Arusha, ambapo amekutana na viongozi wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari (United Nations Mechanism for International Criminal Tribiunals-MICT) na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (African Court on Human and Peoples' Rights). Pia ametembelea Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
Mhe. Maas akiambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya Bw. Jestas Nyamanga (mwenye tai ya Njano) mara baada ya kuwasili uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro.
Mhe. Maas (kulia) akisalimiana na Afisa mahusiano wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari Bw. Ousman Njikam, mara baada ya kuwasili katika mahakama hiyo.
Bw. Njikam akimtambulisha Msajili Mkuu wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari (United Nations Mechanism for International Criminal Tribiunals-MICT) Bi. Sera Attika kwa Waziri Haeko Maas
Waziri Maas. akiweka saini kwenye kitabu cha wageni kilichoandaliwa kwenye mahakama hiyo.
Bw. Njikam akielezea namna mahakama hiyo inavyofanya kazi kwa Waziri Maas, wa kwanza kulia ni Bi. Attika na wapili kutoka kushoto ni Afisa mwandamizi wa mahakama hiyo Bi. Thembile Segoete wakisikiliza kwa makini.
Bi. Attika akimwelezea jambo Mhe. Maas
Waziri Haeko Maas, pamoja na Bw. Nyamanga wakiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari.
Rais wa Mahakama ya Haki za Binadamu na watu Mhe. Jaji Sylvain Ore (wa kwanza kulia) akiongozana na Waziri wa Ujerumani Mhe. Haeko Maasi mara baada ya kuwasili kwenye Mahakama hiyo tayari kwakufanya mazungumzo, mazungumzo hayo yameudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Jestas Nyamanga. Makao Makuu ya Mahakama hiyo yapo jijini Arusha.
Waziri Haeko Maasi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt Libérat Mfumukeko walipokutana na kufanya mazungumzo. 
Mhe. Haeko Maas akizungumza na Majaji wa mahakama hiyo (hawapo pichani)
Sehemu ya Majaji wa Mahakama hiyo wakimsikiliza kwa makini Mhe. Maas (hayupo pichani)
Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya Bw. Jestas Nyamanga akifuatilia kwa mikini mazungumzo hayo kati ya Jaji Sylvain Ore (hawapo pichani)
Jaji Ore akimkabidhi Mhe. Maas zawadi ya Nembo ya Mahakama hiyo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Waziri Haeko Maasi pamoja na Jaji Sylvain Ore wakiwa katika picha ya pamoja na majaji wa mahakama pia na ujumbe ulioambatana na Mhe. Maas.
Waziri Haeko Maasi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt Libérat Mfumukeko walipokutana na kufanya mazungumzo. 

Mhe. Maas pamoja na Dkt. Mfumukeko wakiwa kwenye mazungumzo

Mazungumzo yakiendelea.
Dkt Libérat Mfumukeko (wa nne kutoka kulia), Waziri Haeko Maas (watatu kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja