Saturday, May 5, 2018

Ziara ya Waziri Heiko Maas Jijini Arusha


Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Mhe. Heiko Maas akiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), tayari kwa kuendelea na ziara yake katika mkoa wa Arusha, ambapo amekutana na viongozi wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari (United Nations Mechanism for International Criminal Tribiunals-MICT) na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (African Court on Human and Peoples' Rights). Pia ametembelea Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
Mhe. Maas akiambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya Bw. Jestas Nyamanga (mwenye tai ya Njano) mara baada ya kuwasili uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro.
Mhe. Maas (kulia) akisalimiana na Afisa mahusiano wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari Bw. Ousman Njikam, mara baada ya kuwasili katika mahakama hiyo.
Bw. Njikam akimtambulisha Msajili Mkuu wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari (United Nations Mechanism for International Criminal Tribiunals-MICT) Bi. Sera Attika kwa Waziri Haeko Maas
Waziri Maas. akiweka saini kwenye kitabu cha wageni kilichoandaliwa kwenye mahakama hiyo.
Bw. Njikam akielezea namna mahakama hiyo inavyofanya kazi kwa Waziri Maas, wa kwanza kulia ni Bi. Attika na wapili kutoka kushoto ni Afisa mwandamizi wa mahakama hiyo Bi. Thembile Segoete wakisikiliza kwa makini.
Bi. Attika akimwelezea jambo Mhe. Maas
Waziri Haeko Maas, pamoja na Bw. Nyamanga wakiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Mahakama ya Kesi ya Masalaia za Mauaji ya Kimbari.
Rais wa Mahakama ya Haki za Binadamu na watu Mhe. Jaji Sylvain Ore (wa kwanza kulia) akiongozana na Waziri wa Ujerumani Mhe. Haeko Maasi mara baada ya kuwasili kwenye Mahakama hiyo tayari kwakufanya mazungumzo, mazungumzo hayo yameudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Jestas Nyamanga. Makao Makuu ya Mahakama hiyo yapo jijini Arusha.
Waziri Haeko Maasi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt Libérat Mfumukeko walipokutana na kufanya mazungumzo. 
Mhe. Haeko Maas akizungumza na Majaji wa mahakama hiyo (hawapo pichani)
Sehemu ya Majaji wa Mahakama hiyo wakimsikiliza kwa makini Mhe. Maas (hayupo pichani)
Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya Bw. Jestas Nyamanga akifuatilia kwa mikini mazungumzo hayo kati ya Jaji Sylvain Ore (hawapo pichani)
Jaji Ore akimkabidhi Mhe. Maas zawadi ya Nembo ya Mahakama hiyo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Waziri Haeko Maasi pamoja na Jaji Sylvain Ore wakiwa katika picha ya pamoja na majaji wa mahakama pia na ujumbe ulioambatana na Mhe. Maas.
Waziri Haeko Maasi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt Libérat Mfumukeko walipokutana na kufanya mazungumzo. 

Mhe. Maas pamoja na Dkt. Mfumukeko wakiwa kwenye mazungumzo

Mazungumzo yakiendelea.
Dkt Libérat Mfumukeko (wa nne kutoka kulia), Waziri Haeko Maas (watatu kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja

























No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.