Monday, May 28, 2018

Waziri Mahiga atembelea Ubalozi wa Palestina nchini

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Augustine Mahiga akisaini kitabu cha maombolezo ya Wapelestina waliouwa kwenye Ukanda wa Gaza hivi karibuni, Mhe.Waziri Mahiga alisaini kitabu hicho alipotembelea katika Ubalozi huo tarehe 28 Mei,2018, anayeshuhudia ni Balozi wa Palestina hapa nchini Mhe. Balozi Hazem Shabat.

 Mhe. Waziri Mahiga akipata maelezo kutoka kwa Mhe. Balozi Shabat kuhusu sanaa ya picha inayoelezea utamaduni wa Wapalestina, aliyesimama kushoto ni Naibu Balozi wa Palestina hapa nchini Bw.Derar Ghannam.

 Mhe. Waziri Mahiga akisisitiza jambo katika mazungumzo yaliyofanyika Ubalozini hapo, lengo la mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine ni kuzidi kuboresha mahusiano yaliyopo kati ya Tanzania na Palestina.
 Mhe. Waziri Mahiga akiwa ameshikilia moja ya picha yenye maelezo ya kuhimiza haki ya Wapalestina  ya kuishi.
 Mhe. Balozi Shabat akimfafanulia jambo kwenye Kitabu alichomkabidhi Mhe. Waziri Mahiga kama zawadi, Kitabu hicho kinaelezea Historia ya Mji wa Yerusalem.



Mhe. Waziri Mahiga akiagana na mwenyeji wake baada ya mazungumzo.

Sehemu ya maelezo ya sanaa ya picha zilizopo Ubalozini hapo, picha hizi zinaelezea kuhusu Amani katika Palestina na Haki ya Kuishi ya Wapalestina.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.