Monday, May 14, 2018

Waziri Mahiga aelezea ziara yake Israel kuwa ya mafanikio

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), amefanya mkutano na waandishi wa habari kuwaelezea yaliyojiri kuhusu ziara yake ya kikazi nchini Israel. Wakati wa ziara hiyo Mhe. Waziri Mahiga alikutana na Waziri Mkuu wa Israel, Mhe. Benjamin Netanyau na kufanya nae mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano. Mhe. Waziri Magiga pia alifungua rasmi Ubalozi wa Tanzania nchini humo.
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki waliohudhuria mkutano huo wa Waziri na waandishi wa habari, wa kwanza kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati Bw. Suleiman Saleh, wa pili kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga,  kushoto ni Katibu wa Waziri Bw. Magabilo Murobi na Afisa Mambo ya Nje Bi. Kisadoris Mwaseba.
Sehemu ya waandishi wa habari waliohudhuria kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.