Thursday, May 3, 2018

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani awasili nchini kuanza ziara ya kikazi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Zanzibar, Mhe. Issa Haji Gavu (kushoto) akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Mhe. Heiko Maas alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili nchini tarehe 03 na 04 Mei, 2018.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Mhe. Heiko Maas akisalimiana na Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Detlef Waechteralipowasili nchini kwa ziara ya siku mbili. Anayeshuhudia ni Mhe. Waziri Gavu.
Mhe. Waziri Maas akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga.


Mhe. Waziri Maas akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga huku Bw. Nyamaga akishuhudia
Mhe. Waziri Gavu akizungumza na Mhe. Waziri Maas mara baada ya kumpokea rasmi nchini kwa ajili ya kuanza ziara yake ya siku mbili.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.