Tuesday, May 8, 2018

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Kampuni ya kutengeneza magari ya Foton.

Katibu Mkuu  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Bw. Apple Sun, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Kutengeneza Magari ya Foton Motors Group Kenya,
 Mazungumzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara, Tarehe 08 Mei,2018, Dar es Salaam.

Katika kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli za Tanzania mpya ya Viwanda na pia katika kuendelea kutekeleza Diplomasia ya Uchumi, Prof.Mkenda alitumia mazungumzo hayo kuishawishi kampuni hiyo kujenga kiwanda cha kutengeneza magari hapa nchini, Kampuni hiyo iwapo itajenga kiwanda hicho hapa nchini itachangia kwa kiwango kikubwa kuongeza ajira kwa Watanzania na pia kusaidia katika juhudi za kutunza mazingira kwani itapunguza uagizaji wa magari yaliyotumika ambayo huchangia katika uharibifu wa mazingira. 

Prof. Mkenda amewahakikishia ushirikiano kutoka Serikalini iwapo watajenga kiwanda hicho hapa nchini.Kampuni hiyo kutoka nchini China inatengeneza magari mbalimbali kama vile pick-up, magari ya kawaida, SUV, maroli, matrekta n.k yenye kutumia teknologia ya hali ya juu na  ubora mkubwa.   
Kwa sasa Kampuni hiyo ina Kiwanda cha kutengeneza magari (Assembling Plant) nchini Kenya. 

Naye Bw. Sun alisema Kampuni yake iko tayari kwa mazungumzo na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuona uwezekano wa kujenga Kiwanda hicho hapa nchini, hata hivyo kwa sasa wameishafungua ofisi ya uwakilishi hapa nchini. 

Bw. Justin Kisoka(Kushoto) na Bw. Bernard Msuya, Maafisa Mambo ya Nje kutoka Wizarani wakifuatilia Mkutano huo.
Bw. Apple Sun akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.


Mkutano ukiendelea

Picha ya Pamoja baada ya mazungumzo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.