Friday, May 11, 2018

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Frederic Clavier, alipomtembelea Wizarani tarehe 10 Mei,2018, Jijini Dar es Salaam,  mazungumzo hayo yalijikita katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ufaransa.

Akiongea katika mazungumzo hayo Katibu Mkuu alimshukuru Mhe. Clavier kwa ushirikiano huo hasa kwa kuwezesha ziara ya wafanyabiashara kutoka Ufaransa hapa nchini na kuendelea kusaidia miradi mbalimbali. 
Naye kwa upande wake Mhe. Clavier alisema anafurahishwa sana na kasi ya Maendeleo hapa nchini na wataendelea kumuunga mkono  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli katika juhudi zake za kujenga uchumi wa Viwanda,pia alisema ataendelea kushawishi wawekezaji wengi kuja hapa nchini na pia kuendelea kusaidia miradi mbalimbali hapa nchini.

 Mkutano ukiendelea, wanaofuatilia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa ni Balozi Celestine Mushy(wa tatu kutoka kulia), anayefuata ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestus Nyamanga na wengine ni Maafisa kutoka Wizarani na Ubalozi wa Ufaransa.
Picha ya Pamoja baada ya mazungumzo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.