Wednesday, May 23, 2018

Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yapitishwa na Bunge


   
Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisoma hotuba ya bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/2019 bungeni jijini Dodoma. 

Mapema leo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepisha kiasi cha Shilingi Bilioni Mia Moja Sabini na Saba, Milioni Sita na Mia Mbili Thelathini na Mbili Elfu.

 Kati ya fedha hizo Shilingi Bilioni Mia Moja Sitini na Sita, Milioni Mia Sita na Sita, na Mia Mbili Thelathini na Mbili Elfu ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, na Shilingi Bilioni Kumi na Milioni Mia Nne ni kwa ajili ya bajeti ya maendeleo.
Pro. Adolf F. Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,(wa kwanza kushoto) akifuatilia uwasilishwaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara. Wa pili kutoka kushoto, ni Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhani Mwinyi akifuatilia hotuba.

Sehemu ya Watendaji wa Wizara wakifuatilia hotuba ya bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/2019 iliyowasilishwa na kupishwa bungeni jijini Dodoma

Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akijibu maswali bungeni mara baada ya kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/2019

Mhe. Dkt. Susan Kolimba Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kushoto), akifuatilia hotuba ya bajeti bungeni jijini Dodoma

Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo mara baada ya kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara.

Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisalimiana na Dkt. Stergomena Tax Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) walipokutana katika viunga vya Bunge jijini Dodoma mara baada kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara.

Mhe. Waziri Mahiga akijadili jambo na Mhe. Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma Mjini katika viunga vya Bunge jijini Dodoma mara baada ya kupitishwa kwa hotuba ya bajeti ya Wizara

Mhe. Waziri  Mahiga na Mhe. Naibu Waziri Kolimba wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi na Watendaji wa Wizara waliohudhuria tukio la uwasilishwaji wa bajeti ya Wizara bungeni jijini Dodoma






HOTUBA YA MHESHIMIWA BALOZI DKT. AUGUSTINE PHILIP MAHIGA (MB), WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA BAJETI YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019



ORODHA YA VIFUPISHO
AF
Adaptation Fund
AfDB
African Development Bank
AfCFTA
African Continental Free Trade Area
AGOA
African Growth and Opportunity Act
AICC
Arusha International Conference Centre
AMISOM
African Union Mission to Somalia
APRM
African Peer Review Mechanism
BBC
British Broadcasting Corporation
CGTN
China Global Television Network
COMESA
Common Market for Eastern and

Southern Africa
COP
Conference of Parties
DW
Deutsche Welle
EAC
East African Community
EPA
Economic Partnership Agreement
FAO
Food and Agriculture Organization

FIB
Force Intervention Brigade

FOCAC
Forum on China-Africa Cooperation

ii



GCF
Green Climate Fund
GEF
Global Environment Facility
GIZ
The Deutsche Gesellschaft für
Internationale Zusammenarbeit GmbH

GPEDC
Global Partnership for Effective

Development Cooperation
IAEA
International Atomic Energy Agency
IGAD
Intergovernmental Authority on

Development
ILO
International Labour Organization
IMF
International Monetary Fund
IOM
International Organization for Migration
IORA
Indian Ocean Rim Association
JNICC
Julius Nyerere International Convention

Centre
KCB
Kenya Commercial Bank
KOICA
Korea International Cooperation Agency
LDCF
Least Developed Countries Fund









iii


MINUSCA                   United Nations Multidimensional Integrated

Stabilisation Mission in the Central African Republic

MK-ICC                       Mt. Kilimanjaro International Convention

Centre

MONUSCO               United Nations Organisation Stabilisation

Mission in the Democratic Republic of the Congo

NPT                                 Non – Proliferation Treaty

PSPF                             Public Sector Pension Fund

RFI                                  Radio France International

RMB                               Renminbi

SADC                            Southern African Development

Community

SDGs                             Sustainable Development

Goals

TAZARA                     Tanzania-Zambia Railway Authority

TBC                                Tanzania Broadcasting Corporation

TEHAMA                   Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

TIC                                  Tanzania Investment Centre

TMEA                           Trademark East Africa

UKIMWI                      Upungufu wa Kinga Mwilini





iv


UNAMID


United Nations African Union Mission in Darfur



UNDP


United Nations Development Progamme




UNDAP



United Nations Development Assistance Plan



UNEP


United Nations Environment Progamme





UNESCO


United Nations Educational Scientific and Cultural Organization



UNFPA


United Nations Population Fund



UN-HABITAT


United Nations Human Settlement Programme



UNHCR


United Nations High Commission for Refugees



UNICEF


United Nations Children’s Emergency Fund



UN-ICTR


United Nations International Criminal Tribunal for Rwanda



UNIDO


United Nations Industrial Development Organization



UNIFIL


United Nations Interim Force in Lebanon



UNISFA


United Nations Interim Security Force for Abyei




v


UNMISS                       United Nations Mission in the Republic

of South Sudan

UTT                                 Unit Trust of Tanzania

VoA                                 Voice of America

WHO                              World Health Organization


WTO                               World Trade Organization

WWF                              World Wildlife Fund






vi


UTANGULIZI

1.   Mheshimiwa Spika, baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara, naomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mpango na bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka wa fedha 2017/18. Aidha, naomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/19.

2.   Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa fadhila na rehema, kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana tena katika Bunge lako Tukufu, kujadili Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yangu.

3.   Mheshimiwa Spika, naungana na wenzangu walionitangulia kuwashukuru na kuwapongeza watoa hoja waliozungumza kabla yangu, hususan Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na Mheshimiwa Dkt. Philip Isdory Mpango (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango ambao kwa hakika hotuba zao sio tu zimezungumzia mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano, bali pia zimetoa dira katika mustakabali wa taifa letu kwa kuainisha masuala muhimu ya kitaifa, kikanda na kimataifa ambayo baadhi yake yanagusa majukumu ya Wizara yangu.



1


4.   Mheshimiwa Spika, naomba pia nitumie fursa hii kutoa shukrani zangu kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama chini ya uongozi wa Mhe. Mussa Azan Zungu (Mb) na Makamu wake Mhe. Salum Mwinyi Rehani (Mb). Kamati hii imetoa mchango mkubwa na imekuwa muhimili muhimu katika kuiwezesha Wizara yangu kutekeleza majukumu yake kwa kutoa ushauri kuhusu masuala mbalimbali ya kiutendaji.

5.   Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naomba nitumie nafasi hii kuwashukuru Mheshimiwa Dkt. Susan Alphonce Kolimba (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki; Prof. Adolf Faustine Mkenda, Katibu Mkuu; Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi, Naibu Katibu Mkuu; mabalozi wa Tanzania nje ya nchi; Wakuu wa Idara na Vitengo; watumishi wa Wizara; na taasisi zilizo chini ya Wizara yangu kwa kujituma na kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kufanikisha kwa kiwango cha juu utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18, pamoja na kuandaa Bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha 2018/19.

Friday, May 18, 2018

Balozi Dkt. Possi awasilisha Hati za Utambulisho kwa Baba Mtakatifu Papa Francis

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambaye anawakilisha pia na Vatican, Mhe. Dkt. Abdallah Saleh Possi, akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Baba Mtakatifu Papa Francis, Vatican tarehe 17 Mei 2018. 

Kabla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho, Balozi Dkt. Possi alipata fursa ya kukutana na viongozi muhimu wa Vatican, wakiwemo Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu Mkuu wa Mambo ya Nchi za Nje na ushirikiano wa kimataifa, Askofu Mkuu Angelo Becciu, Katibu Mkuu Msaidizi wa Vatican.

Mabalozi wengine waliowasilisha Hati za Utambulisho ni pamoja na Balozi Ahmad Naseem Warraich kutoka Pakistan, Balozi Risto Piipponen kutoka Finland, Balozi Lundeg Purevsuren kutoka Mongolia, Balozi Retšelisitsoe Calvin Masenyetse kutoka Lesotho, Balozi Karsten Vagn Nielsen kutoka Denmark,  na Balozi Sulaiman Mohammed kutoka Ethiopia. 

Baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho, Balozi Dkt. Possi alipata fursa ya kukutana na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Vatican. Katika kikao hicho, Dkt. Possi aliwaeleza Watanzania hao kwamba wana jukumu kubwa la kutumia.nafasi zao kuhakikisha nchi ya Tanzania inadumu katika misingi ya uadilifu, umoja, na amani ambavyo ni misingi muhimu ya maendeleo.

Balozi Dkt. Possi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin.

Balozi Dkt. Possi na Mama Balozi, Bi. Sada Mshana, katika picha ya pamoja na Baba Mtakatifu Papa Francis. Picha kwa hisani ya Vatican


Thursday, May 17, 2018

Balozi Shiyo afunga mafunzo ya mfumo wa Ufuatiliaji na Taathmini wa SADC

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Innocent E. Shiyo (Katikati) akifunga  Warsha ya siku tatu(3) ya Mafunzo ya Mfumo wa Ufuatialiaji na Tathmini wa SADC (SADC Results Based Online Monitoring and Evaluation System), mmoja wa Wakufunzi wa Warsha hiyo kutoka SADC Bi. Lerato Moleko(kulia) na wa mwisho  kushoto ni Bw. Meneja Mradi kutoka GIZ Bw. Robson Chakwama. 

 Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Wizara kwa kushirikiana  na Serikali ya Ujerumani chini ya Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) na Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), yametolewa kwa Maafisa wa Serikali na Taasisi za Umma, tarehe 15 - 17 Mei,2018 katika ukumbi wa Mikutano wa  Mwalimu Nyerere, Jijini Dar es Salaam.
 Hafla hiyo ikiendelea
 Sehemu ya Maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia hafla ya kufunga mafunzo hayo
 Sehemu ya Washiriki wakifuatilia hafla ya kufunga mafunzo hayo
 Bi. Felister Rugambwa ambaye alikuwa Mshereheshaji wa shughuli hiyo akitoa utaratibu wa shughuli.
Picha ya Pamoja baada ya shughuli hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika akutana na Balozi wa Italia nchini

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga akizungumza na Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberto Mengoni alipofika Wizarani kwa mazungumzo kuhusu ushirikiano baina ya Tanzania na Italia.
 Bi. Tunsume Mwangolombe, Afisa Mambo ya Nje akinukuu mazungumzo kati ya Bw. Nyamanga na Balozi Mengoni(hawapo pichani)

PRESS RELEASE-SADC VACANCY ANNOUNCEMENT






PRESS RELEASE

VACANCY ANNOUNCEMENT FROM THE SOUTHERN AFRICA DEVELOPMENT COMMUNITY SECRETARIAT (SADC)

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received 50 vacant positions from the Southern Africa Development Community Secretariat (SADC) inviting qualified Tanzanians to apply. The vacant positions are open to all 16 member countries.

Interested Tanzanians are required to present their application letters not later than or on 30th May 2018 through the following address:-

Permanent Secretary,
President's Office,
Public Services Management
University of Dodoma,
P.O.Box 670,
40404 DODOMA.

Applicants may also send their application letters through this Email address: - ps@utumishi.go.tz or shiyo27@yahoo.co.uk.  

For further details please visit the following websites: - www.sadc.int or www.utumishi.go.tz or www.foreign.go.tz. We are sending  an attachment of the stated positions with this press release.

NB: The SADC positions are highly competitive. Thus, interested candidates are advised to send their Curriculum Vitae that meets regional and international standards.

Issued by:
Government Communication Unit,
 Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dar es Salaam.
17th May 2018

=========================================================