Monday, September 17, 2018
Dkt. Gwajima azindua ziara ya kitabibu Wilayani Kondoa
Sehemu ya Watumishi kutoka wilaya ya Kondoa wakimsikiliza kwa makini Dkt. Gwajima alipokuwa akihutubia kwenye ufunguzi wa Ziara ya Madaktari na wauguzi |
Sehemu ya Wananchi waliojitokeza kwenye Ufunguzi huo wakimikiliza kwa makini Dkt. Gwajima |
Juu na chini sehemu ya wananchi wakiendelea kusikiliza hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa kwenye uzinduzi huo.
Juu na chini sehemu ya wananchi wakianza kupata huduma za kiafya mara baada ya kufanyika kwa uzinduzi huo
Picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa zoezi la ufunguzi |
Balozi Anisa Mbega akiagana na Dkt. Gwajima mara baada ya kumaliza ufunguzi wa Ziara ya Madaktari na Wauguzi. |
Sunday, September 16, 2018
Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Mabalozi wa India na Qatar waliopo nchini
Katika hatua nyingine, Prof. Mkenda alikutana na Balozi wa Qatar nchini na kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Tanzania na Qatar. |
Maadhimisho ya Saba ya Siku ya Mara (Mara Day) yafanyika Kenya
Gavana wa akaunti ya Narok, Mhe. Samuel Oletunai akihutubia watu mbalimbali walioshiriki maadhimisho ya Siku ya Mara ambayo yalifanyika katika kaunti yake ya Narok. |
Watu mbalimbali waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Mara wakifuatilia hotuba za viongozi. |
Mwakilishi wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) akivalishwa vazi la kimasai kabla hajatoa hotuba yake katika maadhimisho hayo. |
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Bibi Caroline Mthapula ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima akitoa neno la mkoa katika maadhimisho hayo. |
Kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dkt. Pindi Chana; Katibu Tawala wa mkoa wa Mara, Bibi Caroline Mthapula; Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Juma Aweso; Waziri wa Maji na Usafi wa Kenya, Mhe. Simon Chelugui wakipata maelezo kutoka moja ya banda la maonesho ya Siku ya Mara kuhusu utunzaji wa mazingira. |
Mstari wa kulia kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dkt. Pindi Chana; Katibu Tawala wa mkoa wa Mara, Bibi Caroline Mthapula; Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Juma Aweso; Waziri wa Maji na Usafi wa Kenya, Mhe. Simon Chelugui wakipata maelezo kutoka mmoja wa washiriki wa maonesho ya siku ya Mara namna anavyoshiriki katika shughuli za kutunza mazingira. |
Kaimu Murugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Kijamii, Bw. Eliabi Chodota akiteta jambo na Katibu Tawala wa mkoa wa Mara, Bibi Caroline Mthapula. |
Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria maadhimisho ya saba ya Siku ya Mara wakisikiliza hotuba za viongozi. |
Burudani kutoka kwa wanafunzi wakihimiza umuhimu wa kutunza mazingira. |
Mmoja wa wanaharakati wa kutunza Mazingira akipokea cheti cha kutambua mchango wake kutoka kwa Gavana wa kaunti ya Narok, Mhe. Samuel Oletunai. katikati ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria, Dkt. Ally Said Matano. |
Friday, September 14, 2018
Prof. Mkenda na Balozi wa Kenya wakutana kujadili utatuzi wa changamoto za biashara mipakani
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dan Kazungu walipokutana jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya. Pamoja na mambo mengine walijadili changamoto za biashara hususan tukio la hivi karibuni la kukwamishwa kwa bidhaa za Tanzania kuingia Kenya kwa sababu mbalimbali ikiwemo vinywaji, mchele na unga wa ngano. Katika kikao hicho ilikubalika Tanzania kuitisha kikao cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Afrika Mashariki na Biashara na Wakuu wa Mamlaka za Mapato za Tanzania na Kenya. Pia walikubaliana kuendelea kuratibu ziara za viongozi wa juu kati ya nchi hizi mbili kwa lengo la kukuza mahusiano. |
Prof. Mkenda na Balozi Kazungu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo yao. |
Thursday, September 13, 2018
Waziri Mahiga afungua rasmi Ofisi za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kwa pamoja na Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Detlef Waechter wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Ofisi Ndogo ya Uwakilishi wa Ubalozi wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani jijini Dodoma. Ofisi hiyo ni ya kwanza kwa Balozi za nje zilizopo Tanzania kufunguliwa Dodoma. Ufunguzi huo ni katika kuitikia wito wa Mhe. Rais baada ya Serikali kuhamia rasmi Dodoma. Ofisi hizo ambazo zipo ghorofa ya nne katika Jengo la PSPF Barabara ya Benjamin Mkapa zitatoa huduma mbalimbali kwa Serikali, Bunge na Wananchi kwa ujumla huku zikisimamiwa na Bw. Richard Shaba ambaye ni Mtanzania. Pia Ofisi hizo zimejumuisha Mashirika ya Misaada ya Ujerumani ambayo ni GIZ na KFW. |
Mhe. Waziri Mahiga kwa pamoja na Balozi Waechter wakifungua kitambaa kuashiria kuwa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani zimefunguliwa rasmi jijini Dodoma |
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo aliipongeza Serikali ya Ujerumani kwa uamuzi huo ambao ni ishara njema kwamba nchi hiyo inaunga mkono kwa dhati uamuzi wa Serikali wa kuhamia Dodoma. Pia alisema Tanzania ina mengi ya kujifunza kutoka Ujerumani kwani nchi hiyo ina uzoefu wa kuhamisha makao makuu kutoka Bonn kwenda Berlin ambapo ilifanya hivyo miaka 30 iliyopita |
Mhe. Waziri Mahiga akiendelea na hotuba yake. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (wa nne kushoto), Balozi Waechter (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga (kushoto), Msimamizi wa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma, Bw. Richard Shaba (wa tatu kushoto), Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu (wa pili kushoto na Wawakilishi kutoka GIZ na KFW. |
Mhe. Balozi Waechter nae akizungumza ambapo alisema wamefungua Ofisi hizo ili kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo katika nyanja mbalimbali kati ya Tanzania na Ujerumani |
Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika picha na Mhe. Balozi Waechter pamoja na viongozi wengine walioshiriki hafla hiyo |
Mhe. Waziri Mahiga akimpongeza Balozi Waechter ufunguzi wa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma |
Wageni waalikwa walioshiriki ufunguzi wa Ofisi hizo wakifuatilia matukio mbalimbali |
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na vyombo vya habari |
Awali Mhe. Waziri Mahiga alisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani zilizopo jijini Dodoma. Kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Detlef Waechter. Wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Binilith Mahenge na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga |
Mhe. Waziri Mahiga, Mhe. Balozi Waechter na Mkuu wa Dodoma Dkt. Mahenge wakiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa walioshiriki hafla hiyo wakiwemo Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki |
Picha ya pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi wa Ujerumani nchini |
Wednesday, September 12, 2018
Tanzania ilivyoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara nchini Msumbiji
Balozi wa Tanzania
nchini Msumbiji, Mheshimiwa Rajabu Luhwavi, (katikati), akikaribishwa katika Maonesho ya Biashara ya
Kimataifa ya 54 ya FACIM yaliyofanyika tarehe 27 Agosti
hadi 2 Septemba 2018 Maputo nchini Msumbiji. Wengine ni Bw. Albert
Philipo, Afisa wa Wizara, Idara ya Diaspora (kushoto) na ndugu Nelson Nkini,
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania (Diaspora) wanaoishi nchini Msumbiji Ushiriki wa wafanyabiashara kutoka Tanzania
uliratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Msumbiji kwa kushirikiana na Mamlaka ya
Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).
|
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Msumbiji, Mheshimiwa Carlos Agostinho do Rosário wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya 54 ya FACIM alipotembelea banda la Tanzania na kukaribishwa na Bi. Getrude Ngweshemi, Kaimu Meneja - Masoko ya Ndani wa TanTrade na Bw. Albert Philipo, Afisa Idara ya Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje ambapo alipatiwa maelezo kuhusu bidhaa za viwandani pamoja na vivutio vya utalii wa Tanzania. |
Balozi Rajabu Luhwavi akifafanua jambo kwa
wafanyabiashara na washiriki kutoka mataifa mengine (hawapo pichani) waliofika katika banda la
Tanzania wakati maonesho ya biashara ya 54 ya FACIM yakiendelea. Wafanyabiashara wa Tanzania walikutana na
wafanyabiashara wenzao kutoka mataifa zaidi ya 20 ambapo walibadilishana mawazo
na kuzitangaza bidhaa na huduma za Tanzania katika maonesho hayo.
|
Balozi Rajabu Luhwavi akipokea maelezo kutoka kwa Afisa wa
Wizara, Bw. Albert Philipo kuhusu bidhaa za Tanzania zilizoletwa na
wafanyabiashara mbambali kutoka Tanzania wakati wa maonesho ya biashara ya
kimataifa ya 54 ya FACIM Maputo, Msumbiji. Wengine katika picha hiyo ni wafanyabiashara
kutoka Kampuni mbalimbali nchini Tanzania.
|
Mheshimiwa Balozi Rajabu Luhwavi akitoa maelezo mafupi wakati
wa ufunguzi wa Maonyesho ya Biashara Nampula yaliyohusisha wafanyabiashara
kutoka Tanzania. Kwa upande wake Balozi Luhwavi, alieleza kuwa
maonesho haya ni ya kimkakati kwa ajili ya kukuza na kuimarisha umoja,
mshikamano na mahusiano ya kiuchumi yaliyojengwa na waasisi wetu hayati Mwalimu
Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
hayati Sheikh Abeid Amani Karume, aliyekuwa rais wa kwanza wa Zanzibar na
hayati Samora Moises Machel, aliyekuwa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Msumbiji.
Maonesho haya yalifungua fursa za masoko kwa bidhaa za viwanda vya Tanzania
pamoja na kuendeleza juhudi za utekelezaji wa diplomasia ya uchumi kwa vitendo
na kukuza uchumi, hususan uchumi wa viwanda.
|
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Ndugu Juma Ali Juma aliyekuwa mgeni rasmi wakati wa kilele cha maonesho ya bidhaa za viwanda vya Tanzania mjini Nampula akiwa pamoja na Balozi Rajabu Luhwavi na Katibu Mkuu wa Jimbo la Nampula, Bi. Veronica Langa wakipata maelezo kuhusu teknolojia ya ufugaji samaki kutoka kampuni ya Dokaman ya nchini Tanzania. |
Kutoka kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mheshimiwa Rajabu Luhwavi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Ndugu Juma Ali Juma, Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara TanTrade, Bi. Anna Bulondo wakipata maelezo kutoka kwa wawakilishi wa kampuni ya A - Z Textile Mills. |
Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mheshimiwa Rajabu Luhwavi akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Ndugu Juma Ali Juma wakipokea maelezo kuhusu bidhaa zinazotengenezwa na Kampuni ya Tanzania M/s Darsh Industries wakati wa maonesho ya bidhaa za viwanda mjini Nampula, Msumbiji. |
Subscribe to:
Posts (Atom)