Sunday, September 16, 2018

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Mabalozi wa India na Qatar waliopo nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa India nchini, Mhe. Sandeep Arya. Katika mazungumzo yao wamekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ya manufaa kwa nchi zote mbili.

Katika hatua nyingine, Prof. Mkenda alikutana na Balozi wa Qatar nchini na kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Tanzania na Qatar.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.