Thursday, September 20, 2018

Maonesho Maalum ya Utalii yaendelea nchini India

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akizungumza na wadau mbalimbali walioshiriki maonesho maalum  ya kutangaza vivutio vya utalii na kuanza kwa safari za Air Tanzania nchini India. Maonesho hayo yalifanyika mjini Gujarat. Ubalozi huo kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) umeandaa maonesho maalum kwenye miji mbalimbali ya India huku tayari maonesho ya aina hiyo yakiwa yamefanyika mjini New Delhi tarehe 17 Septemba, 2018. Safari za shirika la ndege la Tanzania kupitia ndege yake mpya ya Dreamliner zitaanza safri mjini Mumbai mwezi Novemba, 2018 kwa lengo la kurahisisha usafiri kwa watalii, wafanyabiashara na wanafunzi kutoka India kuja nchini.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.