Monday, September 17, 2018

Dkt. Gwajima azindua ziara ya kitabibu Wilayani Kondoa

Mkurugenzi wa Tiba wa Wizara ya Afya, Dkt. Dorothy Gwajima akihutubia kwenye uzinduzi wa ziara ya Madaktari Wauguzi kutoka taasisi binafsi ya Health Education Development (HEAD INC) ya watanzania waishio nchini Marekani ya kutoa huduma za kitabibu  kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa. Dkt. Gwajima alitumia fursa hiyo kuwapongeza taasisi hiyo kwakuona umuhimu wa kuja nyumbani kutoa huduma za afya kwa watanzania wenzao. Dkt. Gwajima hakusita kuipongeza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Idara ya Diaspora kwa kuwezesha kufanikisha Ziara ya Madaktari na Wauguzi hao kutoka Nchini Marekani ambapo inaonyesha namna mwitikio wa Watanzania waishio nje ya nchi katika kuchangia maendeleo nchini.  Madaktari na Wauguzi hao watakuwa kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa kwa siku nne (4) wakitoa huduma za Afya kwa wagonjwa mbalimbali. 
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Sezaria Makutta (wa kwanza kushoto), na Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Anisa Mbega wakimsikiliza kwa makini Dkt. Gwajima alipokuwa akihutubia kwenye ufunguzi wa ziara ya Madaktari na Wauguzi kutoka (Head Inc)
Sehemu ya Watumishi kutoka wilaya ya Kondoa wakimsikiliza kwa makini Dkt. Gwajima alipokuwa akihutubia kwenye ufunguzi wa Ziara ya Madaktari na wauguzi 
Sehemu ya Wananchi waliojitokeza kwenye Ufunguzi huo wakimikiliza kwa makini Dkt. Gwajima
Mkuu wa Wilaya Kondoa Mhe. Sezaria Makutta naye alipata fursa ya kuwakaribisha Madaktari na Wauguzi hao kwenye Wilaya ya Kondoa na kuwaahidi kuwapa ushirikiano wa kutosha kwa kipindi chote cha siku nne watakachokuwa wanatoa huduma za Afya katika Hospitali hiyo.
Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora Wizara ya Mambo ya NJe na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Anisa Mbega naye alipata Fursa ya kuwasalimia wananchi wa Wilaya ya Kondoa walio jitokeza kwenye Uzinduzi wa Ziara hiyo ya Madaktari na Wauguzi, pia alitumia fursa hiyo Kuwashukuru wanadiaspora kwa kuendelea kuchangia maendeleo ya nchini kwa namna mbali mbali ikiwemo kuleta ujuzi wao,  kuwekeza kwenye sekta mbalimbali. Pia aliushukuru uongozi wa Wilaya ya Kondoa kupitia Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Sezaria Makutta kwa maandalizi na mapokezi mazuri ya ziara hiyo. 

 Juu na chini sehemu ya wananchi wakiendelea kusikiliza hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa kwenye uzinduzi huo.

 Juu na chini sehemu ya wananchi wakianza kupata huduma za kiafya mara baada ya kufanyika kwa uzinduzi huo

Picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa zoezi la ufunguzi
Balozi Anisa Mbega akiagana na Dkt. Gwajima mara baada ya kumaliza ufunguzi wa Ziara ya Madaktari na Wauguzi.










No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.