Saturday, September 22, 2018

Ubalozi wa Tanzania nchini India wahitimisha maonesho maalum ya utalii

Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bibi Devotha Mdachi akizungumza wakati wa kuhitimisha maonesho maalum ya utalii yaliyofanyika  nchini India kwenye baadhi ya miji mikubwa ya New Delhi, Mumbai, na Ahmedabad. Maonesho hayo ambayo yalifanyika kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini India yalilenga kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini ikiwemo Hifadhi za Taifa za Wanyama kama Ngorongoro, Serengeti, fukwe zilizopo Zanzibar na Mlima Kilimanjaro. Pia wakati wa maonesho hayo Balozi wa Tanzania nchini India Mhe. Baraka Luvanda alitumia fursa hiyo kutangaza kuanza rasmi kwa safari za Shirika la Ndege la Tanzania mjini Mumbai mwezi Novemba 2018. 
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akizungumza na mmoja wa wadau  kutoka India aliyeshiriki maonesho hayo maalum ya utalii

Afisa kutoka Tanzania akitoa ufafanuzi kwa wadau mbalimbali wa sekta ya utalii ya India walioshiriki maonesho
ya maalum ya utalii yaliyoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini humo kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania

Wadau mbalimbali wa sekta ya utalii wakijadili masuala mbalimbali kuhusu sekta hiyo na kubadilishana uzoefu 

Mtaalam kutoka Tanzania akitoa ufafanuzi kwa mdau wa sekta ya utalii wa nchini India

Balozi Luvanda akiwa na mmoja wa wadau walioshiriki maonesho hayo


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.