Saturday, March 14, 2020

PROF. KABUDI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE KUJITOA MHANGA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akifungua rasmi Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara lililofanyika kwenye Ukumbi wa Hazina jijini Dodoma tarehe 14 Machi, 2020. Pamoja na mambo mengine, Mhe. Prof. Kabudi amewataka Wafanyakazi wa Wizara hiyo kutekeleza majukumu yao kwa kujituma na kutanguliza mbele maslahi ya Taifa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara, Bw. Issa Ng'imba wakati wa ufunguzi wa  Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika jijini Dodoma

Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara hiyo uliofanyika jijini Dodoma
Sehemu nyingine ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nao wakifuatilia hotuba ya Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara hiyo uliofanyika jijini Dodoma
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Ibuge naye akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika jijini Dodoma
Mhe. Prof. Kabudi na wajumbe wengine wakimsikiliza Katibu Mkuu, Balozi Kanali Ibuge (hayupo pichani)
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Baraza hilo
Naibu Katibu Mkuu TUGHE-Taifa, Bw. Amani Simon Msuya akiwa na Mwakilishi wa TUGHE-Dodoma wakifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Wajumbe wa Baraza la Wafanayakazi wakiwa kwenye ufunguzi wa mkutano
Sehemu nyingine ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye ufunguzi wa mkutano wa Baraza hilo
Wajumbe wa Baraza wakiwa kwenye ufunguzi wa mkutano
Naibu Katibu Mkuu TUGHE-Taifa, Bw. Msuya nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu TUGHE-Taifa, Bw. Msuya (hayupo pichani)

Sehemu nyingine ya Wajumbe wa Baraza
Mjumbe wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Zanzibar, Balozi Mohammed Hamza akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza hilo wakati wa ufunguzi 


Sehemu ya Wajumbe wa Baraza wakimsikiliza Balozi Hamza (hayupo pichani)
Wajumbe wa Baraza
Wajumbe wengine wa Baraza
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu, Balozi Ibuge na Wajumbe wa TUGHE-Taifa na Wizarani
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ambao pia ni Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi mara baada ya kufungua rasmi Mkutano wa Baraza hilo
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wote wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Thursday, March 12, 2020

Balozi Amour katika juhudi za kutafuta fursa nchini Kuwait

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhandisi Aisha S. Amour amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Fawaz Al-Khaled Al-Hamad Al-Sabah, Gavana wa Mkoa wa Ahmadi, Kuwait.  Uongozi huo wa Mkoa wa Ahmadi ulionyesha utayari wa kushirikiana na Mkoa mmojawapo wa Tanzania katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo mara baada ya kukubaliana kwa kupitia Wizara ya Mambo Nje ya Kuwait.

Mhe. Mhandisi Aisha S. Amour, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait akipokea zawadi ya alama ya Mkoa toka kwa Mhe. Fawaz Al-Khaled Al-Hamad Al-Sabah, Gavana wa Mkoa wa Ahmadi, Kuwait katika ofisi za Mkoa huo, ambapo Mhe. Balozi alifanya ziara.

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhandisi Aisha S. Amour atembelea ofisi za Mamlaka ya Kilimo na Uvuvi ya Kuwait na kufanya mazungumzo na Mhe.Mohamed Al-Yousef Al-Sabah, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo.  Mkurugenzi huyo alieleza utayari wa kushirikiana na Mamlaka za Tanzania katika sekta ya kilimo na uvuvi kwa ajili ya kubadilishana uzoefu katika tafiti na teknolojia mbalimbali hasa katika mbegu, kilimo cha umwagiliaji, pamoja na kilimo cha kitalu nyumba.
 Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhandisi Aisha S. Amour atembelea mashamba ya tafiti wa kilimo cha mbogamboga kwa upandaji wa kawaida. Kushoto kwa Mhe. Balozi ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Utafiti wa mazao, Dr. Reem Ahmed Al-Hazeem.
Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhandisi Aisha S. Amour akiangalia uzalishaji wa bilinganya kwa ajili ya utafiti kwa kwa njia ya kitalu nyumba, ‘greenhouse.

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait Mhandisi Aisha S. Amour akingalia uzalishaji wa matango kwa ajili ya utafiti kwa njia ya kitalu nyumba.
 Balozi wa Tanzania nchini Kuwait. Mhe. Mhandisi Aisha S. Amour alikutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Balozi Abdulhamid Al-Failakawi, Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje ya Kuwait – Idara ya Afrika. Katika mazungumzo hayo, Mhe. Balozi Eng. Aisha aliwasilisha salamu za shukrani kwa Serikali ya Kuwait kwa ushirikiano mkubwa katika ujenzi wa miradi ya maendeleo kwa kupitia Kuwait Fund. Aidha, alieleza fursa mbalimbali za uwekezaji, biashara na Utalii zilizopo Tanzania na kumuomba kuwezesha katika kukutana na Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali ya Kuwait ili kuangalia uwezekano wa ushirikiano kati ya Kuwait na Tanzania katika nyanja mbalimbali.
Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Mhandisi Aisha S. Amour afanya mazungumzo na Bw. Emad Abdullah Al-Zaid, Mkurugenzi Msaidizi wa Kuwait Chamber of Commerce & Industry kuhusu kupanga mikakati ya kuwakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania na Kuwait pamoja na kutangaza fursa mbalimbali zilizopo Tanzania. 

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Mhandisi Aisha S. Amour atembelea kiwanda cha AlHomaizi Food kiwanda cha kuchakata nafaka.  Al-Homaizi ni Kampuni mama ya Alrifai ambayo imeanza kununua korosho za Tanzania na kuzisafirisha nchi za Mashariki ya kati ikiwa ni pamoja na Kuwait.

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhandisi Aisha S. Amour akiwa katika maabara ya kiwanda hicho, akipewa maelezo namna ya upimaji ubora wa mazao ya nafaka kabla ya kuchakata na baada.

 Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhandisi Aisha S. Amour akutana na kufanya mazungumzo na Bw. Ahmad A. Eid, Mkurugenzi Mtendaji wa Ushirika wa Kuwait Shipping Companies & Agent Association kuhusu fursa za uwekezaji na usafirishaji wa baharini. Bw. Ahmad alieleza utayari wa kuleta meli nchini Tanzania kuchukua mizigo ya biashara moja kwa moja kutoka Tanzania mpaka Kuwait.
Balozi wa Tanzania nchini Kuwait. Mhandisi Aisha S. Amour,  akutana na kufanya mazungumzo viongozi wa Umoja wa Watalii Kuwait kuhusu masuala ya utalii Tanzania. Katika mazungumzo na viongozi hao ambao wanawanachama Zaidi ya 150, ilikubalika kuandaa kwa safari ya watalii Zaidi ya 70 kuja Tanzania mwezi Julai 2020. Aidha, viongozi hao walikubali kuwa mabalozi wa utalii wa Tanzania nchini Kuwait.
 Balozi wa Tanzania nchini Kuwait. Mhe. Mhandisi Aisha S. Amour akutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Automobile Agents kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania katika sekta hiyo. Viongozi hao walikubali kufikisha taarifa kwa wajumbe wa umoja wao na kujipanga kufika Tanzania kuangalia utaratibu wa uwekezaji katika sekta yao ya magari.

Wednesday, March 11, 2020

NAIBU WAZIRI DKT. NDUMBARO AKUTANA NA MABALOZI WA UINGEREZA, NORWAY NA KOREA


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Balozi Sarah Cooke, Balozi wa Norway nchini Mhe. Balozi Elisabeth Jacobsen pamoja na Balozi wa Korea nchini Mhe. Balozi CHO tae-ick.

Dkt. Ndumbaro amekutana na mabalozi hao leo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili masuala ya kuongeza ushirikiano wa kidiplomasia pamoja na mikakati ya kujikinga na kupambana na homa ya virusi vya corona.

Pia, Mabalozi hao waliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Kushirikiana na Jumuiya ya  Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika –SADC kwa maamuzi yake ya busara kupitia mawaziri wa Afya ya kuamua vikao vyote vinavyoendelea kufanyika kwa njia ya mtandao yaani (Video Conference) ikiwa ni hatua mathubuti ya kukabiliana  na maambukizi ya Ugonjwa huo.

Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiongea na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Balozi Sarah Cooke pamoja na Balozi wa Norway nchini Mhe. Balozi Elisabeth Jacobsen


Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Balozi Sarah Cooke akimuelezea jambo Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro. Katikati ni Balozi wa Norway nchini Mhe. Balozi Elisabeth Jacobsen.

Balozi wa Norway nchini Mhe. Balozi Elisabeth Jacobsen akimuuliza jambo Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro. Kushoto kwake ni Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Balozi Sarah Cooke.

Balozi wa Korea nchini Mhe. Balozi CHO tae-ick akiongea na Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro 


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro pamoja na Balozi wa Korea nchini Mhe. Balozi CHO tae-ick wakifuatilia taarifa kuhusu mikakati ya kujikinga na kupambana na homa ya virusi vya corona

Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akimfafanulia jambo Balozi wa Korea nchini Mhe. Balozi CHO tae-ick  






Tuesday, March 10, 2020

DKT. NDUMBARO AFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WA PALESTINA NA USWISI NCHINI


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Palestina nchini Mhe. Balozi Hamdi Mansour AbuAli Pamoja na Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher, katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo ya Mhe. Dkt. Ndumbaro pamoja na Balozi wa Palestina, Mhe. Balozi Abuali walikubaliana kuendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi hasa katika sekta ya uwekezaji wa kiwanda cha dawa na vifaa tiba pamoja na kilimo.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Dkt. Ndumbaro na Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher mazungumzo yao yalihusu maandalizi ya mpango mpya wa maendeleo wa mwaka 2021-2024 baina ya Tanzania na Uswisi yanayoendelea.

Mpango wa maendeleo uliopo unatarajiwa kufikia ukomo mwaka huu 2020. Ambapo mpango mpya utajikita zaidi katika kuimarisha sekta ya afya, mazingira, utawala bora na kukuza ajira kwa vijana na wanawake nchini.

Masuala mengine yaliyojadiliwa yalihusu programu ya Ukuzaji Ujuzi wa Ajira nchini (Skills for Employment Tanzania) na shuguli zinazofanywa na NGOs za Uswisi zilizopo nchini.

Pia Kaimu Balozi huyo alieleza kuwa Uswisi itaendelea kusaidia mradi wa malaria na kuchangia fedha katika Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Kwa upande wake Mhe. Dkt. Ndumbaro alisifu uhusiano baina ya nchi hizi mbili kwa kueleza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Uswisi katika kukuza zaidi mahusiano hayo.


Balozi wa Palestina Nchini Mhe. Balozi Hamdi Mansour AbuAli akimuelezea jambo Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiongea na Balozi wa Palestina Nchini Mhe. Balozi Hamdi Mansour AbuAli walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher akiongea na Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akimfafanulia jambo Kaimu Balozi wa Uswisi nchini Bw. Leo Nascher wakati wa mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI WA SADC



Saturday, March 7, 2020

Wafanyabiashara Mumbai Wahimizwa Kutumia Air Tanzania

Ubalozi wa Tanzania nchini India wakishirikiana na Shirika la Ndege la Tanzania [Air Tanzania] waliandaa Kongamano la Biashara na Uwekezaji lililofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Mumbai ambapo wafanyabiashara wapatao 40 kutoka Tanzania, Maofisa kutoka Kituo Cha Uwekezaji [Tanzania Investment Centre] na “Air Tanzania” walikutanishwa na wafanyabiashara, wawekezaji na wasafirishaji wa bidhaa wa India wapatao 60.

Pamoja na mambo mengine kongamano hilo lililenga kuwakutanisha wafanyabiashara, wawekezaji  na wasafirishaji wa bidhaa wa Tanzania na India ili kupanua wigo wa biashara kati ya Tanzania na India hususan, ununuzi wa bidhaa zinazozalishwa Tanzania kuja India. Wafanyabiashara wa Tanzania walipata fursa adhimu ya kubadilishana taarifa zinazohusu bidhaa zinazozalishwa kwa wingi Tanzania kwa minajili ya kupata  masoko zaidi ya bidhaa hizo na kuongeza idadi ya mizigo inayosafirishwa na ‘Air Tanzania’ kutoka Dar es Salaam kuja Mumbai.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda alieleza, pamoja na mambo mengine, kuwa Kongamano hilo litasaidia wafanyabiashara wa Tanzania kukutana na wenzao wa India na kuanzisha uhusiano wa kibiashara unaotarajiwa kufungua masoko zaidi ya bidhaa zao nchini baada ya wadau hao kupata maelezo ya kutosha kuhusu bidhaa wanazozalisha nchini na faida zake.

 Kwa ujumla, India ina soko kubwa la bidhaa. Hivyo,matarajio ni kuona  kiwango cha bidhaa kutoka Tanzania zinazouzwa India kinaongezeka zaidi hususan, baada ya kurejeshwa tena kwa ndege za Shirika la Ndege, Tanzania, kati ya Dar es Salaam na Mumbai mwezi Julai 2019.  Balozi Luvanda alitoa rai kwa wafanyabiashara hao kutumia usafiri wa ‘Air Tanzania’ kwa kuwa ni wa uhakika, wa muda mfupi zaidi na pia bei yake ni nafuu. Aidha, Mhe. Luvanda aliwaomba wafanyabiashara hao kuongeza ushirikiano na Tanzania katika utalii, hasa ikizingatiwa kuwa India inatoa watalii zaidi ya milioni 20 kwa mwaka kutembelea nchi mbalimbali duniani.
Akimwakilisha Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania, Bwana Patrick Ndekana alieleza historia ya Shirika hilo na hali ilivyo kwa sasa. Aidha, Bwana Ndekana aliwaeleza washiriki wa Kongamano kuwa Shirika hilo limejipanga kuhakikisha usafiri wa uhakika, bora na salama kwa kuwa linamiliki ndege mpya na za kisasa.

Vilevile, Bwana Ndekana alifafanua shabaha ya kuitisha Kongamano kuwa ilitokana na wadau mbalimbali kama vile wasafairishaji wa bidhaa kukosa taarifa za fursa za usafirishaji zilizopo kwenye shirika hilo. Hivyo, alieleza matarajio ni kuwa wadau hao wataweza kutumia zaidi usafiri wa Shirika hilo baada ya Kongamano hilo mahsusi.
Akiwasilisha mada kuhusu biashara na uwekezaji nchini Tanzania, Afisa kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania [TIC], Bwana Nestory Kissima alieleza kuwa Tanzania imefanya mabadiliko makubwa katika sera zake za kuvutia biashara na uwekezaji na amewaomba wafanyabiashara waliohudhuria kongamano hilo kuchangamkia fursa za biashara zilizopo Tanzania hususan, katika ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya asili ya biashara kama vile mkonge, pamba, korosho,madini,matunda mbalimbali kama vile parachichi, na nafaka mbalimbali pamoja na ununuzi wa mazao hayo ambayo yanahitajika sana nchini India.
Bwana Kissima alieleza kuwa, kwa kiasi kikubwa mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji nchini Tanzania yameboreshwa ikiwa ni pamoja na Serikali kufanyia kazi changamoto mbalimbali zilizokuwepo kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi. Jitihada hizo zinafanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kwenye viwanda na miradi ya kimkakati ifikapo 2025.inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli za kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati kupitia uwekezaji 
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akihutubia wakati wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji lililofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Mumbai tarehe 05 Machi 2020.
Kaimu Mkurugenzi wa Air Tanzania akizungumza katika 
Kongamano hilo.

Bwana Nestory Kissima, kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania [TIC ] akiwasilisha mada katika Kongamano hilo.

Umati wa washiriki wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji wakifuatilia hotuba zilizokuwa zikiwasilishwa na wataalamu mbalimbali katika Ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Mumbai tarehe 05 Machi 2020.