Thursday, October 8, 2020

BALOZI WA TANZANIA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO KWA MFALME WA LUXEMBOURG


 Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji ambaye anawakilisha pia nchini Luxembourg, Mhe. Jestas Abuok Nyamanga amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Mfalme wa Luxembourg, Grand Duke Henri tarehe 2 Oktoba 2020.

Wakati wa hafla hiyo, Balozi Nyamanga na Mfalme Henri walifanya mazungumzo kuhusu umuhimu wa kuongeza wigo wa ushirikiano baina ya nchi mbili hizi na kutumia ipasavyo fursa mbalimbali zilizopo kwa ajili ya manufaa ya pande mbili. Miongoni mwa maeneo ya ushirikano yaliyojadiliwa ni pamoja na ushirikiano wa anga hususan ndege za mizigo, ushirikiano katika sekta za kifedha na kibenki na sekta ya madini hususan madini ya chuma kama yale ya Mchuchuma na Liganga, eneo ambalo Luxembourg ina uzoefu mkubwa.

Matukio katika Ubalozi wa Tanzania, Abu Dhabi

KUTAFUTA SOLO LA KOROSHO

Mhe. Balozi Mohamed Mtonga alifanya mazungumzo na wafanyabiashara, Bw. Abdo Shamakh Al-Shibani wa kampuni ya SHAFA iliyopo Dubai na Bw. Dzhuraev Khairullo ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya FoodArt LLC yenye Makao Makuu yake mjini Moscow nchini Urusi. Kampuni ya FoodArt LLC imekuwa ikinunua korosho sehemu mbalimbali duniani na kuziuza katika nchi mbalimbali za Ulaya ikiwamo Urusi.

Mhe. Balozi Mtonga aliwaonesha fursa ya kuweza kununua zao la korosho kutoka Tanzania na kuwapa mwongozo wa ununuzi kama ulivyotolewa na Wizara ya Kilimo na Ushirika na Bodi ya Korosho Tanzania.

Kwa ujumla wafanyabiashara hao walionesha dhamira ya kununua zao la korosho kutoka Tanzania katika msimu huu wa mwaka 2020/2021.

KUKABIDHI UENYEKITI WA SADC

Mhe. Balozi Mohamed Mtonga alikabidhi Uwenyekiti wa SADC Group of Ambassadors hapa Abu Dhabi kwa Balozi wa Nchi ya Msumbiji. Mhe. Balozi Tiago Recibo Castigo. Balozi Tiago, alimshukuru Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa Mwenyekiti wa SADC aliyemaliza muda wake kwa mafanikio makubwa katika kipindi chake cha uenyekiti licha ya changamoto ya ugonjwa wa COVID-19.


KUTANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

Mhe. Mohamed Abdallah Mtonga, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu alifanya mazungumzo na Wakurugenzi wa Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Abu Dhabi (ADNOC), Bw. Khaled Salmeen, Bw. Iman Al Hosani, Bw. Mohamed Al Suwaidi na Bw. Abdulla Al Qubaisi kwa njia ya mtandao (Virtual Meeting).

Balozi alitumia fursa hiyo kuwajulisha fursa kadhaa zilizopo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia katika eneo hili la Mafuta na Gesi. Maeneo aliyowajulisha kwa uwekezaji ni yale yaliyohusu uwekaji wa miundombinu katika biashara ya Gesi na Mafuta. Aidha, Balozi aliwajulisha fursa za kibiashara katika biashara ya mbolea aina ya Urea kwa utaratibu wa Bulk Procurement System unaoratibiwa na Tanzania Fertilizers Regulatory Authority na uletaji wa Mafuta kwa pamoja unaoratibiwa na Bulk Procurement System for Petroleum Products. Bidhaa zote hizi huzalishwa na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Abu Dhabi (Abu Dhabi National Oil Company (ADNOC).

Vilevile, Balozi aliwasilisha kwa ADNOC miradi ambayo ipo tayari kwa uwekezaji iliyopo katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (Tanzania Investment Centre) ambayo inatafuta wawekezaji au wabia.

Miradi hiyo ni kama ifuatavyo:

·       Establishment of Strategic Petroleum Reserve Infrastructures (Farm Tanks).

Kwa mujibu wa andiko Mradi utajikita katika ujenzi wa Matanki ya kuhifadhia mafuta katika miji ya Dar Es Salaam, Morogoro, Isaka(Kahama),Makambako, Mbeya, Songwe na Tanga. Watekelezaji wa Mradi huu ni Mwekezaji Mshirika (Strategic Partner) na Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (Tanzania Petroleum Development Corporation). 

·       LPG Bulk Distribution Project

Kwa mujibu wa andiko Mradi huu ni kuweka miundombinu ya Kupokea,kuhifadhi na kuweka miundombinu ya kujaza Gesi aina ya LPG. Mradi huu utatekelezwa kwa awamu katika miji ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara. Watekelezaji wa Mradi huu ni Mwekezaji Mshirika (Strategic Partner) na Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (Tanzania Petroleum Development Corporation).

Kwa upande wao, Wakurugenzi wa ADNOC wamehitaji taarifa mbalimbali ambazo Mhe. Balozi Mohamed Mtonga ameziwasilisha katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania kwa kufanyiwa kazi.







 

Wednesday, October 7, 2020

RAIS MHE.DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AMPOKEA MGENI WAKE RAIS WA MALAWI DKT. LAZARUS CHAKWERA JIJINI DAR ES SALAAM

 


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi akiongea jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati walipokuwa wakimsubiri Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam. Kushoto mwa Balozi Kijazi ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwele pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera akikagua Gwaride la Heshma lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam 



Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera akizungumza na Wanahabari (hawapo pichani) kutoka Tanzania na Malawi mara baada ya mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanahabari kutoka Tanzania na Malawi (hawapo pichani) katika mkutano na Waandishi wa Habari mara baada ya mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera


Waziri wa Mabo ya Ndani Mhe. George Simbachawene mwenye (suti ya blue) pamoja na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge (kushoto) wakiwa pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali wakifuatilia mkutano wa pamoja wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Chakwera wakati walipokuwa wakiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) Ikulu Jijini Dar es Salaam.








Tuesday, October 6, 2020

ZIARA RASMI YA KITAIFA YA SIKU TATU YA RAIS WA MALAWI DKT. LAZARUS MCCARTHY CHAKWERA

 






RAIS DKT MAGUFULI AMUANDIKIA BARUA YA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KIONGOZI MPYA WA KUWAIT

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemwandikia barua ya salamu za rambirambi Kiongozi mpya (Amir) wa Kuwait, Mtukufu Sheikh Nawaf Al-Ahmad Al-Sabah kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait hapa nchini amemkabidhi Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua iliyoandikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kwa Kiongozi mpya wa Kuwait.

Prof. Kabudi amesema Tanzania na Kuwait zina mahusiano mazuri sana na muda mrefu katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo akitolea mfano wa mfuko wa Kuwait ambao umekuwa wa msaada mkubwa katika kwa Tanzania ambao umekuwa ukisaidia katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali hapa nchini ikiwemo barabara.

Ameongeza kuwa msiba wa Kiongozi huyo wa Kuwait ni msiba wa Watanzania wote kwa kuwa kwa muda wote ambao Hayati Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah amekuwa Kiongozi wa Taifa hilo amekuwa karibu sana na Tanzania.


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait nchini, kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John akimkabidhi Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua iliyoandikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kwa Kiongozi mpya wa Kuwait


 


Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John mara baada ya kumaliza kusaini kitabu cha maombolezo 





Friday, October 2, 2020

Mradi wa Umeme wa Pamoja wa Tanzania, Burundi, Rwanda Wafikia Pazuri


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge akipokelewa na Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Mutukula, alipowasili kwenye kituo hicho kujionea shughuli zinavyoendelea.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge akikagua ubora wa mashine ya kukagulia mizigo iliyofungwa katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja cha Mutukula.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiongea na mmoja wa wafanyakazi wa Kituo cha Hudum kw Pamoja Mpakani cha Mutukula.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akisaini kitabu cha kabla ya kuanza kikao na watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Mutukula.


Mkurugenzi wa Miundombinu kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Kamugisha Kazaura akitoa maelezo namna EAC inavyoratibu upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kikanda. 




Ujenzi wa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge  akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye eneo unapojengwa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera.


Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Dkt. Jilly Maleko akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye eneo unapojengwa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera.

 Mhandisi wa Kampuni inayojenga Mtambo wa kuzalisha umeme katika Mto Kagera akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mtambo huo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiuliza maswali kwa wahandisi wanaojenga mradi wa kuzalisha umeme katika Mto Kagera.

Sehemu ya Eneo unapojengwa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera.

OSBP ya Rusumo

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akisalimiana na watumishi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo, mara baada ya kuwasili kituoni hapo kwa ziara ya kikazi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiongea na Mtalaam wa Afya katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.

Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo, Bw. Jackson Mushi akitoa taarifa ya utekelezaji wa kituo hicho kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  IbugeA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiongea na watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo

Watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo wakiwa katika kikao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge.

Mkurugenzi wa Miundombinu kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Kamugisha Kazaura na Msaidizi wa Katibu Mkuu, Bw. Hangi Mgaka wakitabasamu akati wa kikao cha briefing kwenye Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge, Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dkt. Jilly Maleko, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote pamoja na ujumbe wao akitemb kwa miguu kuelekea katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.

Malori yakiwa katika foleni ya ukaguzi katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.

Bango la kutoa elimu kuhusu wafanyabiashara wadogo wanavyoweza kufanya shughuli zao katika nchi a EAC bila usumbufu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.


 





Wednesday, September 30, 2020

AfDB Yamwaga Neema Kigoma




Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge akisalimiana na watumishi wanaofanya kazi katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja cha Kabanga kwenye Mpaka wa Tanzania na Burundi. alipowasili katika kituo hicho kwa ziara ya kikazi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge akiongea na wasafiri wanaokwenda Burundi na Uganda wanaosubiri taratibu za uhamiaji katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja cha Kabanga
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge akiongea na Afisa Uhamiaji katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja cha Kabanga kwenye Mpaka wa Tanzania na Burundi.
Kaimu Meneja wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja cha Kabanga akisoma taarifa kuhusu utendaji wa Kituo hicho.
Ujumbe uliongozana na Balozi Ibuge wakisaini Kitabu cha Wageni katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja cha Kabanga kwenye Mpaka wa Tanzania na Burundi.


Malori yakiwa katika foleni ya kusubiri ukaguzi kutoka maafisa wa Burundi ili yaendelee na safari.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge na ujumbe wake wakiwa mpakani mwa Tanzania na Burundi kwenye eneo la Kabanga.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na  watumishi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja cha Kabanga kwenye Mpaka wa Tanzania na Burundi.





Tuesday, September 29, 2020

SERIKALI YAONGEZA KASI UTEKELEZAJI WA AHADI ZA MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI KWA WANANCHI WA KIGOMA






Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kamishna wa Polisi Thobias Andeng'enye alipowasili katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kujitambulisha kabla hajaanza ziara ya ukaguzi wa miradi ya miundombinu inayoratibiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akisalimiana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Bw. Rashidi Kassim alipowasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya kujitambulisha, kabla hajaanza ziara ya kukagua miradi ya miundombinu inayoratibiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kamishna wa Polisi Thobias Andeng'enye akiwa katika kikao cha kupeana taarifa kuhusu mkoa huo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Kanali Michael Ngayalina kwenye Mpaka wa Tanzania na Burundi, Eneo la Manyovu ambapo kutajengwa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP). 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Kanali Michael Ngayalina pamoja na ujumbe wao wakikagua Eneo litakalojengwa kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani mwa Tanzania na Burundi katika miji ya Manyovu/Mugina.

Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Kanali Michael Ngayalina akimuonesha jiwe linalotenganisha Mpaka wa Tanzania na Burundi lililopo kwenye Mji wa Manyovu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akimsikiliza Mshauri Mwelekezi wa ujenzi wa mradi wa Barabara kutoka Kasulu hadi Kibondo ambao unajengwa na Mkandarasi kutoka China kwa fedha za mkopo nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Mipango na Miundombinu, Mhandisi Steven Mlote (Kulia) akiwasikiliza wakandarasi kutoka China wanaojenga barabara inayounganisha Tanzania na Burundi kutoka Kasulu hadi Kibondo.

Bi. Edna Chuku akibadilishana mawzo na Mhandisi wa TANROADS wa Mkoa wa Kigoma walipokuwa kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert A. Ibuge akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Kambi ya Wakimbizi ya Nduta iliyopo mkoani Kigoma. Sehemu ya Kambi hiyo itapitiwa na barabara inayounganisha Tanzania na Burundi.