Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemwandikia barua ya
salamu za rambirambi Kiongozi mpya (Amir) wa Kuwait, Mtukufu Sheikh Nawaf
Al-Ahmad Al-Sabah kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu
Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah.
Waziri wa
mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi
mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait hapa
nchini amemkabidhi Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua
iliyoandikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli kwenda kwa Kiongozi mpya wa Kuwait.
Prof.
Kabudi amesema Tanzania na Kuwait zina mahusiano mazuri sana na muda mrefu
katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo akitolea mfano wa mfuko wa Kuwait ambao
umekuwa wa msaada mkubwa katika kwa Tanzania ambao umekuwa ukisaidia katika
ujenzi wa miundombinu mbalimbali hapa nchini ikiwemo barabara.
Ameongeza
kuwa msiba wa Kiongozi huyo wa Kuwait ni msiba wa Watanzania wote kwa kuwa kwa
muda wote ambao Hayati Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah amekuwa
Kiongozi wa Taifa hilo amekuwa karibu sana na Tanzania.
|
Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John
akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait nchini, kufuatia kifo
cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber
Al-sabah.
|
|
Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John akimkabidhi
Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua iliyoandikwa na
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwenda
kwa Kiongozi mpya wa Kuwait |
|
Balozi
wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan akiongea na Waziri wa Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John mara baada ya
kumaliza kusaini kitabu cha maombolezo |