Friday, July 9, 2021

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA KENYA BALOZI RAYCHELLE OMAMO AFANYA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MOJA NCHINI KUTEKELEZA MAAGIZO YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN NA UHURU KENYATTA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiteta jambo na Balozi Wa Kenya Nchini Tanzania Balozi Dany Kazungu (kushoto) na Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dkt. John Simbachawene (kulia) wakati wakimsubiri Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo anayetarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku moja hapa Nchini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku moja 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo mara baada ya kuwasili Nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo katika mazungumzo ya faragha kabla ya kuanza kwa mazungumzo rasmi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika mazungumzo rasmi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo. Mazungumzo hayo yamehudhuriwa pia na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine na Viongozi,Maafisa waandamizi wa Wizara za Mambo ya Nje wa Kenya na Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) barua rasmi ya mualiko wa kutembelea Kenya 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo walipokutana na kufanya mazungumzo na Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake wa Tanzania
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Wafanyabiasahara na Wajasiriamali Wanawake wa Tanzania (hawapo pichani) Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo na kushoto ni Bi Angelina Ngalula Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF)
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake. Aliyekaa Kushoto kwa Balozi Mulamula ni Bi Angelina Ngalula Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akigonga glasi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo kupongezana wakati akihitimisha ziara yake ya siku moja ya kikazi hapa nchini (Aliyevaa koti ni Bi Angelina Ngalula Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) 


 

Thursday, July 8, 2021

BALOZI MULAMULA ASHIRIKI MKUTANO 112 WA BARAZA LA MAWAZIRI WA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA NCHI ZA AFRIKA,CARIBBEAN NA PACIFIC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wa 112 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Nchi za Afrika,Caribbean na Pacific  unaofanyika kwa njia ya mtandao 

Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Mhandisi Zena Ahmed Said akifuatilia mjadala katika Mkutano wa 112 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Nchi za Afrika,Caribbean na Pazific unaofanyika kwa njia ya mtandao - Dar es Salaam

Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Mhandisi Zena Ahmed Said (kushoto) akiwa na Kamishna wa fedha za Nje wa Wizara ya feda na Mipango Bi Sauda Msemwa (katikati) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Bw. Hassan Mwamweta wakifuatilia mjadala katika Mkutano wa 112 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Nchi za Afrika,Caribbean na Pazific unaofanyika kwa njia ya mtandao - Dar es Salaam




 

TANTRADE, BALOZI ZA TANZANIA ZAELEKEZWA KUTANGAZA FURSA ZA BIASHARA

Na Mwandishi wetu, Dar

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imeelekezwa kushirikiana na Balozi za Tanzania katika kutangaza fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji hapa nchini.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

“…………….Balozi zetu zina uhusiano wa karibu na TanTrade ambapo TanTrade moja kati ya majukumu yake ni kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wetu hapa nchini wanapata taarifa sahihi ili kusaidia kujua ni bidhaa gani za Tanzania zinaweza kuuzwa nje kwa urahisi lakini pia kujua ni nchi husika yenye uhitaji wa bidhaa hizo,” amesema Balozi Fatma 

Balozi Fatma ameongeza kuwa ili bidhaa za Tanzania ziendelee kuuzwa katika masoko ya kimataifa ulimwenguni, TanTrade iendelee kushirikiana kwa karibu na Balozi za Tanzania katika kuhakikisha kuwa inatoa taarifa sahihi za bidhaa.

“Ushirikiano baina ya TanTrade na Balozi zetu uendelee kuimarishwa ili kuwawezesha wafanyabiashara kupata taarifa sahihi na kwa wakati, lakini pia ushirikiano huu utasaidia kutangaza fursa za biashara zilizopo nchini Tanzania katika Mataifa ya Kigeni,” amesema Balozi Fatma

Balozi Fatma pia ametoa wito kwa watanzania kutumia fursa ya maonesho ya Sabasaba kujifunza kutoka kwa wafanyabiashara kutoka nje ya Nchi walioshiriki katika maonesho hayo ili kujua ni kwa namna gani wataweza kunufaika na fursa za kuuza bidhaa zetu kwenye nchi za kimataifa

“Kupitia maonesho haya watanzania watumie fursa hii kujifunza kutoka kwa wafanyabiashara kutoka nje ya Nchi walioshiriki katika maonesho haya, lakini pia kuangalia ni namna gani watanufaika na fursa za kuuza bidhaa zetu kwenye nchi za kimataifa,” Amesema Balozi Fatma Rajab. 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akisaini kitabu cha wageni katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam 


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akipokea nakala ya Jarida la Diplomasia linalochapishwa na  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam 


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akimsikiliza mtumishi wa Wizara alipokuwa akimpatia maelezo juu ya baadhi ya viongozi (Mawaziri) waliohudumu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki tangu mwaka 1961 hadi sasa mwaka 2021


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akiongea na waandishi wa habari wakati alipokuwa katika banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam 


Afisa kutoka Tume ya Utalii Zanzibar akimfafanulia jambo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab wakati alipotembelea banda la tume hiyo katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam 


Afisa kutoka Bodi ya Mapato Zanzibar akimuelezea jambo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab wakati alipotembelea banda la Bodi hiyo katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam




BALOZI MULAMULA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI MKAZI WA WHO

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Tigest Ketsela Mengestu ambapo pamoja na mambo mengine wamezungumzia juu ya masuala ya mapambano dcidi ya ugonjwa wa Corona
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Tigest Ketsela Mengestu akimsikiliza mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) hayupo pichani walipokutana kwa jailli ya mazungumzo


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Tigest Ketsela Mengestu mara baada ya mazungumzo

 

Wednesday, July 7, 2021

BALOZI LIBERATA MULAMULA ASHIRIKI MKUTANO WA 23 WA KAMATI YA MAWAZIRI WA ASASI YA SIASA,ULINZI NA USALAMA YA SADC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. George Simbachawene katika mkutano wa 23 wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa,Ulinzi na Usalama (MCO) unaofanyika kwa nia ya mtandao. Nyuma ya Mawaziri hao aliyevaa barokoa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Edward Sokoine

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. George Simbachawene (Mb) wakifuatilia kwa karibu mjadala unaoendelea katika mkutano wa 23 wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa,Ulinzi na Usalama (MCO) unaofanyika kwa nia ya mtandao. Nyuma ya Mawaziri hao aliyevaa barokoa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Edward Sokoine


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. George Simbachawene (Mb) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Edward Sokoine (aliyevaa barokoa nyeupe) wakiwa pamoja na ujumbe wa Tanzania katika kutano wa 23 wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa,Ulinzi na Usalama (MCO) unaofanyika kwa nia ya mtandao



 

Tuesday, July 6, 2021

BALOZI MULAMULA AAPA KUWA MJUMBE WA BARAZA LA MAAMUZI LA EALA

Na Mwandishi wetu, Dar

Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) limemuapisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula kuwa Mjumbe wa Baraza la Maamuzi wa Bunge hilo.

Akizungumza mara baada ya kuapishwa na Spika wa Bunge hilo Mhe. Martin Ngoga leo tarehe 6 Juni 2021 katika mkutano uliofanyika kwa njia ya Mtandao jijini Dar es Salaam Balozi Mulamula amesisitiza umuhimu wa bunge hilo kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano kutokana na umuhimu  na matarajio ya Wananchi kwa Bunge hilo.

Aidha Balozi Mulamula amepongeza jitihada zinazofanywa na Bunge hilo kuendelea na vikao vyake kwa njia ya mseto ikiwa ni pamoja na kukutana ana kwa ana ama kwa njia ya mtandao licha ya changamoto ya uwepo wa ugonjwa wa UVIKO – 19 hali inayoonesha dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi.

“Wananchi wamekuwa na matarajio makubwa sana kupitia Bunge hili la Afrika Mashariki kiuweza kuona faida na mambo mazuri yanayofanyika kupitia jumuiya hii ya Afrika Mashariki,” Amesema Balozi Mulamula

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiapa kuwa Mjumbe wa Baraza la Maamuzi wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) leo tarehe 6 Juni 2021 katika mkutano uliofanyika kwa njia ya Mtandao jijini Dar es Salaam 



Monday, July 5, 2021

DKT. MPANGO: WIZARA NA BALOZI ENDELEENI KUAINISHA, KUTANGAZA FURSA

Na Mwandishi wetu, Dar

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango ameitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Balozi za Tanzania kuainisha na kutangaza fursa mbalimbali zilizopo nchini hususani biashara na uwekezaji.

Dkt. Mpango ametoa maelekezo hayo alipotembelea banda la Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lililopo katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam. Mara baada ya kuwasili katika banda la Wizara, Dkt. Mpango amepokelewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.

“Naipongeza Wizara kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia ……..lakini pia Wizara iendelee kuzishirikisha Balozi zetu katika kutangaza fursa mbalimbali zilizopo nchini, na Balozi hizo ziainishe fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye nchi za uwakilishi kwa ajili ya Watanzania,” Amesema Dkt. Mpango

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Mpango ameielekeza Wizara ya Maambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuendelea kuboresha majukumu ya Wizara ikiwa ni pamoja na balozi za Tanzania na Taasisi zake.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango akiongea na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk pamoja na watumishi wa Wizara wakati alipotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango akiongea na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk pamoja na watumishi wa Wizara wakati alipotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na watumishi wa Wizara wakati alipotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam 

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na watumishi wa Wizara wakati alipotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Geoffrey Mwambe (Mb) akipokea nakala ya Jarida la Diplomasia linalochapishwa na  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam 

 

Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Ibrahim Mmbaga akifafanua jambo kwa mwananchi aliefika kwenye banda la Wizara katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es salaam








BALOZI MULAMULA ATEMBELEA MAONESHO YA SABSABA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) alipowasili katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere kutembelea maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kujionea shughuli zinazoendelea katika maonesho hayo


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika banda la Chuo cha Diplomasia alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam

 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Emmanuel Buhohela akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika picha moja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam











Saturday, July 3, 2021

MAREKANI YAADHIMISHA MIAKA 245 YA UHURU

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisalimiana na Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright mara baada ya kuwasili katika makazi ya Balozi huyo Dar Es Salaam kushiriki katika hafla ya miaka 245 ya Uhuru wa marekani
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa pamoja na Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright wakiimba wimbo wa Taifa la Marekani katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani. Hafla hiyo imefanyika katika makazi ya Balozi huyo Jijini Dar Es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa pamoja na Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright wakiimba wimbo wa Taifa la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania wakati wa maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani. Hafla hiyo imefanyika katika makazi ya Balozi huyo Jijini Dar Es Salaam
Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright akisoma risala katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi huyo. Kushoto aliyekaa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) ambale ni mgeni rasmi katika maadhimisho hayo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiinua glasi dhidi ya Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright ikiwa ni ishara ya kutakiana heri katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi huyo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb)akisoma risala katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright

Hadhira  ya Wageni waalikwa katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb)