Friday, July 9, 2021

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA KENYA BALOZI RAYCHELLE OMAMO AFANYA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MOJA NCHINI KUTEKELEZA MAAGIZO YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN NA UHURU KENYATTA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiteta jambo na Balozi Wa Kenya Nchini Tanzania Balozi Dany Kazungu (kushoto) na Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dkt. John Simbachawene (kulia) wakati wakimsubiri Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo anayetarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku moja hapa Nchini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku moja 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo mara baada ya kuwasili Nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo katika mazungumzo ya faragha kabla ya kuanza kwa mazungumzo rasmi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika mazungumzo rasmi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo. Mazungumzo hayo yamehudhuriwa pia na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine na Viongozi,Maafisa waandamizi wa Wizara za Mambo ya Nje wa Kenya na Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) barua rasmi ya mualiko wa kutembelea Kenya 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo walipokutana na kufanya mazungumzo na Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake wa Tanzania
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Wafanyabiasahara na Wajasiriamali Wanawake wa Tanzania (hawapo pichani) Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo na kushoto ni Bi Angelina Ngalula Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF)
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyabiashara na Wajasiriamali Wanawake. Aliyekaa Kushoto kwa Balozi Mulamula ni Bi Angelina Ngalula Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akigonga glasi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Raychelle Omamo kupongezana wakati akihitimisha ziara yake ya siku moja ya kikazi hapa nchini (Aliyevaa koti ni Bi Angelina Ngalula Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) 


 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.