Wednesday, July 28, 2021

WAZIRI MULAMULA AMUAGA BALOZI WA UHOLANZI

 Na mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amemuaga Balozi wa Uholanzi nchini, Mhe. Jeroen Verheul ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi.

Balozi Mulamula amempongeza Balozi Verheul kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kudumisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Uholanzi na Tanzania wakati wote wa uwakilishi wake hapa nchini.

“Tanzania tunakuahidi ushirikiano lakini pia tunakutakia kila la kheri katika maisha yako nje ya Tanzania na ni imani yangu kuwa utakuwa balozi mzuri wa Tanzania duniani," Amesema Balozi Mulamula

Balozi wa Uholanzi aliyemaliza muda wake wa Uwakilishi Mhe. Verheul ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano iliompatia wakati wote alipokuwa akitekeleza majukumu yake ya uwakilishi hapa nchini.

“Nawashukuru sana kwa ushirikiano mlionipatia wakati wote niliokuwa hapa nikitekeleza majukumu yangu kama Balozi, hakika nilifarijika sana……….Ninawaahidi kuwa balozi mwema kote niendako,” Amesema Balozi Verheul

Katika tukio jingine, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao walijadili masuala ya kukuza, kuimarisha na kudumisha uhusiano mzuri uliopo baina ya Tanzania na UAE.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Balozi wa Uholanzi nchini, Mhe. Jeroen Verheul wakati wa hafla ya kumuaga mara baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. 


Balozi wa Uholanzi nchini, Mhe. Jeroen Verheul akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Libarata Mulamula akimkabidhi moja kati ya zawadi Balozi wa Uholanzi nchini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi nchini, Mhe. Jeroen Verheul


Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Libarata Mulamula wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Libarata Mulamula akiongea na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Libarata Mulamula na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) hapa nchini Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi yakiendelea



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.