Monday, July 5, 2021

BALOZI MULAMULA ATEMBELEA MAONESHO YA SABSABA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) alipowasili katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere kutembelea maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kujionea shughuli zinazoendelea katika maonesho hayo


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika banda la Chuo cha Diplomasia alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam

 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Emmanuel Buhohela akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika picha moja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam











Saturday, July 3, 2021

MAREKANI YAADHIMISHA MIAKA 245 YA UHURU

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisalimiana na Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright mara baada ya kuwasili katika makazi ya Balozi huyo Dar Es Salaam kushiriki katika hafla ya miaka 245 ya Uhuru wa marekani
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa pamoja na Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright wakiimba wimbo wa Taifa la Marekani katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani. Hafla hiyo imefanyika katika makazi ya Balozi huyo Jijini Dar Es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa pamoja na Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright wakiimba wimbo wa Taifa la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania wakati wa maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani. Hafla hiyo imefanyika katika makazi ya Balozi huyo Jijini Dar Es Salaam
Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright akisoma risala katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi huyo. Kushoto aliyekaa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) ambale ni mgeni rasmi katika maadhimisho hayo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiinua glasi dhidi ya Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright ikiwa ni ishara ya kutakiana heri katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi huyo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb)akisoma risala katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright

Hadhira  ya Wageni waalikwa katika maadhimisho ya miaka 245 ya Uhuru wa Taifa la Marekani yaliyofanyika Jijini Dar Es Salaam katika makazi ya Balozi wa Marekani hapa Nchini Dkt. Donald Wright wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb)

Friday, July 2, 2021

BALOZI SOKOINE: WAFANYABIASHARA TUMIENI BALOZI ZA TANZANIA

Na Mwandishi wetu, Dar

Wafanyabiashara nchini wanaofanya biashara nje ya nchi wameshauriwa kuwasiliana na balozi za Tanzania ili kupata taarifa sahihi kuhusu fursa za biashara na uwekezaji katika nchi wanazopenda kufanya nazo biashara.

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Balozi Sokoine amesema kuwa endapo wafanyabiashara watatumia Balozi za Tanzania Nje ya Nchi itakuwa rahisi kwao kuwapatia taarifa sahihi zaidi kuliko kutumia vyanzo vingine.

“Endapo wafanyabiashara wetu wanaofanya biashara nje watatumia fursa ya kuwasiliana na Wizara ya Mambo ya Nje kupitia Balozi zake Nje ya Nchi watapatiwa taarifa sahihi ambazo zitawasaidia kuokoa muda na kupata bidhaa kwa wakati,” Amesema Balozi Sokoine.

Pamoja na mambo mengine, Balozi Sokoine amewasihi watanzana kwa ujumla kupita katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje ili kuweza kupata uelewa wa taarifa/ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kidiplomasia.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Joseph Sokoine akisaini kitabu cha wageni katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Joseph Sokoine akimsikiliza Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bw. Emmanuel Buhohela katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade  Balozi Mteule, Mhe. Edwin Rutageruka.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Joseph Sokoine akiongea na waandishi wa habari katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Joseph Sokoine, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade  Balozi Mteule, Mhe. Edwin Rutageruka na Mwakilishi kutoka chuo cha Diplomasia, Mhe. Balozi Innocent Shio wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Joseph Sokoine akipata ufafanuzi kutoka banda la magazeti ya Serikali (TSN) wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Joseph Sokoine akiwa katika banda la Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) wakati alipotembelea Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam 















WIZARA YA MAMBO NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI YAVUTIWA NA KASI YA UJENZI WA SGR


Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inajivunia na kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi wa reli mpya ya kisasa (Standard Gauge Railway - SGR) unaoendelea katika hatua mbalimbali nchini. 

Haya yamesemwa na Bw. Eliabi Chodota Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii,alipotembelea mradi huo ambao kwa sasa ndio mradi pekee mkubwa wa reli ya kisasa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ameongeza kuwa mradi huu sio tu ni muhimu kwa Tanzania bali utazinufaisha pia nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi zingine jirani. Bwana Chodota pia ameeleza kuridhishwa kwake na ushiriki wa Watanzania katika katika ujenzi wa mradi huo, ambapo kati ya Wafanyakazi zaidi ya 6000, zaidi ya asilimia 80 ni Watanzania. 

Bwana Chodota ametembelea maradi huo unaotekelezwa katika awamu tano (5) kama ifuatavyo: sehemu ya awamu ya kwanza Kilomita 202 (Dar es Salaam-Morogoro), awamu ya pili Kilomita 348 (Morogoro – Makutopora) awamu ya tatu Kilomita 294 (Makutopora-Tabora) awamu ya nne (Tabora-Isaka), na sehemu ya awamu ya tano Kilomita 341 (Isaka-Mwanza) kwa lengo la kujionea hatua ya maendeleo iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Mradi huu wa SGR, unaoendelea kujengwa kwa kasi, baada ya kukamilika kwake unatarajiwa kuiunganisha Tanzania na nchi jirani za Rwanda na Uganda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Reli hii mpya inatarajiwa kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya usafiri na usafirishaji nchini kwa kupunguza msongamano barabarani, kupunguza muda wa kusafiri na kupunguza uharibifu wa miundombinu ya barabara. Sambamba na hayo, pia inatarajiwa kupunguza gharama za usafirishaji kwa 40%. Kila treni ya mizigo inatarajiwa kusafirisha hadi tani 10,000 kiasi ambacho kinaweza kusafirishwa na malori 500 kwa njia ya barabara.

Bwana Chodota ametoa rai kwa Watanzania hasa ambao wanazunguka eneo la mradi kuendelea kutoa ushirikiano kwa mamlaka na Mkandarasi ili kuendelea kuruhusu kasi ujenzi wa mradi iendelee na kuweka mazingira rafiki na salama kwa mradi huo wakati wote.
Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Bw. Eliabi Chodota (wa kwanza kushoto) wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa katika kituo cha reli ya kisasa SGR cha mjini Morogoro muda mfupi baaada ya kuwasili katika kituo hicho. Wengine pichani ni Watumishi wa Wizara na Shirika la Reli Nchini.
Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Bw. Eliabi Chodota (wa kwanza kulia) akifuatilia maelezo ya Waandisi wa ujenzi wa mradi wa SGR.
Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Bw. Eliabi Chodota (wa pili kushoto) akifuatilia maelezo ya Waandisi wa ujenzi wa mradi wa SGR katika Kituo Kikuu cha mradi huo jijini Dar es Salaam
Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Bw. Eliabi Chodota (mwenye tai) akiwa na baadhi ya watumishi wa Wizara na Shirika la Reli nchini kwenye kituo cha SGR cha Soga.
Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Bw. Eliabi Chodota (mwenye tai) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Wizara aliombatana nao katika ziara ya kutembelea mradi wa SGR.

Thursday, July 1, 2021

MHE WAZIRI MULAMULA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA JAJI WA MAHAKAMA YA AFRIKA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Jaji wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu iliyopo Arusha, Mhe. Tujilane Chizumila alipomtembelea Ofisi kwake jijini Dodoma leo tarehe 1 Julai 2021 kwa ajili ya kumsalimia na kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Waziri. 


Mhe. Waziri akimsikiliza Mhe. Jaji Chizumila wakati wa mazungumzo kati yao

Mazungumzo yakiendelea

Mhe. Waziri akimweleza jambo Mhe. Jaji Chizumila mara baada ya kumaliza mazungumzo kati yao



 

BALOZI SOKOINE AKUTANA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MKAZI WA (PEACE CORPS)

 Na Mwandishi wetu, Dar

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Wafanyakazi wa Kujitolea la Kimarekani (Peace Corps) Bibi. Stephanie Joseph de Goes kwa lengo la kujitambulisha na kuelezea maandalizi ya ujio wa wafanyakazi  wa kujitolea wa Shirika hilo kutoka Marekani.

Bibi. Stephanie Joseph de Goes amemueleza Balozi Sokoine kuwa wafanyakazi hao wanatarajiwa kuwasili hapa nchi kwa ajili ya kufanya kazi katika maeneo mbalimbali yenye uhitaji.

Pamoja na Mambo mengine, Katibu MKuu Balozi Sokoine amemhakikishia Mkurugenzi Mkazi huyo ushirikiano na kwamba Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki iko tayari kuratibu utendaji wa shirika hilo hapa nchini kwa kushirikiana na Wizara nyingine za Kisekta zinazoguswa kiutendaji na Shirika hilo kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Wafanyakazi wa Kujitolea la Kimarekani (Peace Corps) Bibi. Stephanie Joseph de Goes katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Wafanyakazi wa Kujitolea la Kimarekani (Peace Corps) Bibi. Stephanie Joseph de Goes katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Wafanyakazi wa Kujitolea la Kimarekani (Peace Corps) Bibi. Stephanie Joseph de Goes akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine Ripoti ya Mwaka ya Shirika hilo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Wafanyakazi wa Kujitolea la Kimarekani (Peace Corps) Bibi. Stephanie Joseph de Goes akiagana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine mara baada ya kumalizika kwa maongezi yao



Monday, June 28, 2021

MAKONSELI WAKUU WA MSUMBIJI NA OMAN WAWASILISHA BARUA ZA UTAMBULISHO

 Na mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula apokea nakala ya barua za utambulisho za Makonseli Wakuu wawili kutoka Msumbiji na Oman wenye makazi Zanzibar.

Makonseli hao ni Mhe. Agustinho Abacar Trinta Konseli Mkuu wa Msumbiji pamoja na Mhe. Said Salim Al Sinawi Konseli Mkuu wa Oman

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao wamedajiliana masuala mbalimbali ya kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia na Kiuchumi baina ya nchi zao na Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokea nakala ya barua za utambulisho kutoka kwa Konseli Mkuu wa Msumbiji mwenye makazi Zanzibar Mhe. Agostinho Abacar Trinta katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Konseli Mkuu wa Msumbiji mwenye makazi Zanzibar Mhe. Agostinho Abacar Trinta katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasilisha nakala ya hati za utambulisho   


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokea nakala ya barua za utambulisho kutoka kwa Konseli Mkuu wa Oman mwenye makazi Zanzibar Mhe. Said Salim Al Sinawi. Uwasilishwaji wa hati hizo umefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam 


Konseli Mkuu wa Oman mwenye makazi Zanzibar Mhe. Said Salim Al Sinawi akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasilisha nakala ya hati za utambulisho      



TANZANIA KUNUFAIKA SOKO ENEO HURU LA BIASHARA AFRIKA

Na Mwandishi wetu, Dar

Serikali ya Tanzania inategemea kunufaika na soko la bidhaa zake katika masoko ya nje baada ya kusainiwa kwa Mkataba wa ushiriki katika Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA).

Akiongea na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCTA) Mhe. Wamkele Mene, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amesema kwa sasa Serikali ipo katika hatua za mwisho kusaini Mkataba wa AfCTA.

“Lengo la ziara ya Mhe. Mene hapa nchini pamoja na mambo mengine ni kukutana na viongozi na wadau wengine muhimu kujadiliana na masuala mbalimbali yanayohusu Mkataba wa AfCTA ikiwa ni pamoja na umuhimu wa Tanzania kuridhia Mkataba huo,” Amesema Balozi Mulamula

Balozi Mulamula ameongeza kuwa, uanzishwaji wa AfCTA ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa ambapo pamoja na mambo mengine, utekelezaji wake unatarajiwa kuongeza wigo wa fursa nafuu za biashara nchini kwa kuwavutia wawekezaji na kuongeza mauzo hasa ya bidhaa za kilimo.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Sekretariati ya Eneuo Huru la Biashara Afrika (AfCTA) Mhe. Wamkele Mene ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano ambao imempatia tangu wakati wa uchaguzi hadi sasa na kuahidi kuwa utekelezaji wa Mkataba huo utanufaisha kila Nchi Mwanachama.

“……….Naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwani tangu ilipoingia Madarakani imetumia muda mfupi katika kushiriki kwa ukamilifu katika majadiliano ya kusaini mkataba huu na Tanzania imeshiriki vizuri sana kwenye majadiliano haya muhimu,” Amesema Mhe. Wene

Ameongeza kuwa kwa sasa Eneo Huru la Biashara Afrika lina Nchi wanachama 38 ambazo zimekubaliana na Mkataba huo na kwamba kwa sasa Sekretariati hiyo inaendelea kuimarika katika kukuza biashara na sekta binafsi katika nchi wanachama wa AfCTA.

Mkataba wa Eneo Huru la Biashara Afrika umesainiwa na Nchi 54 kati ya nchi 55 za Umoja wa Afrika ikiwemo Tanzania. mkataba huo ulipata nguvu ya Kisheria Julai, 2019 baada ya nchi 28 kuridhia Mkataba huo. Mkataba wa AfCTA unahusisha maeneno ya ushirikiano katika bishara ya bidhaa, biashara ya huduma, uwekezaji, hakimiliki na ubunifu pamoja na Sera za ushindani.

Katika tukio jingine, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameshiriki uzinduzi wa Kongamano la Usawa wa Kijinsia ambapo pamoja na mambo mengine, Balozi Mulamula kongamano hili litakuwa mahsusi kuangalia masuala ya uswa wa jinsia kwa kizazi hiki na kizazi kijacho na kwamba wakuu wa Nchi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa watakuatana Ufaransa katika kongamano hilo kuanzia tarehe 30 Juni hadi 2 Julai 2021.

Balozi Mulamula ameongeza kuwa, Tanzania itashiriki katika kongamano hilo ambapo Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan atawakilishwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango

Uzinduzi wa Kongamano la Usawa wa Kijinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam umehudhuriwa na Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Fredric Clavie pamoja na Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Bibi Hodan Addou.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongea na waandishi wa Habari wakati alipokutana na Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA) Mhe. Wamkele Mene leo Jijini Dar es Salaam


Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA) Mhe. Wamkele Mene akiongea na waandishi wa Habari wakati wa Mkutano baina yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb)uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam


Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA) Mhe. Wamkele Mene akiongea na waandishi wa Habari wakati wa Mkutano baina yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb)uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam


Mkutano ukiendelea


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akihutubia wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Usawa wa Kijinsia ulifanyika Jijini Dar es Salaam  


Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mhe. Fredric Clavie akihutubia wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Usawa wa Kijinsia ulifanyika Jijini Dar es Salaam  


Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Bibi Hodan Addou akihutubia wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Usawa wa Kijinsia Jijini Dar es Salaam 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb), Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mhe. Fredric Clavie pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Bibi Hodan Addou wakiwa katika picha ya pamoja