Thursday, December 9, 2021

RAIS SAMIA AWAONGOZA WATANZANIA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaongoza Watanzania kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Marais na viongozi wa Mataifa mbalimbali pamoja na viongozi wakuu wa Serikali.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia Watanzania kwenye sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam  


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam  


Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam  


Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete katika sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam    


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Hussein Ali Mwinyi akiwasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara  


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akihutubia wananchi katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam   


Baadhi ya Mawaziri na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi Pamoja na Viongozi waandamizi wa Serikali wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 


Baadhi ya Makatibu Wakuu wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 

Baadhi ya Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 




Sehemu ya Mawaziri wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 





RAIS KENYATTA AWASILI NCHINI KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU NA KUANZA ZIARA RASMI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimtambulisha Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. John Simbachawene kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta wakati wa mapokezi ya Mhe. Rais Kenyatta alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimaifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 09 Desemba 2021 kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanzania Bara pamoja na kuanza ziara rasmi ya siku mbili nchini.


Mhe. Rais Kenyatta akisalimiana na Balozi wa Kenya hapa nchini, Mhe. Dani Kazungu wakati wa hafla ya mapokezi yake
Mhe. Balozi Mulamula akiendelea na zoezi la utambulisho wa viongozi mbalimbali  wa hapa nchini  waliofika kumpokea Mhe. Rais Kenyatta 

Mhe. Rais Kenyatta akisalimiana na Bi. Felister Rugambwa, Afisa Mambo ya Nje na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya ambaye yupo nchini kushiriki ziara ya Rais.

Gwaride la Heshima

Mhe. Rais Kenyatta akiwa ameongozana na Mhe. Balozi Mulamula wakipita katikati ya gwaride maalum lililoandaliwa kwa  heshima yake.

Mhe. Rais Kenyatta akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Balozi Mulamula mara baada ya kuwasili nchini

Mazungumzo yakiendelea. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Mhe. Raychaelle Omamo pamoja na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dani Kazungu.
























Wednesday, December 8, 2021

WAZIRI MULAMULA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI MBALIMBALI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula leo tarehe 08 Disemba 2021 amekutana kwa nyakati tofauti na kufanya mazungumzo na Viongozi kutoka nchi mbalimbali ambao wapo nchini kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yatakayofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 09 Desemba 2021.

Miongoni mwa Viongozi aliokutana nao ni pamoja na Rais Mstaafu wa Malawi, Mhe. Dkt. Joyce Banda, Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, Mhe. Veronica Macamo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Eswatini, Mhe. Seneta Thulisile Dladla na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Dkt. Vicent Biruta.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Balozi Mulamula amewakaribisha nchini  viongozi hao na kuwashukuru kwa kukubali mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wa kuja kushiriki maadhimisho hayo pamoja na wananchi wa Tanzania. Kadhalika, viongozi hao wamekubaliana kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zao na Tanzania kwenye maeneo mbalimbali.

Rais Mstaafu wa Malawi, Mhe. Dkt. Joyce Banda akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, Mhe. Veronica Macamo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Eswatini, Mhe. Seneta Thulisile Dladla katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Dkt. Vicent Biruta katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Mhe. Meja Jenerali Charles Karamba.    



TANZANIA YANADI BIDHAA ZA KILIMO NCHINI MAREKANI

Na Mwandishi Wetu,

Katika kusheherekea miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara na miaka 60 ya uhusiano kati ya Tanzania na Marekani, Serikali ya Tanzania kupitia Ubalozi wake nchini Marekani imefanya Kongamano kwa njia ya Mtandao kuhusu biashara ya bidhaa za Kilimo za Tanzania.

Mkutano huo umeandaliwa kwa kushirikiana na Taasisi za Kituo cha Kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Baraza la Kilimo Tanzania (ACT), Sister Cities International na Thunderbird School of Global Management. Lengo la Kongamano hilo lilikua ni kuimarisha mauzo ya bidhaa za kilimo za Tanzania nchini Marekani.

Kongamano hilo lilishirikisha wajumbe kutoka Serikali za Tanzania na Marekani, Wafanyabishara na wadau wa kilimo wa nchi hizo mbili na Taasisi za Fedha, ambapo Waziri wa Kilimo Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb), ameshiriki kwenye Kongamano hilo, kadhalika, Meya wa Jiji la   Helena-West, Arkansas, Mstahiki Kevin Smith naye pia ameshiriki.

Wakati wa Kongamano hilo, fursa mbalimbali za biashara ya mazao kati ya Tanzania na Marekani zilijadiliwa. Mazao hayo ni pamoja na maparachichi, ufuta, samaki, asali, kokoa, mchele, mvinyo, pareto, na mazao ya bahari.

Akizungumza kwenye Mkutano huo, pamoja na kueleza jitihada zinazochukuliwa na Serikali katika kuboresha sekta ya kilimo na kuongeza mauzo ya nje, Mhe. Waziri Prof. Mkenda ameeleza pia changamoto zilizopo kwenye sekta hiyo pamoja na fursa za uwekezaji pamoja na kuwasihi wawekezaji kutoka Marekani kuwekeza katika sekta ya kilimo.

Kwa upande wake, Meya Kevin Smith ameeleza kwamba Jiji lake la Helena-West linalima mchele kwa wingi na lipo tayari kushirikiana na Tanzania katika biashara ya zao hilo.

Akizungumza kwenye Kongamano hilo, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Dkt. Elsie Sia Kanza, ameeleza kuwa Kongamano hilo ni mwanzo wa makongamano mengine mengi ya namna hiyo, kwa sababu Ubalozi umejizatiti kuimarisha mauzo ya bidhaa mbalimbali za Tanzania nchini Marekani, hasa bidhaa za kilimo. Pamoja na mambo mengine, Balozi Kanza ameahidi Ubalozi utaendelea kushirikiana na mwekezaji au mfanyabiashara yeyote mwenye lengo la kuwekeza Tanzania.

Waziri wa Kilimo Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb), akiwasilisha hotuba yake kwenye Kongamano hilo lililofanyika kwa njia ya mtandao 


Balozi wa Tanzani nchini Marekani Dkt. Elsie Kanza akiwa pamoja na wajumbe wa Ubalozi wakishiriki kwenye Kongamano hilo 


Sehemu ya Wajumbe walioshiriki katika Kongamano   


Balozi Kanza akizungumza wakati wa kongamano  


Meya Kevin Smith wa Jimbo la Helena-West Arkansas, nchini Marekani akizungumza wakati wa Kongamano



Tuesday, December 7, 2021

WAZIRI MULAMULA APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MKURUGENZI MKAZI WA FAO

Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea Hati za Utambulisho za Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kupokea hati hizo Balozi Mulamula ametumia fursa hiyo kumweleza Mkurugenzi Mkazi huyo vipaumbele vya Serikali katika mpango mzima wa kuendeleza kilimo pamoja na mpango Mkakati wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ‘Strategic Development Cooperation programme’.

Pia viongozi hao wameangalia maeneo ambayo yatapewa kipaumbele katika uwekezaji wa miundombinu, uzalishaji zaidi lakini pia kuangalia jinsi gani mazao yanayolimwa yanatunzwa vizuri.

“Tumejadili mbalimbali ikiwa ni pamoja na mpango wa FAo wa kusaidia nchi kuwa na bidhaa zinazozitambulisha nchi husika katika masoko ya kimataifa,” amesama Balozi Mulamula.

Pamoja na mambo mengine, Balozi Mulamula amemhakikishia Mkurugenzi Mkazi wa FAO kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana kwa karibu na FAO katika kutekeleza miradi mbalimbali hasa mradi wa maendeleo wa miaka mitano.

Kwa Upande wake, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo amesema atahakikisha FAO inatekeleza vipaumbele vya Serikali ya Tanzania pamoja na kuongeza ushirikiano wake kwa maslahi ya pande zote mbili.

“Mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, tumejadili jinsi ya kusaidia kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi, kupunguza utapiamlo na kuona ni jinsi gani FAO inaweza kusaidia Tanzania katika kuboresha lishe kwa watanzania na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo kwa ujumla,” amesema Dkt. Tipo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akipokea Hati za Utambulisho za Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula mara baada ya kumkabidhi Hati za Utambulisho katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mwakilishi Msaidizi wa FAO Bwana Charles Tulahi akieleza jambo wakati wa kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo wakiwa katika picha ya pamoja na badhi ya maafisa kutoka Wizarani pamoja na Ofisi za FAO 




WAZIRI MULAMULA AIPONGEZA FINLAND KWA KURIDHIA MKAKATI MPYA WA USHIRIKIANO NA TANZANIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula ameipongeza Serikali ya Finland kwa kuridhia Mkakati Mpya wa ushirikiano kati yake na Tanzania kuanzia mwaka 2021 hadi 2025 ikiwa ni pamoja na mchango wa nchi hiyo kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Mhe. Waziri Mulamula alipozungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 104 ya uhuru wa Taifa la Finland yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 06 Desemba 2021 na kuhudhuriwa na wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo Mabalozi na Wakauu wa Mashirika ya Kimataifa waliopo nchini.

Balozi Mulamula amesema kuwa, kuridhiwa kwa mkakati huo mpya wa ushirikiano kati ya Tanzania na Finland kunadhihiridha jinsi ambavyo nchi hiyo imedhamiria kuendelea kushrikiana na Tanzania ili kuiwezesha kukamilisha agenda na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa hapa nchini kwa ushirikiano na nchi hiyo.

“Tanzania inatoa shukrani kwa Serikali ya Finland kwa kuridhia Mkakati Mpya wa Ushirikiano na Tanzania kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Kuridhiwa kwa Mkakati huu kunadhihirisha namna ambavyo Serikali ya Finland ipo tayari kuendelea kushirikiana na Tanzania ili kuwezesha utekelezaji wa agenda za maendeleo zilizopo” amesema Waziri Mulamula.

Balozi Mulamula amesema kwamba, katika kipindi cha miaka 56 ya ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Finland, nchi hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya nchi hii kwa kuchangia miradi ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali zikiwemo elimu, utunzaji wa mazingira na misitu, nishati, TEHAMA na program za kuwawezesha wanawake kiuchumi. 

Ameongeza kusema kuwa, miongoni mwa masuala muhimu ya kupigiwa mfano kwenye ushirikiano huu ni pamoja na nchi hiyo kuwezesha kuanzishwa kwa Mpango wa Kuboresha ukusanyaji Kodi ambao kwa kiasi kikubwa umechangia kuongezeka kwa ukusanyaji mapato ya ndani hapa nchini. Pia, Finland kupitia Mchakato wa Helsinki kuhusu masuala ya utandawazi na demokrasia, uliwezesha kuanzishwa kwa Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute) ambayo hutoa mafunzo kwa viongozi waaandamizi serikalini na wadau mbalimbali katika kuwajengea uwezo wa utendaji kazi zao za kila siku.

Katika kuwawezesha wanawake kiuchumi, Balozi Mulamula amesema, Serikali ya Finland kupitia ubalozi wake hapa nchini umeanzisha program mbalimbali za kuwawezesha wanawake kujikwamua kiuchumi ikiwemo ile ya “Wanawake Wanaweza”.

Kwa upande wake, Balozi wa Finland hapa nchini, Mhe. Riitta Swan amesema nchi yake itaendelea kushirikiana na Serikali kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo na kuipongeza Tanzania Bara inapoelekea kusherehekea miaka 60 ya uhuru.

Tanzania na Finland zilianzisha rasmi ushirikiano wa kidiplomasia mwaka 1965.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza kama mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya miaka 104 ya uhuru wa Taifa la Finland yaliyofanyika tarehe 06 Desemba 2021 jijini Dar es Salaam. Maadhimisho hayo ambayo yaliandaliwa  na Balozi wa Finland hapa nchini, Mhe. Riita Swan, yalihudhuriwa pia na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa waliopo nchini.
Sehemu ya Mabalozi na wageni waalikwa wakimsikiliza Mhe. Balozi Mulamula (hayupo pichani) akizungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 104 ya uhuru wa Taifa la Finland. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme.

Balozi wa Finland nchini, Mhe. Riitta Swan akizungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 104 ya uhuru wa Finland.

Sehemu ya Mabalozi na wageni waalikwa wakimsikiliza Mhe. Baloz Swan (hayupo) pichani.

Mhe. Balozi Mulamula na Mhe. Balozi Swan pamoja na wageni waalikwa wakiwa wametulia wakati nyimbo za Taifa la Finland na Tanzania zikiimbwa kuadhimisha miaka 104 ya uhuru wa Taifa la Finland.


Maafisa kutoka Ubalozi wa Finland wakiimba wimbo kwa Lugha ya Kifini kuwaburudisha wageni waalikwa wakati wa maadhimisho ya miaka 104 ya Taifa la Finland
Mhe. Waziri Mulamula akiwa ameongozana na mume wake, Dkt. George Mulamula wakipokelewa na Balozi wa Finland nchini, Mhe. Riitta Swan pamoja na mume wake walipowasili Ubalozi wa Finland kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 104 ya Finland.


 

Monday, December 6, 2021

MKUTANO WA 21 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA KISEKTA LA AFYA WA EAC UMEFUNGULIWA MJINI ZANZIBAR

Mkutano wa 21 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta (BLM) la Afya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki umefunguliwa leo tarehe 06 Desemba 2021 katika Hotel Verde mjini Zanzibar.

Mkutano huo umeanza na ngazi ya Maafisa Waandamizi kwa lengo la kuandaa taarifa zitakazowasilishwa katika mkutano wa Makatibu Wakuu na Mawaziri. Pia unafanyika ukiwa umewakutanisha nchi wanachama wote isipokuwa wajumbe wawili (Rwanda na Sudan ya Kusini) ambao wanashiriki mkutano kwa njia ya mtandao. 

Akifungua mkutano Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Sekta za Uzalishaji na Jamii, Mhe. Christophe Bazivamo ameeleza umuhimu wa mkutano wa sekta ya afya hasa wakati huu ambapo dunia imetangaza kuwepo kwa wimbi la nne la janga la UVIKO-19.

Mhe. Bazivamo amesisitiza nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki kuendelea kushirikiana na kamati ya uratibu ya UVIKO-19 ya jumuiya hiyo ili kuweza kuhakikisha tahadhari zinaendelea kutiliwa mkazo sambamba na utolewaji wa chanjo ili kuweza kudhibiti maambukizi mapya ya ugonjwa huo na kuruhusu kuendelea kwa shughuli za kiuchumi kwa ustawi wa wananchi.

“Hakuna nchi iliyo salama dhidi ya janga la UVIKO-19 kwakuwa kama nchi nyingine ndani ya jumuiya haipo salama ni hatari kwa jumuiya yetu na dunia kwa ujumla” alisema Mhe. Bazivamo

Pia alifafanua, kupitia mkutano huo nchi wanachama zitapata fursa ya kusikia taarifa zitakazowasilishwa na kila nchi ili kwa pamoja kuweza kuchangia na kushauri namna bora ya kukabiliana na janga hilo, kuwasilisha changamoto, na maoni yatakayosaidia kusimamia afya za wananchi kwa ujumla.

Vilevile masuala mtambuka yanayozigusa nchi wanachama yatapata nafasi ya kujadiliwa na kupatiwa suluhu ya pamoja. Masuala hayo ni pamoja na; taratibu za kufuatwa mipakani wakati janga la UVIKO-19 likiendelea kudhibitiwa, taratibu za upimaji wa UVIKO-19 ndani ya jumuiya, na kuwezesha usafiri huru wa wafanyakazi, huduma, ajira na bidhaa unasimamiwa kwa maslahi mapana ya jumuiya.

Mkutano huo unafanyika katika ngazi tofauti kwa utaratibu ufuatao:- Tarehe 06 -  08 Desemba 2021 ni Mkutano wa ngazi ya Watalaamu; Tarehe 09 Desemba 2021 ni Mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu; na tarehe 10 Desemba 2021 ni Mkutano wa ngazi ya Mawaziri.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa ngazi ya watalaamu umeongozwa na Dkt. Abdul S. Ali, Mganga Mkuu na Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, akishirikiana na Bw. Eliabi Chodota Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wajumbe wengine walioshiriki mkutano huo wanatoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto – Tanzania Bara, Wizara ya Afya, Ustawi wa Jami, Wazee, Jinsia, na watoto – Tanzania Zanzibar; Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia, pamoja na taasisi zilizo chini ya Wizara za Afya.

=============================================================


Mwenyekiti wa Mkutano ngazi ya Wataalamu kutoka Jamhuri ya Kenya, Dkt. Kuria Francis akiwakaribisha wajumbe katika Mkutano wa 21 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofunguliwa leo tarehe 6 Desemba 2021 katika Hotel Verde Mjini Zanzibar.

Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania ambaye pia ni Mganga Mkuu na Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt. Abdul S. Said (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota wakifatilia mkutano. 

Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mkutano.

Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania

Ujumbe kutoka Jamhuri ya Burundi

Ujumbe kutoka Jamhuri ya Kenya

Ujumbe kutoka Jamhuri ya Uganda.