Wednesday, July 26, 2023

MHE. RAIS SAMIA AFUNGUA RASMI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA KUHUSU RASILIMALI WATU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa nchi za Afrika kuwekeza zaidi katika kuboresha afya, elimu na lishe kwa watu wake ili kutengeneza rasilimali watu inayoweza kuchangia maendeleo na ukuaji wa uchumi barani Afrika.

 

Rai hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam leo tarehe 26 Julai 2023 wakati akifungua rasmi Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere.

 

Amesema Mkutano huu umetoa fursa kwa nchi za Afrika kujadili na kupanga mikakati mipya ya namna ya kutumia Rasilimali Watu ambayo Afrika imejaliwa kuwa nayo kama nyenzo muhimu katika kuchangia maendeleo na mafanikio ya Bara la Afrika.

 

Ameongeza kusema kwa upande wa Tanzania tayari mikakati mbalimbali imewekwa ya kuendeleza Rasilmali Watu ikiwemo kutenga fedha kwa ajili ya kuongeza afua za lishe na huduma za afya ya mama na mtoto ambapo amesema ameingia mkataba na Wakuu wa Mikoa kuhakikisha wanasimamia suala hili katika mikoa yao.

 

Amesema ifikapo mwaka 2050 Afrika itakuwa na asilimia 42 ya vijana duniani kote hivyo uwekezaji kwenye rasilimali watu yenye tija unahitajika ili kuwa na hatima nzuri. Amesema jitihada zaidi zinahitajika ili kuepuka kuzalisha vijana wasio na ujuzi, wasio ajirika na vijana wenye kujiingiza kwenye vitendo viovu vya kihalifu na uvunjifu wa amani.

 

Ameongeza kusema uwekezaji kwenye rasilimali watu unaanza tangu mtoto anapozaliwa kwa kumpatia lishe bora na chanjo stahiki ili kuondoa udumavu ambao husababisha upungufu wa uelewa na uwezo wa kusoma vizuri kwa watoto. Pia amesisitiza kuwekeza katika elimu ya awali ambayo ni msingi wa kuwaandaa watoto kimwili, kiakili, kihisia na kiubunifu.

 

Kadhalika ameeleza kuwa Tanzania inaendelea kuboresha utoaji huduma za jamii na kufanya maboresho ya miundombinu kama madarasa, vituo vya afya, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa sekta ya elimu na afya na kutekeleza mpango wa elimu bure kwa shule za msingi hadi sekondari.

 

Awali akizungumza, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuridhia Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano huo muhimu ambao amesema umehudhuriwa na zaidi ya Washiriki 2,500. Pia ameipongeza na kuishukuru Benki ya Dunia kwa kuandaa mkutano huo kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.

 

Amesema Mkutano huo ni jukwaa kwa nchi za Afrika kupanga mikakati bora zaidi ya kuendeleza rasilimali watu kwa maendeleo endelevu ya Bara la Afrika.

 

Naye Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwakwa amesma Benki hiyo itaendelea kushirikiana na kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanywa na Nchi za Afrika katika kuendeleza rasilimali watu ili hatimaye kuwa na maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

 

Mkutano huo ambao umehudhuriwa na Wakuu wa Nchi kutoka Nchi sita za Kenya, Madagascar, Sao Tome na Principe, Sierra Leone, Malawi na Msumbiji na wadau mbalimbali kutoka sekta binafsi naza umma umemalizika kwa kupitishwa kwa Azimio la Dar es Salaam ambalo limeainisha mikakati ya kuboresha maendeleo ya rasilimali watu barani Afrika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akifungua rasmi Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Afrika Kuhusu Rasililmali Watu uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai 2023

Mhe. Rais Samia akihutubia mkutano
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akitoa neno la utangulizi wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu kabla ya kumkaribisha Mhe. Rais Samia kufungua rasmi mkutano huo.
 
Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwakwa akizungumza wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu
 
Marais kutoka Nchi za Afrika ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu. Kutoka kushoto ni Rais wa Kenya, Mhe. William Ruto, Rais wa Malawi, Mhe. Lazarus Chakwera na Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi
 
Mhe. Rais Dkt. Samia (wa nne kushoto) akiwa na Marais walioshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu. Kutoka kushoto ni Mhe. Rais Ruto, Mhe. Rais Chakwera, Mhe. Rais Nyusi, Mhe. Rais Andry Rajoelina wa Madagascar, Mhe. Rais Carlos Vila Nova wa Sao Tome na Principe na Mhe. Rais Julius Maada Bio wa Sierra Leone

Mhe. Dkt. Tax akiteta jambo na Mhe. William Lukuvi

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akifurahia jambo kwa pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliani Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.
Mkutano ukiendelea
Wageni waalikwa wakishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila akishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.

Katibu Mkuu, Balozi Dkt. Shelukindo akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe. Mathew Mkingule wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu. Anayeshuhudia  katikati ni Balozi Kasiga

Balozi wa Afrika Kusini nchini, Mhe. Noluthando Mayende-Malepe akishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme (kushoto) akiwa Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Mteule, Iman Njalikai wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikino wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana akishiriki  Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Caesar Waitara akishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu.

Picha ya pamoja

Picha ya pamoja

Picha ya pamoja




 

Tuesday, July 25, 2023

VIONGOZI AFRIKA WAENDELEA KUWASILI NCHINI KUSHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI KUHUSU RASILIMALI WATU

Viongozi kutoka mataifa mbalimbali Barani Afrika wameendelea kuwasili nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023.

Viongozi waliowasili alfajiri ya Leo tarehe 25 Julai 2023, ni Makamu wa Rais wa Zambia, Mhe. W.K. Mutale Nalumango,  Makamu wa Rais wa Benin, Mhe. Madam Mariam Chabi Talata, Waziri Mkuu wa Eswatini, Mhe. Cleopas Sipho Dlamin, Waziri Mkuu wa Somalia, Mhe. Hamze Abdi Barre.

Wengine ni Waziri wa Elimu wa Misri, Mhe. Reda Hegazy, Waziri wa Fedha wa Djibouti, Mhe. Ilyas Moussa Dawaleh pamoja na Waziri Ofisi ya Rais  - Namibia, Mhe. Christine Hoebes.
Makamu wa Rais wa Zambia, Mhe. W.K. Mutale Nalumango akisalimiana na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023

Makamu wa Rais wa Zambia, Mhe. W.K. Mutale Nalumango akizungumza na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023

Makamu wa Rais wa Benin, Mhe. Madam Mariam Chabi Talata akipokelewa na Waziri wa Maji, Mhe. Juma Aweso baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam  kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023

Makamu wa Rais wa Benin, Mhe. Madam Mariam Chabi Talata katika mazungumzo na Waziri wa Maji, Mhe. Juma Aweso baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam  kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023

Waziri Mkuu wa Eswatini, Mhe. Cleopas Sipho Dlamin akizungumza na Waziri wa nchi Afisi ya Rais Ikulu - Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Jamal Kassim Ali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam  kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023

Waziri Mkuu wa Somalia, Mhe. Hamze Abdi Barre akifurahia jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega baada ya kuwasili nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023

Waziri wa Elimu wa Misri, Mhe. Reda Hegazy akiwa na Balozi wa Misri nchini, Mhe. Sherif Abdelhamid Ismail baada ya kuwasili kuwasili nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu kuanzia tarehe 25 - 26 Julai, 2023 





Monday, July 24, 2023

VIONGOZI MBALIMBALI WAENDELEA KUWASILI NCHINI KUSHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI KUHUSU RASILIMALI WATU

Viongozi mbalimbali kutoka Barani Afrika wameendelea kuwasili nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu utakayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar Es Salaam, tarehe 25 - 27 Julai 2023. 

Leo tarehe 24 Julai 2023, kwa nyakati tofauti viongozi mbalimbali wamewasili nchini kushiriki Mkutano huo. Viongozi waliowasili leo ni mke wa Rais wa zamani wa Msumbiji, Mama Graca Machel, Balozi wa Ivory Coast nchini Afrika Kusini, Mhe. Sakaria Kone.

Wengine ni Waziri wa Fedha wa Kenya, Mhe. Prof. Njuguna Ndug’u, Waziri wa Elimu wa Afrika Kusini, Mhe. Dr. Bonginkosi Nzimande pamoja na Waziri wa Elimu wa Togo, Mhe. Prof. Dodzi Komla Kokoroko.

Mbali ya Wakuu wa Nchi na Serikali, mkutano huo utawahusisha Mawaziri wa Fedha, Mawaziri wa Sekta nyingine zinazohusika na maendeleo ya Rasilimaliwatu, Watendaji Wakuu wa Benki ya Dunia na watu mashuhuri.
 
Mke wa Rais wa zamani wa Msumbiji, Mama Graca Machel akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Mama Machel yupo nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu utakayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar Es Salaam, tarehe 25 - 27 Julai 2023.  

Mke wa Rais wa zamani wa Msumbiji, Mama Graca Machel akizunguza na Waziri wa Nchi Utawala na Utumishi wa Umma - Msumbiji, Mhe. Ana Comoane baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Ivory Coast nchini Afrika Kusini, Mhe. Sakaria Kone akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu tarehe 25 - 27 Julai 2023 
Balozi wa Ivory Coast nchini Afrika Kusini, Mhe. Sakaria Kone akizungumza na mmoja kati ya wajumbe alioambatana na kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu tarehe 25 - 27 Julai 2023 

Waziri wa Elimu wa Togo, Mhe. Prof. Dodzi Komla Kokoroko  akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu tarehe 25 - 27 Julai 2023 
Waziri wa Elimu wa Togo, Mhe. Prof. Dodzi Komla Kokoroko  pamoja na ujumbe wake wakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Viongozi hao wapo nchini kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu tarehe 25 - 27 Julai 2023 

Waziri wa Elimu wa Afrika Kusini, Mhe. Dr. Bonginkosi Nzimande akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Rasilimali Watu tarehe 25 - 27 Julai 2023 
Waziri wa Elimu wa Afrika Kusini, Mhe. Dr. Bonginkosi Nzimande akizungmza na Balozi wa Afrika Kusini nchini, Mhe. Noluthando Mayende-Malepe katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Fedha wa Kenya, Mhe. Prof. Njuguna Ndug’u (kushoto) akizungumza na mmoja kati ya wajumbe wake katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam 

Friday, July 21, 2023

NCHI WANACHAMA WA SADC ZARIDHIA KUMUUNGA MKONO DKT. TULIA NAFASI YA URAIS UMOJA WA MABUNGE DUNIANI

Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) imeridhia kwa kauli moja kumuunga mkono mgombea wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb.), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama mgombea wa Kanda katika nafasi ya Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Luanda, Angola mwezi Oktoba 2023.

 

Hatua hiyo imefikiwa wakati wa Mkutano wa 25 wa Kamati hiyo uliofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023, baada ya Kamati hiyo kupokea na kuridhia ombi la Serikali ya Tanzania la kumuunga mkono Mhe. Dkt. Tulia lililowasilishwa kwao na Kiongozi wa Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax.

 

Aidha, wakati wa Mkutano huo, Jamhuri ya Zimbabwe ilitangaza kuwa imemuondoa kwenye kinyang’anyiro hicho mgombea wake ambaye ni Spika wa Bunge la nchi hiyo, Mhe. Jacob Mudenda ili kumuunga mkono mgombea wa Tanzania kuwania nafasi hiyo.

 

Akizungumza mara baada ya hatua hiyo, Mhe. Dkt. Tax ameishukuru Jamhuri ya Zimbabwe na Kanda kwa ujumla kwa kumuunga mkono mgombea wa Tanzania na kueleza kuwa Kanda itawezesha mgombea huyo huyo kushinda nafasi hiyo.

 

Vile vile, Mhe. Dkt. Tax ameieleza Kamati hiyo kwamba Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) tayari ameungwa mkono na Umoja wa Afrika (AU), Bunge la Afrika (PAP), Jukwaa la Maspika wa Mabunge ya Afrika Mashariki na Jukwaa la Mabunge ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC PF) katika kugombea nafasi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ambao umefanyika jijini Windhoek, Namibia  tarehe 20 na 21 Julai, 2023. Wengine wanaoishiriki ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa, kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kaspar Mmuya na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa (kushoto) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Mnyepe (katikati), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kaspar Mmuya (mwenye vifaa vya kusikilizia) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma (kulia)
Mwenyekiti wa  Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika  ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah akifunga Mkutano wa Kamati hiyo uliofanyika jijini Windhoek, Namibia tarehe 20 na 21 Julai 2023
Meza Kuu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Mhe. Dkt. Naledi Pandor naye ni miongoni mwa Mawaziri walioshiriki Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
Taratibu za kufunga rasmi Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika zikiendelea ambapo wimbo wa Taila la Namibia na Wimbo wa SADC ziliimbwa
Hafla ya kufunga mkutano ikiendelea
Mhe. Dkt. Tax  (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Bashungwa (wa tatu kushoto) mara baada ya kushiriki Mkutanoi wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika uliofanyika Windhoek tarehe 20 na 21 Julai 2023. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu wa Ulizni na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Mnyepe (wa tatu kulia), Katibu Mku wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mmuya (wa pili kushoto) na Naibu katibu mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma (kushoto)
Picha ya pamoja

Picha ya pamoja