Sunday, December 10, 2023

WAJASIRIAMALI KUTOKA NCHI WANACHAMA WA EAC WAPONGEZWA KWA KUCHANGIA MAENDELEO

Serikali za Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zitaendelea kuthamini mchango unaotolewa na sekta isiyo rasmi katika  kukuza maendeleo ya nchi hizo ikiwemo ajira.

 

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Brigedia Jenerali Salum Mnumbe wakati akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Tanzania maarufu kama Tanzania Day yaliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya shughuli za Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa.

 

Amesema kuwa Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki zilianzisha Maonesho hayo kwa kutambua na kuthamini mchango unaotolewa na sekta isiyo rasmi katika maendeleo ya nchi hizo ikiwemo kuzalisha fursa za ajira kwa wingi na kuzalisha bidhaa zinazotumiwa zaidi na wananchi.

 

“Lengo la kuanzisha maonesho hayo lilikuwa ni kuwapatia fursa wajasiriamali wa sekta hii ili waweze kushiriki katika uzalishaji na kuwawezesha kukua na kuingia kwenye sekta rasmi” amesema Brig. Jen. Mnumbe.

 

Pia amewahamasisha Wajasiriamali hao kushirikiana na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuongeza bidii katika kuzalisha bidhaa bora kwa viwango vya kimataifa na kuzitangaza bidhaa hizo ndani na nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kuongeza wigo wa soko.

 

Pia amewataka kuendelea kushirikiana, kubadilishana mawazo na ujuzi katika uzalishaji wa bidhaa na utengenezaji wa vifungashio na kuthaminisha.

 

Kadhalika ametumia fursa hiyo kuwapongeza na kuwashukuru wajasiriamali kutoka Tanzania wanaoshiriki maonesho hayo kwa kuandaa bidhaa zenye ubunifu, ubora wa hali ya juu na zenye asili ya kitanzania.

 

Maadhimisho ya Tanzania Day yaliambatana na shughuli mbalimbali zilizofanywa na wajasiriamali wa Tanzania kwa kuonesha utamaduni wa Tanzania pamoja na bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini. Miongoni mwa shuguli zilizofanywa ni pamoja na maonesho ya mavazi ya asili, ngoma za asili na muziki. 

 

Maonesho ya 23 ambayo yamewashirikisha wajasiriamali 1,500 kutoka nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wakiwemo 259 kutoka Tanzania yanafanyika kwa mara ya tatu nchini Burundi tangu kuanzishwa kwake mwaka 1999.

Mgeni Rasmi na  Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Brigedia Jenerali Salum Mnumbe akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023
Mgeni Rasmi na  Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Brigedia Jenerali Salum Mnumbe (kushoto) akiwa jukwaa kuu na wageni wengine waalikwa walioshiriki maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Bernard Haule na katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Fedha na Biashara, Bi. Annette Mutaawe.
Mgeni Rasmi, Brigedia Jenerali Mnumbe akiwa jukwaa kuu na wageni waalikwa
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Fedha na Biashara, Bi. Annette Mutaawe akitoa salamu za Sekretarieti ya Jumuiya hiyo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi


Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati Afrika Mashariki, Bw. Josephat Rweyemamu naye akizungumza
Brigedia Jenerali Mnumbe akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Fedha na Biashara, Bi. Annette Mutaawe alipotembelea banda la Sekretariei ya Jumuiya hiyo

Mgeni Rasmi na  Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Brigedia Jenerali Salum Mnumbe akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika banda la Tanzania kabla ya kuanza kwa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023

Mgeni Rasmi na  Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Brigedia Jenerali Salum Mnumbe akipata maelezo kutoka kwa Mjasiriamali wa Tanzania alipotembelea mabanda ya wajasiriamali hao wakati wa maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023

Mgeni Rasmi na  Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Brigedia Jenerali Salum Mnumbe akipata maelezo kutoka kwa Mjasiriamali wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo alipotembelea mabanda ya wajasiriamali  kutoka nchi za EAC wakati wa maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023
Watanzania wakiwa na furaha wakati wa  wa maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023
Sehemu nyingine ya Watanzania


Wajasiriamali kutoka Tanzania wanaoshiriki Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini Bujumbura wakionesha ubunifu wa mavazi mbalimbali wanayotengeza ikiwa ni shamrashara za kuadhimisha siku ya Tanzania 
Mkurugenzi wa  Ajira na Ukuzaji Ujuzi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Ally Msaki (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watanzania walioshiriki maadhimisho ya Siku ya Tanzania iliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini hapa kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023


Picha ya pamoja


WAJASIRIAMALI WAHAMASISHWA KUCHANGAMKIA SOKO HURU LA BIASHARA LA AFRIKA

 

Wajasiriamali Wadogo na wa Kati kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kuchangamkia fursa za Soko Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) kwa kujua matakwa ya kisheria ya soko hilo, kuongeza thamani ya bidhaa zao na kutumia teknolojia.

 

Rai hiyo imetolewa na Afisa Forodha Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bw. Donald Tindamanyire wakati akiwasilisha mada kuhusu “Umuhimu wa Kuwandaa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati Kuchangamkia Fusa za Soko Huru la Biashara kwa Wajasiriama” kwenye maadhimisho ya “SIKU YA TANZANIA” yaliyofanyika jijini Bujumbura tarehe 10 Desemba 2023.

 

Bw.  Tindamanyire amesema  kuwa wajasiriamali wana nafasi kubwa katika kutumia soko hilo la Afrika na kueleza kuwa kinachohitajika sasa ni wajasiriamali hao kujifunza taratibu mbalimbali zinazohitajika kwenye kulifikia soko hilo zikiwemo sheria, taratibu na kanuni za ufanyaji biashara za kuvuka mipaka ili kuepuka vikwazo vinavyoweza kujitokeza pindi wanapohitaji kulitumia soko hilo.

 

Ameongeza kusema kuwa, wajasiriamali pia wanatakiwa kuboresha na kuongeza thamani ya bidhaa zao pamoja na kutumia teknolojia ili kuzalisha kwa wingi na kuweza kuingia kwenye ushindani na nchi zingine za Afrika.

 

Kadhalika Bw. Tindamanyire ametoa wito kwa Serikali za Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwashirikisha wajasiriamali wadogo kutoa maoni kwenye uandaaji wa Itifaki  mbalimbali zinazohusu biashara za kuvuka mipaka kabla ya kuanza utekelezaji wake pamoja na kuboresha miundombinu kama barabara na reli ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa mbalimbali.

 

Pia Bw.  Tindamanyire alitumia fursa hiyo kuwahimiza wanawake na vijana kutumia fursa ya soko hilo ambalo limeandaa Itifaki Mahsusi kuhusu kundi hilo la watu engo la kuanzishwa kwa soko huru la bishara barani Afrika ni kukuza na kuimarisha biashara miongoni mwa nchi za Afrika ambayo kimsingi bado ni ndogo ukilinganisha na biashara kati ya Afrika na nchi za Asia na Ulaya.

 

Wajasiriamali 259 kutoka Tanzania wanashiriki Maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayofanyika nchini humo kuanzia tarehe 05 hadi 15 Desemba 2023. Pamoja na mambo mengine maonesho hayo hutenga siku kwa kila nchi mwanachama kujitangaza kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo utamaduni kama muziki, mavazi na vyakula.

 

Itifaki ya Soko Huru la Biashara Barani Afrika hadi sasa imeridhiwa na nchi 47 kati ya 54 za Afrika ikiwemo Tanzania na imeanza kutumika tangu mwezi Januari 2021.

Afisa Forodha Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bw. Donald Tindamanyire  akiwasilisha mada kuhusu “Umuhimu wa Kuwandaa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati Kuchangamkia Fusa za Soko Huru la Biashara kwa Wajasiriama” ikiwa ni sehemu maadhimisho ya “SIKU YA TANZANIA” yaliyofanyika jijini Bujumbura tarehe 10 Desemba 2023.

Afisa Forodha Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bw. Donald Tindamanyireakiendelea kuwasilisha mada kuhusu “Umuhimu wa Kuwandaa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati Kuchangamkia Fusa za Soko Huru la Biashara kwa Wajasiriama” kwenye maadhimisho ya “SIKU YA TANZANIA” yaliyofanyika jijini Bujumbura tarehe 10 Desemba 2023.

Wadau mbalimbali wakiwemo wajasiriamali kutoka Tanzania wakifuatilia mada kuhusu “Umuhimu wa Kuwandaa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati Kuchangamkia Fusa za Soko Huru la Biashara kwa Wajasiriama” ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya “SIKU YA TANZANIA” yaliyofanyika jijini Bujumbura tarehe 10 Desemba 2023.

Sehemu nyingine ya washiriki

Wadau wakifuatilia mada

Sehemu nyingine ya wadau wakati wa uwasilishwaji mada

Mwonekano wa mabanda ya wajasiriamali wanaoshiriki maonesho ya 23 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki
























 

Saturday, December 9, 2023

BALOZI MWAMWETA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Hassan Iddi Mwamweta amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Frank Walter Steinmeier katika Ikulu ya Nchi hiyo Jijini Berlin.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya Hati hizo Mheshimiwa Rais Frank Walter Steinmeier alifafanua kuwa Serikali yake inaunga mkono jitihada za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais was Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tanzania na Ujerumani zinashirikiana kwenye maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi ya afya; elimu; utunzaji wa mazingira; utamaduni; uhifadhi wa mazingira; utalii; biashara; uwekezaji pamoja na kubidhaisha kiswahili.

Itakumbukwa pia katika jitihada za kuimarisha ushirikiano Mheshimiwa Steinmeier alifanya ziara ya siku tatu nchini Tanzania kuanzia tarehe 30 Oktoba mpaka tarehe 1 Novemba 2023 akiwa ameambatana na ujumbe wa Makampuni mbalimbali kwa ajili ya kuangalia fursa ili kuwekeza nchini.

Pamoja na ratiba nyingine, akiwa nchini alifanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo mazungumzo ya viongozi hao yalijikita katika kuendeleza na kukuza ushirikiano wa kijamii na kiuchumi kwa maslahi ya pande zote mbili.



Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Hassan Iddi Mwamweta (kushoto) akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Frank Walter Steinmeier katika Ikulu ya Nchi hiyo jijini Berlin

Picha ya Pamoja  Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Frank Walter Steinmeier na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Hassan Iddi Mwamweta katika Ikulu ya Ujerumani jijini Berlin.

Mheshimiwa Balozi Mwamweta (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi wa Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani kutoka katika Ofisi ya Rais na Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi hiyo.

Mhe. Balozi Mwamweta akikaribishwa katika Ikulu ya Ujerumani jinini Berlin wakati wa hafla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho Utambulisho.

Mheshimiwa Balozi Mwamweta akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Ujerumani jijini Berlin.

Bendera ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikipandishwa katika Ikulu ya Ujerumani jijini Berlini kwa heshima ya Serikali ya Tanzania wakati wa hafla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho. 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Hassan Iddi Mwamweta (kushoto) akijitambulisha na kuwasilisha ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, Mheshimiwa Frank Walter Steinmeier katika Ikulu ya Nchi hiyo jijini Berlin.