Thursday, November 9, 2017

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa IFAD nchini

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Pro.Adolf Mkenda akiwa katika mzungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) inchini Bibi Abla Beuhammouche,Wizarani Jijini Dar es Salaam. Pamoja na masuala mengine mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili njia bora zaidi za kutekeleza miradi ya kilimo na uhifadhi wa mazingira. IFAD inatekeleza miradi ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo kwa wananchi na uhifadhi wa mazingira katika maeneo mbalimbali nchini.

Katibu Mkuu Prof. Adolf Mkenda akimsiliza Mkurugenzi Mkazi wa IFAD nchini Tanzania  Bibi Abla Beuhammouche walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Prof. Adolf Mkenda na Mkurugenzi Mkazi wa IFAD nchini Tanzania  Bibi Abla Beuhammouche wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.