Monday, November 13, 2017

Waziri Mahiga afanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa nchi wa Falme za Kiarabu nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Umoja wa nchi wa Falme za Kiarabu nchini Tanzania Mhe. Balozi Abdulla Ibrahim Alsuwaidi walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yalikita katika kujadili masuala mbalimbali ya namna ya kudumisha na kukuza uhusiano baina ya pande mbili. (Tanzania na Umoja wa Nchi wa Falme za Kiarabu)  
Waziri Mhe.Balozi Dkt.Mahiga na Mhe. Balozi Alsuwaidi wakifurahia jambo wakati walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akifafanua jambo wakati wa mazunguzo
Waziri Mhe. Mahiga akimsikiliza Balozi wa Nchi wa Falme za Kiarabu nchini Mhe.Abdulla Ibrahim Alsuwaidi walipokutana kwa Mazungumzo Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.