Friday, November 3, 2017

Msichana wa Kitanzania kuiwakilisha nchi Mkutano wa Dunia wa Vijana

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Deusdedit Kaganda akimkabidhi Bendera ya Taifa, Bi Hilda Jacob Mwakatumbula ambaye amechaguliwa na Kamati ya Kimataifa ya Vijana kuiwakilisha Tanzania kwenye Mkutano wa Dunia wa Vijana utakaofanyika Belize, Amerika ya Kati kuanzia tarehe 6 hadi 9 Novemba, 2017. Bi. Mwakatumbula ambaye anachukua Shahada ya Uzamivu katika Chuo Kikuu cha Waseda nchini Japan amepata ufadhili wa kushiriki Mkutano huo kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (kushoto). Akimkabidhi Bendera hiyo, Bw. Kaganda alimwomba Bi. Mwakatumbula kuwa Balozi mzuri wa Vijana wa Kitanzania kwenye mkutano huo hususan katika kutekeleza Malengo Endelevu ya Maendeleo.
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.