Wednesday, November 22, 2017

Naibu Waziri afanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Tanzania

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Korea chini Tanzania Mhe. Song, Geum-Young walipokutana  na kufanya mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mhe. Dkt. Kolimba katika mazungumzo hayo ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kuchangia katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ikiwemo eneo la afya, elimu na teknolojia. Aidha amemuhakikishia Mhe. Balozi Young kuwa Wizara na Serikali kwa ujumla wataendelea kuboresha uhusiano mzuri wa Kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Jamhuri ya Korea

Naibu Waziri Mhe.Dkt. Kolimba akimsiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea Mhe. Young, kulia ni Maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo

Mhe. Dkt. Kolimba akifafanua jambo wakati wa mazungumzo

Naibu Waziri Mhe. Dkt. Kolimba akipokea machapisho yenye ujumbe mbalimbali kutoka kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe.Young mara baada ya mazungumzo 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.